Haki miliki ya pichaIKULU YA RAIS TANZANIAImage captionRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikagua paredi ya maafisa wapya kundi la 61/16 kabla ya kuwatunuku kamisheni kuwa maafisa wa jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika Uwanja wa shekhe Amri Abeid
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amewatunuku kamisheni maafisa wapya 422 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)
Maafisa hao wametunukiwa cheo cha Luteni Usu ambapo 314 kati yao walihitimu katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi cha Monduli Mkoani Arusha, 84 wakihitimu mafunzo katika shule ya ubaharia ya kijeshi, 14 wakiwa wamehitimu mafunzo katika shule ya urubani ya kijeshi na 10 wakiwa wameiitimu mafunzo ya kijeshi nje ya nchi.
Akizungumza baada ya kuwatunuku kamisheni hizo rais Magufuli amewapongeza maafisa hao na kuwataka kuendelea kulitumia Taifa kwa kuzingatia kiapo chao.
Amesema kuwa jeshi la ulinzi limefanya kazi kubwa kulinda mipaka na kukabiliana na vitisho mbalimbali huku akisisitiza dhamira yake ya kuendelea kuliboresha ili liwe la kisasa zaidi.
Vilevile rais Magufuli amelipatia ruhusa Jeshi hilo kuajiri askari wapya 3,000 huku akiwataka raia wa taifa hilo kuliunga mkono Jeshi lao.
Rais Magufuli aidha alitumia sherehe hizo kueleza juhudi mbalimbali zilizofanywa na serikali ya awamu ya Tano tangu iingie madarakani zikiwa ni pamoja na kukabiliana na wizi na rushwa, kununua ndege 6 kwa lengo la kuimarisha usafiri na utalii, kuanza ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge), kuondoa watumishi hewa na wenye vyeti feki katika utumishi wa umma na kuongeza mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu.
Magufuli amewataka wananchi wa eneo la Arusha kuungana na juhudi mbalimbali zinazofanywa na serikali yake na kujiepusha na ushawishi unaolenga kuvuruga umoja na mshikamano hasa wakati huu ambapo Serikali imeamua kuinua uchumi na kudhibiti mianya iliyosababisha upotevu wa rasilimali za Taifa.
"Ahadi niliyoitoa wakati nawaomba kura bado ipo palepale, nitaendelea kuwatumikia watanzania wote bila kuwabagua.
"Tunataka Tanzania mpya yenye maendeleo, tumechezewa mno, wanatupa viroba wao wanakwenda kuchukua dhahabu, wanatupa viroba wao wanakwenda kuiba almasi, wanatupa viroba wao wanakwenda kuiba Tanzanite, nimesema tumechezewa vya kutosha, ni lazima sasa Watanzania tubadilike, ni lazima kila mahali alipo Mtanzania tuweke maslahi ya Tanzania kwanza, Wakati mwingine ukitaka kuwaibia watu unatumia mbinu ya kuwapumbaza na kuwafanya wagombane wao kwa wao, oooh mimi nipo CHADEMA, mimi nipo CCM, ulipozaliwa wala hukuwa na chama, niwaombe Watanzania tubadilike" alisema rais Magufuli
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni