Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mabadiliko ndani ya Simba SC Tanzania ni muamko mpya?















Mmiliki mwenza wa Simba SC Mohammed Dewji anijtahidi kuona klabu hiyo inakuwa ndani na nje ya uwanja (Picha kwa hisani ya Mahmoud Bin Zubeiry)

Siku ya Jumanne mashabiki wa mojawapo wa timu kongwe Tanzania watakusanyika katika uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam kusherehekea "Simba Day".



Ni katika kuidhinisha wiki ya Simba au kwa umaarufu "Simba Week" na inahusisha mechi ya kirafiki dhidi ya Power Dynamos ya Zambia pamoja na mechi za timu za wanawake walio chini ya miaka 20.

Shughuli zilizopangwa kwa siku saba zimenuiwa kuongeza ukaribu na ushirikiano baina ya wachezaji na mashabiki wa timu hiyo pamoja na Simba kuisaidia jamii kupitia miradi tofuati.





Ni sehemu ya azimio la Bilionea Mohammed Dewji, mmiliki mwenza wa klabu hiyo anayeitaka klabu hiyo ikuwe ndani na nje ya uwanja ili kuhakikisha ufanisi zaidi.

"Niliwahi kukutana na mojawapo ya viongozi wa Zamalek (mnamo 2003) na niligundua wakati huo kuwa bajeti ya Zamalek ni mara 50 zaidi ya bajeti ya Simba," anaielezea BBC Sport."

"Naweza kuilinganisha na dereva anayeendesha Toyota na mwingine anayeendesha Ferrari - mtu hufanya awezalo."

Azimio la Dewji


Simba ilicheza dhidi ya Asante Kotoko ya Ghana mnamo 2018 "Simba Week" (Picha kwa hisani ya Mahmoud Bin Zubeiry)

Aliporudi Tanzania baada ya mashindano hayo ya ubingwa barani Afrika, Dewji alifahamu kuwa mambo yanahitaji kubadilika katika namna ambavyo klabu hiyo inaendeshwa iwapo inataka kushindana.

Kwa wakati huo, pendekezo lake la kubadilishi mfumo wa umiliki wa klabu hiyo, haukupokewa vizuri na alijitoa Simba mnamo 2004.

Miaka 11 baadaye, katika televisheni nchini humo alijadili atakachokifanya kuongeza mara tatu bajeti ya klabu hiyo, kuwekeza katika miundo mbinu na namna ambavyo wangeliliziba pengo katika kufikia klabu kubwa barani Afrika.

"Ilikuwa kama mzaha tu lakini Simba ilikuwa haifanyi vizuri na mzaha ukashika kasi," alifafanua.

Miaka miwili baadaye 'mzaha' huo ulimfanya shabiki sugu wa Simba arudi na kumiliki 49% ya hisa katika klabu hiyo.

Umiliki na mageuzi hayo yalioidhinishwa na wafuasi wa klabu ya Simba ulikuwa kama kivuko kuingia katika ufanisi wa klabu hiyo msimu uliopita.

Mnamo 2018 walifanikiwa kuidhinisha usajili wa wachezaji mahiri katika safari ya Uturuki na ilionuiwa kuimarisha ushindani wa klabu hiyo nchini na kimataifa.

Zaidi ya hapo walifanikiwa kuwekeza katika miundo mbinu msingi, ikiwemo ujenzi wa uwanja wa kisasa na wa kufanya mazoezi.



Hisia ya mashabiki wa Simba baada ya mchezo

Simba ilifikia malengo yake msimu uliopita - kwa kushinda katika ligi na kufika kiwango cha makundi katika ligi ya mabingwa, walifanikiwa zaidi kwa kufuzu katika robo fainali ya mashindano ya klabu barani.

Licha ya kufanikiwa kuiongeza bajeti ya mwaka zaidi ya mara mbili kwa klabu hiyo, Dewji anafahamu kuwa ipo kiwango cha chini ikilinganishwa na klabu nyingine barani zilizofanikiwa, lakini anaamini itazifikia kifedha katika miaka mitano ijayo.

"Miaka miwili iliyopita tumeongeza bajeti yetu mara mbili kutoka takriban $1m kwa mwaka hadi $2.5m," Dewji amefafanua.

"Tutashirikiana na makampuni kama Mohammed Enterprises na Total. Tunafahamu kuwa kila Mtanzania ni lazima anunuwe mafuta, mchele na sukari.

"Iwapo mashabiki watanunua bidhaa kutoka Mohammed Enterprises watapata punguzo la bei, na kwa upande wao, washirika watawapa thamani ya kutosha ya mauzo hayo."

Kuwaleta mashabiki


Simba imewahimiza mashabiki zaidi wajitokeze na kuinga mkono timu hiyo (Picha kwa hisani ya Mahmoud Bin Zubeiry)

Njia nyingine ambayo klabu hiyo inatumai kushindana ni kwa kuimarisha ushirikiano na mashabiki wake.

"Tunawavutia. Tumekusanya taarifa kuwahusu. Tumelenga thamani inayostahili katika suala la kiingilio," Dewji ameendelea kusema.

"Tumezusha shauku kubwa. Tumeidhinisha ukaribu na magazeti na vituo vya redio. Nadhani ndio mwanzo mkoko unaalika maua."

Simba imejaribu kuifanya soka iwe na bei nafuu na inayowavutia kila mtu aliye na fikra kama vile tiketi za gharama ya chini zinazo wavutia walio na kipato cha chini.

Wakati huo huo kuna tiketi za gharama ya juu - platinum level - kwa wanaojiweza na inayojumuisha fulana ya Simba, usafiri wa basi kwenda na kutoka uwanjani, na viti vya watu muhimu.

Shauku ya mashabiki wao 60,000 katika mechi za nyumbani zimewavutia watazamaji wengi wa soka Afrika.





"Nilikuwa ninazunguma na rais wa shirikisho la soka Caf Ahmad na amesema hajawahi kuona mashabiki wa Afrika wakijaza uwanja katika mechi za nje kama ilivyokuwa kwa Simba. Mpango wetu wa kuwa na uwazi una manufaa."

Uwazi huo umehimiza ushirikiano wa karibu baina ya mashabiki na Dewji amesisitiza umuhimu wa hilo kwa wanachama wa bodi yake.

"Simba ni klabu kubwa. Ni nembo kubwa," aliongeza.

" Ni jukumu letu kama viongozi wa klabu hii na kama mmiliki wa klabu hii kwamba A) tuwe na maadili katika tunachokifanya B) Tunahitaji kuwa na uwazi mkubwa katika tunachokifanya na C) tunahitaji kuwasiliana na mashabiki wetu kupitia vyombo vya habari kufafanuwa azimio letu ni lipi."

Ushawishi wa Simba kwa timu ya Taifa


John Bocco wa Simba ni moja kati ya wanne katika kikosi cha klabu hiyo Tanzania katika kombe la mataifa ya Afrika

Ufanisi wa Simba umeathiri pia timu ya taifa ya Tanzania wakati Taifa Stars ilipofuzu kwa mara ya kwanza katika miaka 39 kushiriki fainali za kombe la mataifa ya Afrika.

Dewji aliongoza kamati iliyohakikisha mechi muhimu ya kufuzu kwa Tanzania dhidi ya Ugnada ilipata uungwaji mkono mkubwa wa mashabiki.

"Kuwaona mashabiki wengi kulitupatia nguvu ya kwenda na kupambana na kufuzu," alisema mchezaji wa kiungo cha kati wa timu hiyo ya taifa Himid Mao, anayeichezeka klabu ya Misri Petrojet.

"Tulipokuwa njiani tukielekea uwanjani, tukawaona mashabiki wengi ilitufanya tuhisi kama tuna deni la kuwalipa."

Mpango ulifanikiwa huku mashabiki wakiwashangilia, timu hiyo ilipata ushindi wa 3-0 ikiwemo mkwaju wa penalti wake Ernesto Nyoni wa klabu ya Simba dhidi ya majirani zake na kufanikiwa kufuzu katika mashindano hayo nchini Misri.

Nyoni wa Simba ni moja kati ya wanne waliocheza katika kikosi cha Tanzania katika kombe la mataifa ya Afrika nchini Misri akiwemo pia Kipa John Bocco, Aishi Manula, na mchezaji wa ziada Mohamed Hussein.

Na kulikuwa na wachezaji wawili pia wa Simba katika kikosi cha Uganda nchini Misri, nao ni Murushid Juuko na Emmanuel Okwi, ambaye ameondoka kujiunga na Al Ittihad ya Misri.

Matumaini ya Simba sasa ni kushinda katika ligi ya mabingwa na kwa mkono wa biashara wa Dewji anayeushikilia usukani, gari hilo ambalo halikuweza kushindana katika siku za nyuma, linaonekana kusogea katika muelekeo mzuri na linashika kasi


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...