Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya TANZANIA

BASHUNGWA AHIMIZA WAANDISHI WA HABARI KUHAMASISHA AMANI NA USALAMA.

Picha
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa, ametoa wito kwa Waandishi wa habari kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuwaelimisha na kuwakumbusha Watanzania juu ya umuhimu wa tunu ya amani na usalama, ambayo ni urithi kutoka kwa waasisi wa taifa letu, Tanzania. Ametoa wito huo wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufungua Mkutano wa Wakuu wa Majeshi ya Polisi kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), unaofanyika katika ukumbi wa JNICC – Dar es Salaam, leo tarehe 5 Juni, 2025. “Niendelee kuwaomba, muendelee kushirikiana na Serikali kwa kuwakumbusha Watanzania kuwa amani ni tunu ambayo waasisi wa taifa letu wametuachia, na ulinzi wa taifa letu ni jukumu la kila Mtanzania,” amesema Bashungwa. Bashungwa amesisitiza nafasi ya vyombo vya habari katika kufanya uandishi wa uchunguzi (investigative journalism), ili kuwaonesha Watanzania hali halisi ya mataifa yanavyopata shida kutokana na kukumbwa na migogoro iliyopelekea amani kutoweka. ...

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imeanzisha majimbo mapya nane na kubadilisha majina ya majimbo 12 ya uchaguzi

Picha
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imeanzisha majimbo mapya nane na kubadilisha majina ya majimbo 12 ya uchaguzi yatakayotumika kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika oktoba mwaka huu. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo tarehe 12 Mei, 2025 Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele amesema Tume imefikia uamuzi huo baada ya kupitia maombi kutoka kwenye mikoa mbalimbali nchini. Amesema uamuzi huo umefanyika kwa kuzingatia masharti ya ibara ya 75(1), (2) na (4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 ikisomwa pamoja na kanuni ya 18(7) ya Kanuni za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi za Mwaka 2024. Ameyataja majimbo hayo kuwa ni Jimbo la Kivule amabalo limegawanywa kutoka Jimbo la Ukonga na Jimbo la Uchaguzi la Chamanzi ambalo limegawanywa kutoka Jimbo la Mbagala yote ya mkoani Dar es Salaam. “Mkoani Dodoma limeanzishwa jimbo jipya moja, ambapo Jimbo la Uchaguzi la Dodoma Mjini limegawanywa na kuanzishwa jimbo jipya la ...

Rais Samia amefungua Mkutano wa 14 wa Baraza la Biashara (TNBC)

Picha
  Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan leo June 09,2023 amefungua na kushiriki Mkutano wa 14 wa Baraza la Biashara (TNBC), Ikulu Dar es salaam ambapo moja ya mambo aliyoyasema kwenye hotuba yake ni kwamba kazi kubwa inaendelea kufanyika ya kuboresha mifumo ya TEHAMA kwenye Sekta za Umma ili ianze kusomana ambapo ameahidi kuwa sio zaidi ya miezi sita RAISkinachotokea Bandarini atakuwa anaweza kukisoma akiwa Ikulu. Rais za Zanzibar Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwa kwenye Mkutano wa 14 wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 09 Juni, 2023. Rais Samia amenukuliwa akisema “Kazi kubwa inaendelea kufanyika ya kuboresha mifumo ya TEHAMA, mifumo yetu haisomani, taarifa hazioani, kazi tunayokwenda kufanya kwa nguvu kubwa sasa ni kufanya mifumo ndani ya Sekta ya Umma isomane pia iwe na vigezo vya Kimataifa” “Changamoto zilizotajwa hapa hizo za Kariakoo na nini ni kwamba mifumo yetu haijaweza kuchukua taarifa zote hizo, kazi iliyopo sasa ni...

BINGWA WA KOMBE LA SHIRIKISHO KUPATA TSH. BILIONI 4.7

Picha
Hivi ndivyo viwango vya fedha kwa washiriki wa Kombe la Shirikisho Afrika na Ligi ya Mabingwa Afrika kuanzia msimu huu wa 2022/23; Ligi ya Mabingwa Afrika Bingwa:   Dola Milioni 4 (Tsh. Bilioni 9.4) Wa pili:  Dola Milioni 2 (Tsh. Bilioni 4.7) Nusu Fainali:   Dola 1.2 (Tsh. Bilioni 2.8) Robo Fainali:  Dola 900,000 (Tsh. Bilioni 2.1) Wa 3 Kundini:  Dola 700,000 (Tsh. Bilioni 1.6) Wa 4 Kundini:  Dola 700,000 (Tsh. Bilioni 1.6) Kombe la Shirikisho Afrika Bingwa:  Dola Milioni 2 (Tsh. Bilioni 4.7) Wa pili:  Dola Milioni 1 (Tsh. Bilioni 2.3) Nusu Fainali:  Dola 750,000 (Tsh. Bilioni 1.8) Robo Fainali:  Dola 550,000 (Tsh. Bilioni 1.3) Wa 3 Kundini:  Dola 400,000 (Tsh. Milioni 940) Wa 4 Kundini:  Dola 400,000 (Tsh. Milioni 940)

MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI ZIARA YA WIKI BARANI AFRIKA

Picha
​ Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris anaanza safari ya wiki moja ya kidiplomasia barani Afrika mwishoni mwa juma hili kwa nia ya kuweka Washington kama mshirika bora wa mataifa ya bara hilo kuliko Beijing.  Harris atatembelea Ghana, Tanzania na Zambia kuanzia wikendi hii, ili kujadili mazoea ya China katika kanda hiyo pamoja na masuala ya kiuchumi ya ndani.

SIMIYU YAJIPANGA KUPAMBANA NA COVID-19

Picha
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema  mkoa umetenga shule za Sekondari za Bweni za Serikali kuwa maeneo ambayo yatatumika kuwahifadhi washukiwa wa Virusi vya Corona  endapo watapatikana mkoani hapa;  baada ya serikali  kufunga shule na vyuo nchini kwa siku 30 lengo likiwa kukabiliana na ugonjwa huo. Mhe. Mtaka ameyasema hayo wakati akipokea mchango kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya  shule ya sekondari Anthony Mtaka uliotolewa na umoja wa madhehebu ya kikirsto Lamadi na kuongeza kuwa mbali na maeneo ya shule Mkoa pia umetenga maeneo ya hoteli ambayo yatatumika endapo washukiwa/watu wanaohisiwa kuwa na ugonjwa huo ambao hawatahitaji kukaa kwenye maeneo ya shule. "mkoa hautatumia hoteli kwa ajili ya kuhifadhi mtu yeyote atakayeshukiwa kuwa na maambukizi ya virusi vya corona badala yake tutatumia shule za zetu za sekondari za bweni lakini ikitokea mtu anahitaji kukaa hotelini tayari tumeandaa hoteli za kutosha"alisema Mtaka. " ...

PICHA| UZINDUZI WA KARAKANA YA KUU YA JESHI

Picha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amezindua karakana kuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) - Lugalo jijini Dar es salaam. Machi 13, 2020

RAIS WA TANZANIA ATOA TAHADHARI KUJIKINGA NA UGONJWA WA CORANA

Picha
Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli Rais wa Tanzania, John Magufuli ametoa tahadhari kuhusu ugonjwa unaotokana na virusi vya corona, akiwataka kutopuuza kwani mpaka sasa umegharimu maisha ya watu wengi duniani. Amezungumza na Umma wa Tanzania alipokuwa akizindua karakana ya jeshi hii leo jijini Dar Es Salaam. Katika kusisitiza tahadhari iliyotolewa hivi karibuni na Waziri wa afya nchini humo, Ummy Mwalimu, Rais Magufuli amewataka raia kutopuuza tahadhari hizo. ''Ugonjwa upo na umekumba nchi nyingi kwa takwimu zilizopo ni kwamba zaidi ya watu 100,000 wameambukizwa na watu 4,500 wamepoteza maisha.'' ''Tunatambua kuwa Tanzania mpaka sasa hatuna mgonjwa wa corona lakini hatuwezi kujiweka pembeni bila kuchukua hatua na hatua zimeanza kuchukuliwa waziri wa wizara ya afya ameshatoa tahadhari tunazopaswa kuchukua''. ''Ugonjwa huu unaua na unaua kwa haraka, sana niwaombe tusipuuze, tusipuuze hata kidogo ni lazima kuchukua hatua za kujikinga...

Msuva, Sure boy , Samatta moto wao nimkali

Sure Boy aipa Taifa Stars kuvuna alama tatu katika mchezo wa kusaka tiketi ya kushiriki fainali za Afcon 2021 baada ya kuifunga Guinea ya Ikweta mabao 2-1. Mchezo huo uliopigwa Uwanja wa Taifa ulishuhudiwa  Stars wakiutawala kwa asilimia kubwa lakini iliweza kujikuta ikienda mapumziko ikiwa nyuma bao 1-0. Mchezo huo ulianza kwa kasi kwa wenyeji kuutawala kutokana na mashambulizi yaliyokuwa yakifanywa na nahodha wa  Stars, Mbwana Samatta aliyekuwa akisaidiana na Simon Msuva kuliandama lango la wapinzani. Samatta alikosa kuiandikia bao Stars dakika ya pili baada ya mpira wake kuokolewa na Mlinda mlango wa Felipe Ovono ambaye alionesha umahiri wake wa kuokoa michomo. Wakati vijana hao wa Kocha, Etienne Ndayiragije wakiendelea kulisakata soka mbele ya watazamaji waliojitokeza kwa wingi kutoa sapoti, walijikuta wakiruhusu bao dakika ya 15 lililofungwa na Petro Obiang ambalo lilidumu hadi mapumziko. Hata hivyo Samatta alikosa nafasi nyingne ya kuisawazishia Stars dakika ya 40 l...

Msuva, Sure boy , Samatta moto wao nimkali

Sure Boy aipa Taifa Stars kuvuna alama tatu katika mchezo wa kusaka tiketi ya kushiriki fainali za Afcon 2021 baada ya kuifunga Guinea ya Ikweta mabao 2-1. Mchezo huo uliopigwa Uwanja wa Taifa ulishuhudiwa  Stars wakiutawala kwa asilimia kubwa lakini iliweza kujikuta ikienda mapumziko ikiwa nyuma bao 1-0. Mchezo huo ulianza kwa kasi kwa wenyeji kuutawala kutokana na mashambulizi yaliyokuwa yakifanywa na nahodha wa  Stars, Mbwana Samatta aliyekuwa akisaidiana na Simon Msuva kuliandama lango la wapinzani. Samatta alikosa kuiandikia bao Stars dakika ya pili baada ya mpira wake kuokolewa na Mlinda mlango wa Felipe Ovono ambaye alionesha umahiri wake wa kuokoa michomo. Wakati vijana hao wa Kocha, Etienne Ndayiragije wakiendelea kulisakata soka mbele ya watazamaji waliojitokeza kwa wingi kutoa sapoti, walijikuta wakiruhusu bao dakika ya 15 lililofungwa na Petro Obiang ambalo lilidumu hadi mapumziko. Hata hivyo Samatta alikosa nafasi nyingne ya kuisawazishia Stars dakika ya 40 l...

Serikali kujenga mabweni wanafunzi wasipate mimba

Picha
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mwita Waitara amesema mpango wa Serikali ni kujenga Mabweni katika Shule zote za Msingi na Sekondari, ili kuwanusuru na wanafunzi wa kike na suala la mimba. Mwanafunzi mwenye mimba Naibu Waziri Waitara ametoa kauli hiyo, wakati akizungumza Bungeni jijini Dodoma leo Novemba 15, 2019 wakati wa kipindi cha maswali na majibu kutoka kwa Wabunge kwenda kwa Mawaziri. Waitara amesema kuwa " mpango wa Serikali ni kujenga Mabweni katika Shule zote za Msingi na Sekondari ili watoto wakike wapate sehemu za kukaa na tuwaepushe na mimba zitakazowafanya washindwe kuendelea na masomo ." Leo Novemba 15, 2019 Bunge hilo linatarajiwa kuahirishwa baada ya kujadili mpango wa maendeleo ya Taifa kwa mwaka ujao wa fedha. Serikali kujenga mabweni ili wanafunzi wasipate mimba.

Tanzania :- Marekani na Uingereza zatilia shaka 'haki za Binadamu kisheria'

Picha
Tamko la Marekani na Uingereza linagusia kesi ya Erick Kabendera kama mfano wa hivi karibuni Ubalozi wa Uingereza na Marekani nchini Tanzania wametoa tamko la pamoja kuhusu kile walichokiita "wasiwasi wa kuzorota kwa kwa haki za kisheria nchini Tanzania." Katika tamko hilo, ofisi hizo mbili za ubalozi zinadai kuwa imedhihirika kwa zaidi ya mara moja watu kutiwa kizuizini kwa muda nchini Tanzania bila kupelekwa mahakamani na kubadilishiwa mashitaka na mamlaka zake za kisheria. "Tuna wasiwasi hasa kwa tukio la hivi karibuni -- jinsi ambavyo halikushughulikiwa kwa haki la kukamatwa, kuwekwa kizuizini na tuhuma za mashtaka ya mwandishi wa habari za uchunguzi Bw Erick Kabendera, ikizingatiwa ukweli kwamba alinyimwa haki ya kuwa na mwanasheria kwenye hatua za awali na kutiwa kizuizini kwake, ambapo ni kinyume cha sheria ya makosa ya jinai," inasema sehemu ya tamko hilo. "Tunaisihi serikali ya Tanzania kutoa hakikisho la mchakato wa kutenda haki kisheria k...

MBWANA SAMATTA KUCHEZA EPL

Picha
Mbwana Samatta atajiunga na EPL? Klabu ya Brighton inayocheza ligi ya Primia ya England inaongoza msururu wa klabu zinazomuwania mshambuliaji wa Tanzania, Mbwana Samatta. Klabu nyengine za England ambazo zinamuwania Samatta ni Aston Villa, Watford, Leicester na Burnley. Kwa mujibu wa gazeti la The Sun la Uingereza Samatta ana thamani ya Pauni milioni 12. Samatta ambaye bado ana mwaka mmoja kwenye mkataba wake na mabingwa wa Ubelgiji KRC Genk pia amezivutia klabu za Roma ya Italia na Lyon ya Ufaransa. Mshambuliaji huyo ambaye aliongoza kwa kupachika mabao msimu uliopita nchini Ubelgiji ameweka wazi kuwa anataka kuelekea nchini England msimu ujao. "Kwa sasa hivi siwezi kusema sana, ni kitu ambacho kipo kwenye mchakato nasubiria kitakapokuwa tayari na wakati utakapofika nitaweza kukizungumza. Lakini sijioni tena Genk, namuomba Mwenyezi Mungu litimie, lakini ikishindikana bado nina mkataba na Genk," aliiambia runinga ya Azam TV ya Tanzania wiki iliyopita. Romelu Lukaku: ...

Shujaa aliyewaongoza kupinga utawala wa kikoloni Afrika

Picha
Chifu Mkwawa: Shujaa aliyewaongoza Wahehe kupinga utawala wa kikoloni Afrika mashariki Fuvu la Chifu Mkwawa limewekwa ndani ya sanduku la kigae katika jumba la ukumbusho la Mkwawa huko Kalenga, Tanzania ya kati. Lakini kama taji, awali lilitundikwa katika nyumba ya afisa wa kikoloni huko Bagamoyo, kabla ya kuondolewa na kupelekwa Ujerumani - mkoloni wa mji huo - mwanzo mwa karne ya 20. Fuvu hilo lilitumika kuwatishia Wahehe, ambao waliongozwa na shujaa huyo katika vita vya kupinga utawala wa kikoloni wa Ujerumani. Na ufanisi wake ulikuwa ni mkubwa katika miaka ya 1890 kiasi cha Ujerumani kutangaza zawadi kwa yeyote atakeleta kichwa chake. Inaaminika kwamba alijitoa uhai mwenyewe mnamo 1898, badala ya kuingia izara ya kukamatwa, wakati alipokuwa akijificha katika pango lililozungukwa na wanajeshi wa Ujerumani. Miongo miwili baadaye, mjadala kuhusu hatma ya fuvu hilo uligubika majadiliano ya wanadiplomasia ambao kwa miezi kadhaa walishindana kuhusu makubaliano ya vita hivyo v...

Fedha za ndani kugharamia mradi wa kufua umeme

Picha
Fedha za ndani kugharamia mradi wa kufua umeme wa kilowati 2115 Raisi wa Tanzania Dokta John Magufuli akisalimiana na Waziri wa nishati wa Misri Dokta Mohamed Shaker Raisi John Magufuli ameweka jiwe la msingi kwenye mradi mkubwa wa kufua umeme katika mto Rufiji utakaozalisha umeme wa kilowati 2115 Mradi huu utakaogharimu kiasi cha trilioni 6.5 za Tanzania, zikiwa fedha za ndani, ulipangwa kutekelezwa kwa miezi 42 hivi sasa ikiwa imebaki miezi 36 pekee ili kuukamilisha, Umeme utakaozalishwa utasafirishwa kutoka Rufiji kuelekea Chalinze , umbali wa km 167 kisha Dar es Salaam na Dodoma pia umeme utakaozalishwa utaweza kuendesha treni za mwendo kasi. Waziri wa Nishati nchini Tanzania, Dokta Medard Kalemani amesema malengo ya serikali ni kuzalisha umeme wa megawatt 10000 ifikapo mwaka 2025. Mradi huu una manufaa gani? Utasaidia udhibiti uharibifu wa mazingira, Dar es Salaam pekee magunia laki 5 ya mkaa hupelekwa na kutumika kila mwezi kutoka msituni, Asilimia 71.2 ya watanz...

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Picha
Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...

TANZANIA YAIKOSOA BENKI YA DUNIA

Picha
Ni kwanini Tanzania imekosoa makadirio ya benki ya dunia ya ukuaji wa uchumi wake Albina Chuwa, mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania (NBS) Taasisi ya takwimu nchini Tanzania imesema kuwa inaweza kutathmini takwimu za ukuaji wa uchumi wake wa mwaka 2018 baada ya Benki ya dunia kutoa takwimu zilizoonyesha kiwango cha chini cha ukuaji wa uchumi wa nchi hiyo. Waziri wa fedha wa Tanzania aliliambia bunge mwezi uliopita kuwa kiwango cha ukuaji wa uchumi kilikuwa ni 7% mwaka jana. Benki ya dunia ambayo ilitoa hesabu zake kwa misingi ya data za taifa , matarajio ya mwaka 2019 ya ukuaji wa kiwango cha 5.4% - pia ilitoa kiwango cha chini cha ukuaji chini ya kile kilichokuwa kimekadiriwa na na serikali cha 7.1%. Albina Chuwa, mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), ametetea njia zake na namna alivyofikia kiwango hicho, Reuters linaripoti. "Tumekwenda kote nchini kukusanya data halisi , sio sawa na mtu ambaye anakaa Washington na kutengeneza sampuli za pato la ndani ...

Mambo yako vipi kwa Air Tanzania hii leo?

Picha
Air Tanzania: Faida ikoje baada ya kufufuliwa shirika la ndege Tanzania? Ndege ya Dreamliner ilipowasili Tanzania Julai 2018 Wiki hii shirika la ndege nchini- Air Tanzania linaidhinisha njia mpya ya usafiri - jambo linalotazamwa kuwa fursa ya ukuwaji linapokuja sula la usafiri wa abiria. Rais John Pombe Magufuli aliahidi kwamba shirika hilo litaimarishwa na ndege mpya kununuliwa mara baada ya kuingia madarakani. Tanzania, kama ilivyo kwa nchi nyingine kama Zambia, Zimbabwe, Nigeria na Uganda, imelifufua shirika lake la ndege, ama kama lijulikanavyo, Air Tanzania. Uwekezaji mkubwa umefanywa mpaka sasa katika kulifanikisha hilo. "Shirika letu la ndege lilikuwa na hali mbaya sana, lilikuwa na ndege moja tu tena ilikuwa inafanyiwa matengenezo mara kwa mara, soko la ATCL lilishuka sana hadi kufikia asilimia 2.5. Lakini sasa tumenunua ndege 7, na nyingine kubwa aina ya Boeing 787-8 Dreamliner itakuja mwaka 2020", alisema Rais Magufuli mwaka jana 2018 katika  hafla ya ...