Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya PAPA

Kujikabidhi kwa Yule anayeongoza Kanisa

Picha
2025.05.08 Uchaguzi wa Papa wa ROma.  (@Vatican Media) Mwariri mkuu wa Baraza la kipapa la Mawasiliano kwa mtazamo wa kuchaguliwa kwa Papa mpya ambaye amebainisha:“Leo hii ulimwengu uko katikati ya dhoruba,inayotikiswa na vita na jeuri.Tuombe amani.Tuombe pamoja na Petro na Petro ambaye leo hii alichukua jina la Leo,akiungana tena na Papa wa Waraka wa kitume wa “Rerum novarum.” Andrea Tornielli Jimbo la Roma lina Askofu wake, Kanisa la ulimwengu wote lina mchungaji wake. Kwa kasi ambayo inaweza  kuwashangaza tu wale wanaosoma maisha ya Kanisa kupitia lenzi za siasa, Mkutano Mkuu umemteua Mrithi wa Petro. Asante, Baba Mtakatifu, kwa kukubali. Asante kwa kusema "ndiyo" na kwa kujiacha kwa Yeye anayeongoza Kanisa. Maneno ya kukumbukwa yaliyosemwa na Paulo VI mbele ya wanafunzi wa Chuo cha Lombardia , mnamo Desemba 1968, wakati wa kipindi kigumu cha kupinga katika kipindi cha baada ya mtaguso, yanakumbuka tena: “Wengi - alisema Papa - wanatarajia kutoka kwa Papa ishara za hisia, ...

Uchaguzi wa Papa,kutoka kwa moshi mweupe hadi Habemus Papam”

Picha
2025.05.08 Papa mpya   (@Vatican Media) Hiki ndicho kilichotokea katika Kikanisa cha Sistine dakika chache ambazo zilifuatiwa na moshi mweupe,ambao unatokea kabla ya tangazo kuu la Kardinali shemasi Mamberti,akiwa katikati ya Dirisha la Baraka la Basilika ya Mtakatifu Petro kwa jina jipya la Askofu wa Roma. Na Alessandro Di Bussolo na Angella Rwezaula – Vatican. Moshi mweupe ulitokea katika bomba lililounganishwa katika Kikanisa cha Sistine, ambao umeashiria kutangaziwa waamini na ulimwengu mzima kuwa amechaguliwa Askofu mpya wa Roma, mfuasi wa Petro. Lakini je ni kitu gani kilitokea chini ya picha za msanii Michelangelo, dakika chache kabla, na ni kitu gani kitaendelea hadi kutangazwa kwa jina jipya la Papa, litakalotangazwa baada ya neno la: "Habemus Papam” yaani "Tunaye Papa" kupitia katikati ya dirisha la Baraka la Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro na Kardinali, Shemasi wa ufaransa, Dominique Mamberti? Jina linalosubiriwa kwa hamu kubwa. Moshi mweupe   (@Vatican Media) I...

Mkutano wa Makardinali wa 11 ulifanyika na kiapo kwa wasaidizi wa mkutano mkuu

Picha
KILINGENI  walitoa kiapo cha usiri kabisa.  (ANSA) Conclave: maofisa na wahusika wengine walitoa kiapo cha usiri kabisa.  (ANSA) Mkutano wa 11 wa Makardinali ulifanyika jioni na mijadala kama 20 hivi ilihusiana na mada kubwa ya umuhimu wa kichungaji na kikanisa.Na wale watakaosaidia katika mkutano wa uchaguzi walitoa kiapo cha usiri kabisa kwa mujibu wa katiba ya Kitume ya Universi Dominici Gregis.Miongoni mwao mshehereshaji wa liturujia za kipapa,watu wa sakrestia,usafi,madaktari,manesi na waungamishi. Vatican News Mkutano wa 11 wa makardinali ulifanyika saa kumi na moja jioni kwa kufunguliwa na sala ya pamoja. Walikuwapo makardinali 170, miongini mwake makardinali 132 wa kupiga kura. Mijadala kama 20 hivi ilijihusiana na mada kubwa ya umuhimu wa kichungaji na kikanisa. Muda ulitolewa kwa suala la ukabila ndani ya Kanisa na  katika jamii. Uhamiaji ulijadiliwa, kwa kutambua wahamiaji kama zawadi kwa Kanisa, lakini pia kusisitiza uharaka wa kusindikizana nao na kuunga...

Kard.Re:Roho Mtakatifu aangazie makardinali kupata Papa anayehitajika kwa wakati wetu

Picha
Kardinali Re   (@Vatican Media) Katika misa kabla ya uchaguzi wa Papa mpya iliyoongozwa na Kadinali Re,Dekano wa Makardinali katika Kanisa Kuu la Vatican ameainisha kazi za kila mrithi wa Petro,kwa kuzingatia amri mpya ya upendo.Wito kwa makardinali wapiga kura:kuchagua kwa majukumu ya juu zaidi ya kibinadamu na ya kikanisa,kuepuka mawazo ya kibinafsi na kuangalia kwa manufaa ya Kanisa na ubinadamu. Na Angella Rwezaula – Vatican. Nitamwinua kuhani mwaminifu, atakayetenda sawasawa na haja za moyo wa Mungu ndiyo ilikuwa antifoni ya wimbo wa ufunguzi iliyosindikiza maandamano marefu ambayo asubuhi ya leo tarehe 7 Mei 2025 iliwaona  wakiingia makardinali wateule kwa upole kama kawaida katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican lililojaa waamini elfu tano, wakati wa Misa ya Pro eligendo Romano Pontifice, yaani kabla ya kuchagua Papa wa Roma. Aliyeongoza misa hiyo katika madhabahu ya kukiri ni Kardinali Giovanni Battista Re, Dekano wa Baraza la Makardinali. Katika mahali pa ...

Makardinali 133 wapiga kura wamewasili Roma na mada nyingi zinajadiliwa

Picha
  Makardinali wanaoendelea na maadalizi katika Mkutano wao,wapo wanajiandaa vema kwa ajili ya Mkutano Mkuu wa uchaguzi ujao na wakati huohuo mkutano wa 10 asubuhi Mei 5,mijadala yao ilihusu hali ya Kanisa na matumaini yao ya siku zijazo. Vatican News Jumatatu tarehe 5 Mei 2025, Makardinali wameendelea na mkutano wa kumi katika kujiandaa kwa ajili ya Mkutano Mkuu ujao wa uchaguzi wa Papa mpya na kuendeleza mijadala yao kuhusu hali ya Kanisa na matumaini yao ya siku zijazo. Msemaji mkuu wa Ofisi ya Waandishi wa Habari ya Vatican, Dk. Matteo Bruni, aliwaambia waandishi wa habari siku ya Jumatatu kwamba Makardinali 179, wakiwemo makardinali 132 wapiga kura, walishiriki katika Mkutano Mkuu wa kumi. Katika taarifa yake alibainisha kwamba Makardinali wote wapiga kura 133 wapo mjini Roma, kabla ya mkutano utakaoanza Jumatano tarehe 7 Mei 2025. Mkutano wa 10 wa makardinali   (@VATICAN MEDIA)   Kwa upande wa Kardinali Giovanni Battista Re, Dekano wa Baraza la Makardinali, aliliambi...

PAPA FRANCISCO NA MAPADRE WATANZANIA & CDF MABEYO

Picha
▪︎Katika picha ni Papa Francisco akiwa na Mapadre watanzania wanaosoma na kufanya utume wako nchini Italia pamoja Na Jenerali Venance Mabeyo, Mkuu wa Majeshi Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. ▪︎Ikumbukwe Maaskofu wote nchini Tanzania wako katika ziara ya Kichungaji yalipo makao makuu ya Kanisa Katoliki duniani mjini Vatican tangu May 14 hadi May 21, 2023. ▪︎Pia katika ziara hiyo wameambatana na Mapadre kadhaa akiwemo Padre Charles Kitima, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania, Padre Chesco Msaga C.PP.S Naibu Katibu Mkuu (TEC) bila kumsahau Padre Thomas Kiangio Msimamizi  wa Jimbo Katoliki Tanga. . . RADIO MARIA TANZANIA

Waraka wa Papa kwa Wachile ni sawa na kutangaza 'hali ya hatari kiroho'

Picha
Waraka wa Papa kwa Wachile ni sawa na kutangaza 'hali ya hatari kiroho' Makao makuu ya Kanisa Katoliki ya Vatican yamesema hatua ya Papa Francis kuomba radhi kutokana na kashfa ya udhalilishaji wa kingono uliofanywa na padri na askofu Chile ni sawa na kutangaza hali ya hatari kiroho katika Kanisa la Chile.Papa amewaomba waathirika kwenda Rome ili awaombe radhi pamoja na kuwaita maaskofu wote wa Chile kwa mkutano wa dharura kujadili namna ya kurekebisha madhara yaliyotokana na kashfa hiyo ambayo imeichafua taswira ya Kanisa Katoliki nchini Chile na sifa ya Papa. Msemaji wa Vatican Grek Burke amesema waraka wa Papa kwa Kanisa Katoliki Chile ni kukiri kuwa alifanya makosa katika mtizamo kuhusu madhila waliyopitia waathiriwa. Hapo jana, Papa alikiri kuwa alifanya makosa makubwa katika maamuzi aliyoyachukua kuhusu sakata la udhalilishaji wa kingono Chile.

Papa aizuru Myanmar inayotuhumiwa kwa mauaji Ziara hii huenda ni jukumu zito kidiplomasia katika miaka minne ya Papa Francis kama kiongozi wa kanisa katoliki.

Picha
Papa Francis aliondoka Roma Jumapili usiku Papa Francis anaanza ziara ya wiki nzima nchini Myanmar na Bangladesh leo Jumatatu, wakati wasiwasi unaendelea wa kimataifa kuhusu usalama na ulinzi kwa wasilamu wa Rohingya. Anatarajiwa kukutana na Aung Sun Suu Kyi na mkuu wa jeshi Myanmar. Hata kabla ya kuondoka Roma, Papa Francis alikuwa anakabailiwana kitendawili cha kidiplomasia: iwapo kuliita kundi dogo la waislamu Myanmar - Rohingya. Ni jina lisilo tumika na serikali ya kiraia na jeshi - wakieleza kuwa ni wahamiaji haramu kutoka Bangladesh na kwahivyo hawapaswi kuorodheshwa kama mojawapo ya makabila nchinihumo. Nchi hiyo yenye idadi kubwa ya maBudda inajitayarisha kumkaribisha Papa Lakini mashirika ya kutetea haki za binaadamu wanamuomba awaite hivyo, yakieleza kuwa nilazima Papa Francis aoneshe huruma kwa watu walionyimwa uraia na tangu Agosti wamekabiliwa na kile kamishna wa haki za binaadamu katika Umoja wa mataifa amekitaja kuwa 'kinachoonekana kuwa mauaji ya kikabila...

Papa Francis apiga marufuku uuzaji wa sigara Vatican

Picha
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage caption Licha ya sigara kuiletea mamilioni ya fedha Vatican ,papa Francis amesema kuwa hawezi kuruhusu binaadamu kuathiriwa kiafya Papa Francis ameagiza marufuku ya uuzaji wa sigara ndani ya Vatican , kuanzia mwaka ujao. Msemaji wa Vatican Greg Burke alisema kuwa mji huo mtakatifu hauwezi kukubali na kitendo ambacho kinahatarisha maisha ya binaadamu. Takriban wafanyikazi 5000 wa Vatican na wale waliostaafu wanaruhusiwa kununua sigara zilizopunguzwa bei . Mauzo hayo yanakadiriwa kuiletea Vatican mamilioni ya yuro kila mwaka. Lakini bwana Burke amesema kuwa hakuna faida ambayo ni halali iwapo sigara zinaathiri afya za wanaadamu. Mtoto amvua kofia Papa Francis Alinukuu takwimu za shirika la afya duniani WHO ambazo zinalaumu uvutaji sigara kwa kusababisha vifo vya takriban watu miioni 7 duniani kila mwaka. ''Nadhani watu wengi wanapenda sigara kwa sababu ya ufadhili wanaopata'' ,alisema. ''Ni kitu ambacho ni lazima...