Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya VATICAN

Mkutano wa Makardinali wa 11 ulifanyika na kiapo kwa wasaidizi wa mkutano mkuu

Picha
KILINGENI  walitoa kiapo cha usiri kabisa.  (ANSA) Conclave: maofisa na wahusika wengine walitoa kiapo cha usiri kabisa.  (ANSA) Mkutano wa 11 wa Makardinali ulifanyika jioni na mijadala kama 20 hivi ilihusiana na mada kubwa ya umuhimu wa kichungaji na kikanisa.Na wale watakaosaidia katika mkutano wa uchaguzi walitoa kiapo cha usiri kabisa kwa mujibu wa katiba ya Kitume ya Universi Dominici Gregis.Miongoni mwao mshehereshaji wa liturujia za kipapa,watu wa sakrestia,usafi,madaktari,manesi na waungamishi. Vatican News Mkutano wa 11 wa makardinali ulifanyika saa kumi na moja jioni kwa kufunguliwa na sala ya pamoja. Walikuwapo makardinali 170, miongini mwake makardinali 132 wa kupiga kura. Mijadala kama 20 hivi ilijihusiana na mada kubwa ya umuhimu wa kichungaji na kikanisa. Muda ulitolewa kwa suala la ukabila ndani ya Kanisa na  katika jamii. Uhamiaji ulijadiliwa, kwa kutambua wahamiaji kama zawadi kwa Kanisa, lakini pia kusisitiza uharaka wa kusindikizana nao na kuunga...

Kard.Re:Roho Mtakatifu aangazie makardinali kupata Papa anayehitajika kwa wakati wetu

Picha
Kardinali Re   (@Vatican Media) Katika misa kabla ya uchaguzi wa Papa mpya iliyoongozwa na Kadinali Re,Dekano wa Makardinali katika Kanisa Kuu la Vatican ameainisha kazi za kila mrithi wa Petro,kwa kuzingatia amri mpya ya upendo.Wito kwa makardinali wapiga kura:kuchagua kwa majukumu ya juu zaidi ya kibinadamu na ya kikanisa,kuepuka mawazo ya kibinafsi na kuangalia kwa manufaa ya Kanisa na ubinadamu. Na Angella Rwezaula – Vatican. Nitamwinua kuhani mwaminifu, atakayetenda sawasawa na haja za moyo wa Mungu ndiyo ilikuwa antifoni ya wimbo wa ufunguzi iliyosindikiza maandamano marefu ambayo asubuhi ya leo tarehe 7 Mei 2025 iliwaona  wakiingia makardinali wateule kwa upole kama kawaida katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican lililojaa waamini elfu tano, wakati wa Misa ya Pro eligendo Romano Pontifice, yaani kabla ya kuchagua Papa wa Roma. Aliyeongoza misa hiyo katika madhabahu ya kukiri ni Kardinali Giovanni Battista Re, Dekano wa Baraza la Makardinali. Katika mahali pa ...