Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya KITAIFA

MPANGO WA KUIMARISHA UBORA WA AFYA NA USTAWI WA WATOTO NI NYENZO MUHIMU- DKT. SHEKALAGHE

Picha
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe amesema Mpango wa Kuimarisha Ubora wa Afya na Ustawi wa Watoto ni nyenzo muhimu katika kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa watoto na vijana nchini. Dkt. Shekalaghe amesema hayo leo Julai 23, 2025 mkoani Arusha wakati wa kongamano la Pili la Kitaifa la Afya na Ustawi wa Watoto baada ya kuzindua rasmi mpango huo wenye lengo la kushughulikia changamoto zinazowakabili watoto na vijana ikiwemo matatizo ya lishe, mimba za utotoni na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU). Mpango huo umeandaliwa na Chama cha Madaktari Bingwa wa Watoto Tanzania (Pediatric Association of Tanzania – PAT) kwa kipindi cha miaka Mitano (5) kuanzia mwaka 2025 hadi 2030 ambao umejikita katika kushughulikia vikwazo vinavyokwamisha maendeleo ya kiafya kwa watoto na vijana, hasa wenye umri wa miaka 15-19. Vipaumbele vya mpango huo ni pamoja na kutoa ushauri wa kitaalamu kwa Wizara ya Afya na wadau wa sekta ya afya, kushawishi na kuandaa sera zitakazosaidia ...

KATIBA YA CCM YARUHUSU MIKUTANO YAKE KUFANYIKA KWA NJIA YA MTANDAO

Picha
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, kufanya mabadiliko madogo ya Katiba ya CCM ambapo sasa Katiba hiyo inatambua ufanywaji wa mikutano ya ngazi mbalimbali kwa njia ya mtandao maarufu kama E- Meeting. Kulingana na Dkt. Samia wakati akitangaza mapendekezo hayo kwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM, Mabadiliko hayo ni katika kuhakikisha kuwa Chama hicho kinaenda sawa na mabadiliko mbalimbali ya teknolojia yanayotokea duniani,suala ambalo limewezesha CCM pia kufunga Mitambo ya teknolojia yenye kuwezesha Ngazi za CCM wilaya na Mikoa kuweza kuunganishwa pamoja na Makao Makuu kwa njia ya mtandao. Rais Samia amebainisha kuwa Idara ya Oganaizesheni ilipendekeza vikao vitakavyoweza kufanyika kimtandao ni Vikao vya Sekretarieti ya Wilaya, Kamati za siasa za wilaya, Sekretarieti za Mikoa, Kamati za siasa za Mikoa, sekretarieti ya Kamati maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Kamati ...

TANROADS, TAA SHIRIKIANENI MIRADI YA KIMKAKATI IKAMILIKE KWA WAKATI

Picha
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega ameziagiza Taasisi ya Wakala wa Barabara (TANROADS) na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) kushirikiana na kufanya kazi kwa pamoja kumsimamia Mhandisi Mshauri wa ujenzi wa jengo la abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato ili mradi huo ukamilike kwa wakati na ubora. Amesisitiza Taasisi hizo kuwa na mawasiliano na ushirikiano wa karibu kwani Watanzania wanasubiria mradi huo na kuahidi yeye pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule kuukagua mradi huo mara kwa mara. Ulega ametoa maelekezo hayo Mkoani Dodoma mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi huo wa kimkakati ambao umefika asilimia 53.9 na kusisitiza kuwa ukikamilika unatarajiwa kuinua uchumi wa Mkoa wa Dodoma na kuwa kitovu cha biashara na uwekezaji. “Nimekagua jengo hili la abiria ambalo ni la kisasa na Mkandarasi yupo nyuma ya muda, hivyo nimeagiza Mkandarasi Beijing Construction Engineering Group na Hebei Construction Group Corporation (BCEG) afanye kazi usiku na mchan...

WAJUMBE NANE WA KAMATI KUU CHADEMA WATUMBULIWA

Picha
Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa nchini leo Mei 13, 2025 imetengua uteuzi wa wajumbe 8 wa kamati kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) walioteuliwa baada ya kikao cha Baraza Kuu la Taifa cha tarehe 22 Januari 2025 siku moja tu baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa chama hiko. Kwa mujibu wa chanzo cha ndani cha Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa amefanyia kazi malalamiko ya Lembrus K. Mchome kwa mamlaka aliyonayo chini ya Kifungu cha 4(5)(a)na(b) cha Sheria ya Vyama vya Siasa Sura ya 258 na Kanuni ya 31(2)(3) ya Kanuni za Usajili na Ufuatiliaji wa Vyama vya Siasa za Mwaka 2019 (Political Parties (Registration and Monitoring) Regulations, 2019 GN. 953) amebaini kuwa malalamiko ya Mchome ni ya ukweli kwamba kikao cha Baraza Kuu la Taifa la CHADEMA kilichofanyika tarehe 22 Januari 2025 kilikuwa batili, kwa sababu kilikuwa hakina akidi inayotakiwa kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA ya Mwaka 2006 toleo la 2019. Vilevile, hata kama kikao hicho. Ameomgeza kuwa hata kama kikao ...

Ofisi ya Makamu wa Rais imesema mchakato wa kulipa mamlaka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)

Picha
Mhe. Khamis Hamza Khamis Ofisi ya Makamu wa Rais imesema mchakato wa kulipa mamlaka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji kupitia mchakato unaoendelea. Kuifanya NEMC kuwa mamlaka kutaipa nguvu ya kisheria ya kusimamia majukumu yake ipasavyo na hivyo kujiwezesha kimapato. Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis ameliarifu Bunge jijini Dodoma leo tarehe 12 Mei, 2025 wakati akijibu swali la nyongeza Mbunge wa Mpendae Mhe. Toufiq Salim Turky lililoulizwa kwa niaba yake na Mbunge wa Viti maalumu Mhe. Amina Ali Mzee aliyetaka kujua ni lini mchakato wa NEMC kuwa mamlaka kamili. Mhe. Khamis amesema Mchakato wa kulifanya Baraza hilo kuwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira (NEMA) tayari umekwishaanza na pindi utakapokamilika utawasilishwa bungeni kwa ajili ya kujadiliwa na kutolewa maamuzi. Alifafanua kuwa changamoto inayosababisha kuchelewa kwa vyeti vya tathmini ya athari kwa mazing...

Kupaa kwa Yesu na Kumwagwa kwa Roho Mtakatifu

Picha
Somo la Kupaa kwa Yesu na Kumwagwa kwa Roho Mtakatifu Utangulizi Baada ya Yesu kufufuliwa kutoka kwa wafu, yeye      alijidhihirisha kwao, baada ya mateso yake, kwa dalili nyingi, akiwatokea siku arobaini, akinena habari za ufalme wa Mungu.      Matendo 1:3 Wanafunzi walipata uthibitisho usio na shaka kwamba Yesu alikuwa amefufuka kweli. Hili lilikuwa lazima, kwa sababu kila mmoja wao angeteseka sana kwa ajili ya Yesu. Haiwezekani kuvumilia mateso mengi kwa kitu ambacho huna uhakika nacho au ambacho unajua ni uwongo! Kupaa Baada ya zile siku arobaini, Yesu alikutana na wanafunzi wake na kuwaambia:      “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.”      Mathayo 28:18 Yesu alikuwa amemshinda Shetani na kumponda kichwa (akitimiza ahadi ambayo Mungu alimpa Hawa kwamba uzao wake ungeponda kichwa cha nyoka) Aliendelea:      "Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa...