Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mfumo wa nyota na sayari unaounda dunia umepinda












Picha mpya za falaki yetu ya Milky Way

Mfumo wetu wa sayari na nyota, ama falaki, upo katika umbo la upinde na si nyoofu kama ilivyodhaniwa hapo awali, utafiti mpya umebaini.

Njia hiyo ya falaki, maarufu kwa lugha ya Kiingereza kama Milky Way, katika vitabu vyote vya sayansi na taaluma inaoneshwa ipo katika unyoofu.

Hata hivyo, utafifiti mpya wa nyota zing'aazo zaidi kwenye falaki hiyo umebaini kuwa nyota hizo hazipo kwenye njia nyoofu, zimepinda.

Wataalamu wa unajimu kutoka Chuo Kikuu cha Warsaw wanadhani kuwa nyota hizo zimepinda kutoka kwenye njia nyoofu ikiwa ni matokeo ya kutangamana na falaki nyengine za karibu.

Ramani mpya tatu za falaki ya Milky Wayzimechapishwa kwennye jarida la Science.

Picha maarufu zaidi ya Milky Way ikiwa katika mstari nyoofu imetokana na utafiti wa nyota milioni 2.5 kati ya nyota zipatazo bilioni 2.5 katika falaki hiyo. Dr University.

"Undani wa kimfumo na historia ya falaki ya Milky Way bado kabisa kujulikana, na moja ya sababu ni kuwa, ni vigumu sana kupima umbali baina ya nyota na maeneo mengine ya mbali ya falaki yetu," ameeleza Dkt Dorota Skowron kutoka Chuo Kikuu cha Warsaw.







Ili kupata picha ya kihalisia zaidi, Dkt Skowron na wataalamu wenzake walipima umbali wa baadhi ya nyota zing'aazo zaidi kwenye falaki yetu ya Milky Way. Nyota hizo ni kubwa, na za umri mdogo ambazo hung'aa mara elfu zaidi ya jua. Pia nyota hizo huongezeka ukubwa kwa kiwango cha juu kinachoendana na ung'aavu wake.



Hali hiyo ya ung'aavu na ukuaji wa nyota hizo unawawezesha wataalamu wa anga za mbali kukagua umali wao kwa ufanisi wa hali ya juu.

Nyingi ya nyota hizo ziligunduliwa kupitia kifaa kifahamikacho kama Optical Gravitational Lensing Experiment (OGLE) kilichopo kwenye eneo la Las Campanas, jangwa la Atacama nchini Chile.

Przemek Mroz, ambaye ni mjumbe wa timu ya OGLE amesema matokeo ya utafiti huo yanastaajabisha.



"Matokeo yetu yanaonesha kuwa falaki ya Milky Way Galaxy si nyoofu. Imepinda na kukunja kona kutoka kwenye kitovu chake. Kupinda huko kunaweza kuwa kumesababishwa na kutengamana na falaki nyengine ama kukutana na vitu vyeusi (vitu visivyoonekana lakini vipo ndani ya falaki)."

Matokeo hayo ya wataalamu kutoka Poland, yanaendana na matokeo mengine ya utafiti kuhusu nyota hizo ambayo yalichapishwa mwezi Februari na wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Macquarie nchini Australia na Taasisi ya Sayansi ya Uchina


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...