Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Merkel: Tunatofautiana wazi wazi na Trump kuhusu Korea ya Kaskazini

MTEULE THE BEST
Deutschland wƤhlt DW Interview mit Angela Merkel (DW)
Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amefanya mahojiano maalumu na DW, na kuelezea mtazamo wake kuhusu masuala kadhaa muhimu kimataifa, ukiwemo mzozo wa nyuklia wa Korea Kaskazini, na pia uchaguzi ujao nchini Ujerumani.
Katika mahojiano na DW, Kansela Angela Merkel wa Ujerumani amesisitiza kuwa lazima mzozo wa Korea Kaskazini usuluhishwe kwa njia za kidiplomasia. Na amesema Ujerumani inaweza kuwa msuluhishi katika mzozo huo.
Katika mahojiano hayo, Kansela Merkel ameikosoa hotuba iliyotolewa na Rais Donald Trump wa Marekani mbele ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Rais Trump alitishia katika hotuba hiyo, kwamba Marekani inaweza kuiangamiza kabisa Korea Kaskazini.
Kansela Merkel amesema kwamba anapinga vitisho vyovyote. ''Napinga vitisho vya aina zote. Lazima niseme maoni yangu binafsi na ya serikali, ni kwamba suluhisho la kijeshi halifai, tunapendelea juhudi za kidiplomasia. Hili lazima litekelezwe kwa dhati. Kwa maoni yangu, vikwazo na kutekeleza vikwazo hivyo ni jibu sahihi. Kitu kingine zaidi kuhusu Korea Kaskazini nadhani ni makosa. Na ni kwa sababu hiyo tunatofautiana kabisa na rais wa Marekani.'' Amesema Kansela Merkel.
Ujerumani tayari kuwa msuluhishi
Deutschland wƤhlt DW Interview mit Angela Merkel (DW)
Kansela Angela Merkel akizungumza na waandishi wa DW, Ines Pohl na Jafaar Abdul Karim
Ujerumani ni miongoni mwa nchi chache ambazo bado zina ubalozi katika mji mkuu wa Korea Kaskazini, Pyongyang, na pia ubalozi wa nchi hiyo mjini Berlin, huku pia ikiwa na mahusiano mema na China, Japan, Korea Kusini na Marekani.
Wakati huo huo, Kansela Merkel amesisitiza utayarifu wa Ujerumani kutoa mchango wake katika kuutafutia suluhisho mzozo wa Korea Kaskazini.
''Ingawa mzozo huo uko mbali nasi kijiografia, bado unaweza kuwa na athari kwetu'', amesema Kansela Angela Merkel katika mahojiano hayo maalumu na DW.
Kansela Merkel amekumbushia mazungumzo ya kuhusu mzozo wa nyuklia ya Iran, ambamo Ujerumani ilishiriki. ''Tunataka majibu ya kidiplomasia, kama tunavyofanya kuhusiana na mgogoro wan Ukraine''. Amesema Merkel, na kuongeza kuwa alimweleza hayo Rais Trump kwa njia ya simu, kabla ya hotuba ya rais huyo katika Umoja wa Mataifa mjini New York.
Uwezekano wa kuwasiliana na Kim Jong-un?
Alipoulizwa kama binafsi anaweza kuwasiliana na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un, Kansela Merkel amesema, ''Hilo haliko kwenye agenda kwa sasa, sizungumzii uamuzi ambao haujachukuliwa. 
Kansela Angela Merkel amezungumzia pia mvutano uliopo baina ya Uturuki na Ujerumani, akisema, ''Hatutaki kuhamishia matatizo ya Uturuki nchini Ujerumani''.
Na kuhusu chama cha Mbadala kwa Ujerumani, AfD ambacho kinapigiwa upatu kupata kura nyingi katika uchaguzi wa Septemba 24, Bi Merkel amesema ''kamwe siwezi kufanya kazi na chama hicho''.
Ujerumani haitaki mgogoro na Uturuki
Asema hataki matatizo ya Uturuki yahamie Ujerumani
Hivi karibuni, mzozo kati ya Ujerumani na Uturuki umekuwa ukishika kasi, lakini katika mahojiano haya, Kansela Merkel amesema Ujerumani haitaki uhasama na Uturuki. Kinachompa wasiwasi, amesema Kansela Merkel, ni uwezekano kuwa makundi ya Waturuki waishio nchini Ujerumani, yanaweza kuwa yakichunguzana. Amesema Ujerumani haiyataki hayo; ''Tutahakikisha kwamba makundi hayo yote yanaishi kwa amani hapa, bila kudhurika''. Amesema Merkel.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...