Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya ARUSHA

MPANGO WA KUIMARISHA UBORA WA AFYA NA USTAWI WA WATOTO NI NYENZO MUHIMU- DKT. SHEKALAGHE

Picha
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe amesema Mpango wa Kuimarisha Ubora wa Afya na Ustawi wa Watoto ni nyenzo muhimu katika kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa watoto na vijana nchini. Dkt. Shekalaghe amesema hayo leo Julai 23, 2025 mkoani Arusha wakati wa kongamano la Pili la Kitaifa la Afya na Ustawi wa Watoto baada ya kuzindua rasmi mpango huo wenye lengo la kushughulikia changamoto zinazowakabili watoto na vijana ikiwemo matatizo ya lishe, mimba za utotoni na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU). Mpango huo umeandaliwa na Chama cha Madaktari Bingwa wa Watoto Tanzania (Pediatric Association of Tanzania – PAT) kwa kipindi cha miaka Mitano (5) kuanzia mwaka 2025 hadi 2030 ambao umejikita katika kushughulikia vikwazo vinavyokwamisha maendeleo ya kiafya kwa watoto na vijana, hasa wenye umri wa miaka 15-19. Vipaumbele vya mpango huo ni pamoja na kutoa ushauri wa kitaalamu kwa Wizara ya Afya na wadau wa sekta ya afya, kushawishi na kuandaa sera zitakazosaidia ...

Magufuli amgusia Lowassa kuhusu maji

Picha
Rais Dkt. John Magufuli amezungumzia kitendo cha Mbunge wa Monduli (CCM), Julius Kalanga kumuomba apeleke maji jimboni kwake ilihali jimbo hilo limewahi kuongozwa na Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa ambaye pia amewahi kuwa waziri wa maji. Rais Dkt. Magufuli akiwa na Waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa. Akizungumza na wananchi wa Arumeru, ambapo amezindua na kuweka jiwe la msingi wa ujenzi wa visima vikubwa vya maji zaidi ya 20 jijini Arusha, Rais Magufuli amesema kuwa anampongeza Kalanga kwa kuhamia CCM akitokea CHADEMA kwakile alichosema ni kitendo cha kijasiri. " Kalanga,  Mbunge wa Monduli aliwahi kuniomba maji akiwa CHADEMA, lakini amesahau kuwa Lowassa amewahi kuwa Waziri wa Maji, simsemi mzee wangu namaanisha kuwa uzalendo unaanzia nyumbani, nikupongeze Kalanga kwa ujasiri wako wa kurudi huku, maji utapata ", amesema Rais Magufuli Katika hatua nyingine amewaomba Watanzania kumuombea ili awatumikie vyema, " Muendelee kuniombea ili cheo changu cha Urai...

Rais John Magufuli leo Desemba 2, 2018 amezindua na kuweka jiwe la msingi ujenzi wa visima vikubwa vya maji zaidi ya 20 jijini Arusha.

Picha
Rais John Magufuli leo Desemba 2, 2018 amezindua na kuweka jiwe la msingi ujenzi wa visima vikubwa vya maji zaidi ya 20 jijini Arusha. Rais Dkt. John Magufuli. Rais amesema kuwa mradi huo utakaogharimu shilingi bilioni 520, unahusisha visima vya kuchimbwa na kumaliza tatizo la maji katika Jiji hilo, na zimekopwa katika Benki ya Maendeleo ya Afrika, hivyo zitalipwa na Watanzania wote kupitia kodi. " Serikali imekopa bilioni 520 kutoka Benki ya maendeleo ya Afrika, kwa ajili ya Arusha ili kutekeleza mradi wa maji, hizi hela zitalipwa na Watanzania wote, na tumezileta kwa wale wale wanaoitukana serikali, na yote ni kwasababu maendeleo hayana chama ", amesema Rais Magufuli. Aidha Rais Magufuli amemuagiza Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Isack Kamwele kutosita kuwafukuza wakandarasi wakishindwa kutekeleza mradi huo kwa wakati, " Waziri usiogope kufukuza wakandarasi, kumbuka hata mimi nimewahi kuwa Waziri wa Ujenzi na sikusita kutimua wakandarasi wasiotekeleza miradi, w...

RC Arusha aonya wakandarasi wababaishaji

Picha
RC ARUSHA AONYA WAKANDARASI WABABAISHAJI  Na Ferdinand Shayo,Arusha.  Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Mashaka Gambo ameonya Wakandarasi wanaofanya ubabaishaji kwenye miradi ya barabara za vijijini Mkoani Arusha kwa kutopewa tenda za serikali na badala yake wachukuliwe hatua za kisheria.  Gambo ametangaza marufuku kwa wakandarasi wababaishaji kupewa kandarasi  wakati akikabidhi mikataba ya kwa   wakandarasi wa wilaya za saba za mkoa wa Arusha ikiwemo Arusha,Meru na Karatu .  Aidha amewataka Wakandarasi kuhakikisha kuwa wanakamilisha miradi kwa wakati na kutumia vizuri fedha za walipa kodi na kuepuka kutekeleza miradi chini ya kiwango.  Katibu Tawala Wilaya ya Arusha Richard Kwitega amesema kuwa serikali imewapa kipaumbele Wakandarasi wazawa ili waweze kuleta tija kwenye miradi ya Barabara ambazo zitachochea maendeleo ya wananchi.  Kaimu Mratibu wa Tarura mkoa wa Arusha Dickson Kanyankole  amesema kuwa miradi hiyo itatekelezwa ka...