Machapisho

MICHEZO

KUSAYA AONGOZA MAPOKEZI YA NDEGE YA ATCL MUSOMA

Picha
Musoma, Mara- Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Ndugu Gerald Musabila Kusaya, leo Septemba 17, 2026 ameongoza mapokezi ya ndege ya abiria ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Musoma, ikiashiria kurejea rasmi kwa safari za abiria baada ya takribani miaka minane. Safari ya mwisho ya ndege ya abiria katika kiwanja hicho ilikuwa Machi 2018 ya Shirika la Precision Air, kabla ya kufungwa kupisha upanuzi na ukarabati.  Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mara wakati wa mapokezi hayo, Kusaya amesema kurejea kwa huduma hizo ni fursa muhimu kwa uchumi wa Mkoa wa Mara. "Kurejea kwa ATCL ni fursa muhimu kwa wananchi kutokana na mchango wa usafiri wa anga katika kurahisisha usafirishaji wa watu na mizigo pamoja na kukuza biashara, utalii na uwekezaji," amesema Kusaya.  Kusaya ametoa shukrani kwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa wa kuboresha kiwanja hicho na kulipa fidia kwa wananchi 58 waliopisha ujenzi. Amewataka wananchi wa Mara na mikoa jiran...

VIBAKA WAVUNJA MAKAZI YA KADINALI ERNEST SIMONI (97) FLORENCE

Picha
Florence, Italia Tukio la kusikitisha limetokea katika Curia ya Piazza Duomo, Florence. Makazi ya Muadhama Kadinali Ernest Simoni, (97), ambaye ni MAlbania na shahidi haiwa mateso ya Kanisa chini ya utawala wa Kikomunisti wa Enver Hoxha, yamevamiwa na wezi sugu. Yaliyotokea Kwa mujibu wa gazeti la Corriere Fiorentino na shirika la habari la Adnkronos, tukio limetokea mchana wakati hakuna mtu nyumbani. Kadinali Simoni yupo London kwa mwaliko wa kukutana na Mfalme Charles III wa Uingereza, huku mpwa wake Tonin Simoni na mkewe wakiwa mgahawani kwao Borgo Albizi. Wezi walifanya kazi kwa utulivu wa kutisha. Walivunja mlango wa kinga na kubomoa sehemu ya ukuta kwa kutumia patasi nzito (scalpelli) kisha wakafungua makabati na masanduku. Waliondoka na kiasi cha takriban €30,000, vito vya dhahabu, na hata kadi ya ukaazi ya Kadinali. Mpwa wake amesema: "Tumeshtushwa sana. Tulijihisi salama. Hatukutegemea kabisa wizi wa kinyama kama huu katikati ya Piazza Duomo. Hii ni aibu kwa jiji." I...

WANANCHI DAR ES SALAAM WAHIMIZWA KUJITOKEZA KUCHUNGUZA MABUSHA

Picha
Wananchi katika Mkoa wa Dar es Salaam na Mikoa Jirani wamehimizwa kujitokeza kuchunguza Mabusha na kupata huduma bure ya upasuaji wa ugonjwa huo. Rai hiyo imetolewa leo Januari 8 ,2026 na Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Mhe. Saad Mtambule kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Dar es Salam Mhe. Albert Chalamila Wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Kambi ya Upasuaji wa Mabusha iliyoanza tarehe 5 hadi 30 Januari, 2026. "Nitoe rai kwa Wananchi wa Dar es Salaam na mikoa jirani kujitokeza kuchunguza afya zao hasa uchunguzi wa Mabusha na endapo atabainika matibabu yanatolewa bila malipo yanagharamiwa na Serikali kwa asilimia 100 na lengo ni kufanya upasuaji wa Mabusha kwa zaidi ya Wananchi 500" amesema Mhe. Mtambule Kwa upande wake Mganga Mkuu mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Mohammed Manuna amesema hadi sasa jumla ya Wananchi 165 wamefanyiwa uchunguzi wa Mabusha huku 127 wakibainika na tatizo hilo na 27 wakiwa tayari wameshafanyiwa huduma ya upasuaji. "Karibu asilimia moja ya wagonj...