Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya DUNIA

Kujikabidhi kwa Yule anayeongoza Kanisa

Picha
2025.05.08 Uchaguzi wa Papa wa ROma.  (@Vatican Media) Mwariri mkuu wa Baraza la kipapa la Mawasiliano kwa mtazamo wa kuchaguliwa kwa Papa mpya ambaye amebainisha:“Leo hii ulimwengu uko katikati ya dhoruba,inayotikiswa na vita na jeuri.Tuombe amani.Tuombe pamoja na Petro na Petro ambaye leo hii alichukua jina la Leo,akiungana tena na Papa wa Waraka wa kitume wa “Rerum novarum.” Andrea Tornielli Jimbo la Roma lina Askofu wake, Kanisa la ulimwengu wote lina mchungaji wake. Kwa kasi ambayo inaweza  kuwashangaza tu wale wanaosoma maisha ya Kanisa kupitia lenzi za siasa, Mkutano Mkuu umemteua Mrithi wa Petro. Asante, Baba Mtakatifu, kwa kukubali. Asante kwa kusema "ndiyo" na kwa kujiacha kwa Yeye anayeongoza Kanisa. Maneno ya kukumbukwa yaliyosemwa na Paulo VI mbele ya wanafunzi wa Chuo cha Lombardia , mnamo Desemba 1968, wakati wa kipindi kigumu cha kupinga katika kipindi cha baada ya mtaguso, yanakumbuka tena: “Wengi - alisema Papa - wanatarajia kutoka kwa Papa ishara za hisia, ...

Kard.Re:Roho Mtakatifu aangazie makardinali kupata Papa anayehitajika kwa wakati wetu

Picha
Kardinali Re   (@Vatican Media) Katika misa kabla ya uchaguzi wa Papa mpya iliyoongozwa na Kadinali Re,Dekano wa Makardinali katika Kanisa Kuu la Vatican ameainisha kazi za kila mrithi wa Petro,kwa kuzingatia amri mpya ya upendo.Wito kwa makardinali wapiga kura:kuchagua kwa majukumu ya juu zaidi ya kibinadamu na ya kikanisa,kuepuka mawazo ya kibinafsi na kuangalia kwa manufaa ya Kanisa na ubinadamu. Na Angella Rwezaula – Vatican. Nitamwinua kuhani mwaminifu, atakayetenda sawasawa na haja za moyo wa Mungu ndiyo ilikuwa antifoni ya wimbo wa ufunguzi iliyosindikiza maandamano marefu ambayo asubuhi ya leo tarehe 7 Mei 2025 iliwaona  wakiingia makardinali wateule kwa upole kama kawaida katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican lililojaa waamini elfu tano, wakati wa Misa ya Pro eligendo Romano Pontifice, yaani kabla ya kuchagua Papa wa Roma. Aliyeongoza misa hiyo katika madhabahu ya kukiri ni Kardinali Giovanni Battista Re, Dekano wa Baraza la Makardinali. Katika mahali pa ...

Makardinali 133 wapiga kura wamewasili Roma na mada nyingi zinajadiliwa

Picha
  Makardinali wanaoendelea na maadalizi katika Mkutano wao,wapo wanajiandaa vema kwa ajili ya Mkutano Mkuu wa uchaguzi ujao na wakati huohuo mkutano wa 10 asubuhi Mei 5,mijadala yao ilihusu hali ya Kanisa na matumaini yao ya siku zijazo. Vatican News Jumatatu tarehe 5 Mei 2025, Makardinali wameendelea na mkutano wa kumi katika kujiandaa kwa ajili ya Mkutano Mkuu ujao wa uchaguzi wa Papa mpya na kuendeleza mijadala yao kuhusu hali ya Kanisa na matumaini yao ya siku zijazo. Msemaji mkuu wa Ofisi ya Waandishi wa Habari ya Vatican, Dk. Matteo Bruni, aliwaambia waandishi wa habari siku ya Jumatatu kwamba Makardinali 179, wakiwemo makardinali 132 wapiga kura, walishiriki katika Mkutano Mkuu wa kumi. Katika taarifa yake alibainisha kwamba Makardinali wote wapiga kura 133 wapo mjini Roma, kabla ya mkutano utakaoanza Jumatano tarehe 7 Mei 2025. Mkutano wa 10 wa makardinali   (@VATICAN MEDIA)   Kwa upande wa Kardinali Giovanni Battista Re, Dekano wa Baraza la Makardinali, aliliambi...

Papa Francis amelazwa katika hospitali ya Gemelli kutokana na matatizo ya kupumua.

Picha
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis (86), amelazwa katika hospitali ya Gemelli kutokana na matatizo ya kupumua. Msemaji wa Vatican Matteo Bruni amesema kuwa katika siku za karibuni Kiongozi huyo amekuwa akilalamika kuhusu shida hiyo. Taarifa iliyotolewa na Makao Makuu ya Kanisa Katoliki imeeleza matokeo ya vipimo kuwa ni tatizo kwenye mfumo wa upumuaji. Aidha Vatican imesisitiza kuwa Papa Francis hana Uviko19. Awali Vatican ilieleza kuwa Kiongozi huyo alipelekwa hospital ili kufanyiwa ukaguzi ambao ulishapangwa. Hata hivyo vyombo vya habari vya Italia vilihoji suala hilo kwani mahojiano ya televisheni aliyotakiwa kufanya Papa jioni ya leo yalifutwa dakika za mwisho.

Korea Kaskazini 'yaiba mabilioni kutengeza makombora'

Picha
Korea Kaskazini inasema jaribio la hivi karibuni la makombora yake ni onyo kwa Marekani na Korea Kusini Korea Kaskazini imeiba dola bilioni mbili (£1.6bn) kufadhili mpango wake wa silaha kupitia uvamizi wa kimtando, inasema ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyovuja. Ripoti hiyo ya kisiri inasema Pyongyang inalenga mabenki na na ubadilishanaji wa sarafu ya crypto-currency kukusanya pesa. Vyanzo vya habari vimethibitishia BBC kwamba UN ilikuwa ikichunguza mashambulio 35 ya kimtandoa. Korea Kaskazini ilifyetua makombora mawili siku ya Jumanne ikiwa ni mara ya nne imechukua hatua hiyo katika kipindi cha chini ya wiki mbili Katika taarifa, Rais wa nchi hiyo Kim Jong-un amesema hatua hiyo ni onyo dhidi ya mazoezi ya pamoja ya kijeshi yanayofanywa na Marekani na Korea Kusini. Pyongyang imeelezea kuwa mazoezi hayo yanakiuka mkataba wa amani. How could war with North Korea unfold? Ripoti t iliyovuja na ambayo ilitumwa kwa kamati ya vikwazo vya Korea Kaskazini katika Baraza Kuu...

Mfumo wa nyota na sayari unaounda dunia umepinda

Picha
Picha mpya za falaki yetu ya Milky Way Mfumo wetu wa sayari na nyota, ama falaki, upo katika umbo la upinde na si nyoofu kama ilivyodhaniwa hapo awali, utafiti mpya umebaini. Njia hiyo ya falaki, maarufu kwa lugha ya Kiingereza kama Milky Way, katika vitabu vyote vya sayansi na taaluma inaoneshwa ipo katika unyoofu. Hata hivyo, utafifiti mpya wa nyota zing'aazo zaidi kwenye falaki hiyo umebaini kuwa nyota hizo hazipo kwenye njia nyoofu, zimepinda. Wataalamu wa unajimu kutoka Chuo Kikuu cha Warsaw wanadhani kuwa nyota hizo zimepinda kutoka kwenye njia nyoofu ikiwa ni matokeo ya kutangamana na falaki nyengine za karibu. Ramani mpya tatu za falaki ya Milky Way zimechapishwa kwennye jarida la Science . Picha maarufu zaidi ya Milky Way ikiwa katika mstari nyoofu imetokana na utafiti wa nyota milioni 2.5 kati ya nyota zipatazo bilioni 2.5 katika falaki hiyo. Dr University. "Undani wa kimfumo na historia ya falaki ya Milky Way bado kabisa kujulikana, na moja ya saba...

IMF lakadiria uchumi kukuwa duniani 2018, lakini Afrika iko wapi?

Picha
Sekta ya kilimo iliimarika kwa sehemu kubwa ikishinikizwa na uwekezaji wa miundo msingi na uzalishaji wa vyakula. Shirika la fedha la kimataifa IMF limesema 2018 ndio mwaka utakaoshuhudia ukuwaji mkubwa wa kiuchumi duniani tangu 2011. Hatahiyo uwezekano wa ukuwaji huo kwa mataifa yanayoendelea kusini mwa jangwa la Sahara hautokuwa rahisi katika miaka mitano ijayo. Je ni kwanini? IMF linakadiria kwamba ukuwaji wa pato jumla la nchi katika mataifa yaliopo kusini mwa jangwa la Sahara utaongezeka taratibu kati ya 2018 na 2019 kwa asilimia 3.4% hadi 3.7%, mtawalaia, huku bei za bidhaa zikipanda. Shirika hilo linalotoa mikopo kwa mataifa duniani hatahivyo linasema lina matumaini kuhusu uwezekano huo wa ukuwaji wa uchumi likitabiria ukuwaji wa hadi 3.9% mwaka huu kutoka 3.8% mwaka 2017 . Ukuwaji wa uchumi katika mataifa ya Afrika kusini mwa jangwa la Sagara umekuwa kwa asilimia 2.4 baada ya kushuka kwa 1.3 mnamo 2016 Limeonya hatahivyo kwamba kasi hiyo huenda isiwe ya muda mr...