Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya ELIMU

FAHAMU KWANINI MWANAUME HUMWAGA SHAHAWA USIKU AKIWA AMELALA/USINGIZINI.

FAHAMU KWANINI MWANAUME HUMWAGA SHAHAWA USIKU AKIWA AMELALA/USINGIZINI. Mwanaume kumwaga mbegu akiwa usingizini huitwa ndoto nyevu (nocturnal emission) au kwa lugha ya kawaida kumwaga bila kukusudia usiku.  Hili ni jambo la kawaida, hasa kwa wanaume vijana na hata watu wazima. Sababu kuu huwa ni za Kisaikolojia, Maumbile na hata Mihemko ya mwili. Nimekuwa naletewa kesi hii na Wanaume wakijua labda ni Matatizo yao ya Ki-Afya au laa Wanavamiwa na Majini mahaba. Ni kweli kuna nafasi ya kuvamiwa na Pepo wa ngono hao jini mahaba lakini pia kuna pepo wa Kingono wajulikanao kama Sexual Transmitted Demons huwavamia Wanaume kwa wanawake pia lakini njia hii huwa ni tofauti na kuota ndoto nyevu. Zifuatazo ni Sababu za kwanini Mwanaume Humwaga Mbegu za Kiume akiwa Usingizini ama laa akiwa amelala hata inapokuwa Mchana. 1. Kwanza ni matokeo ya Mwili Kujisafisha. Mwili wa Mwanaume hutengeneza mbegu (manii) kila siku, Kama hajafanya tendo la ndoa wala kufanya punyeto yaani kujichua kwa muda mrefu...

WAZIRI MKUU AZURU CHUO KIKUU CHA KILIMO BELARUS

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea Chuo Kikuu cha Kilimo cha Belarus (Belarusian State Agrarian Technical University - BSATU) na kufanya mazungumzo na viongozi wa chuo hicho wakiongozwa na Mkuu wa Chuo, Bw. Romaniuk Nikolai.   Mazungumzo hayo yamefanyika leo (Jumatano, Julai 23, 2025) kwenye ukumbi wa mikutano wa chuo hicho jijini Minsk ambapo masuala ya ushirikiano baina ya vyuo vikuu vya Tanzania vikiwemo vya Sokoine na DIT yalijadiliwa.   Waziri Mkuu aliwaeleza viongozi wa chuo kikuu hicho jinsi Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa  Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ilivyoboresha sera ya elimu ambayo inataka elimu ya amali na stadi za ufundi ziwe sehemu muhimu katika mitaala ya mafunzo yanayotolewa nchini kote.    Aliwaeleza viongozi hao juu ya hati ya makubaliano kwenye sekta ya elimu iliyosainiwa jana mbele ya Waziri Mkuu wa Belarus na kwamba sasa ni wakati muafaka wa kuangalia namna ya kuandaa ziara za mafunzo, kubadilishana wanafunzi na wahadh...