KUSAYA AONGOZA MAPOKEZI YA NDEGE YA ATCL MUSOMA
Musoma, Mara- Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Ndugu Gerald Musabila Kusaya, leo Septemba 17, 2026 ameongoza mapokezi ya ndege ya abiria ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Musoma, ikiashiria kurejea rasmi kwa safari za abiria baada ya takribani miaka minane. Safari ya mwisho ya ndege ya abiria katika kiwanja hicho ilikuwa Machi 2018 ya Shirika la Precision Air, kabla ya kufungwa kupisha upanuzi na ukarabati. Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mara wakati wa mapokezi hayo, Kusaya amesema kurejea kwa huduma hizo ni fursa muhimu kwa uchumi wa Mkoa wa Mara. "Kurejea kwa ATCL ni fursa muhimu kwa wananchi kutokana na mchango wa usafiri wa anga katika kurahisisha usafirishaji wa watu na mizigo pamoja na kukuza biashara, utalii na uwekezaji," amesema Kusaya. Kusaya ametoa shukrani kwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa wa kuboresha kiwanja hicho na kulipa fidia kwa wananchi 58 waliopisha ujenzi. Amewataka wananchi wa Mara na mikoa jiran...