Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya DINI

Uchaguzi wa Papa,kutoka kwa moshi mweupe hadi Habemus Papam”

Picha
2025.05.08 Papa mpya   (@Vatican Media) Hiki ndicho kilichotokea katika Kikanisa cha Sistine dakika chache ambazo zilifuatiwa na moshi mweupe,ambao unatokea kabla ya tangazo kuu la Kardinali shemasi Mamberti,akiwa katikati ya Dirisha la Baraka la Basilika ya Mtakatifu Petro kwa jina jipya la Askofu wa Roma. Na Alessandro Di Bussolo na Angella Rwezaula – Vatican. Moshi mweupe ulitokea katika bomba lililounganishwa katika Kikanisa cha Sistine, ambao umeashiria kutangaziwa waamini na ulimwengu mzima kuwa amechaguliwa Askofu mpya wa Roma, mfuasi wa Petro. Lakini je ni kitu gani kilitokea chini ya picha za msanii Michelangelo, dakika chache kabla, na ni kitu gani kitaendelea hadi kutangazwa kwa jina jipya la Papa, litakalotangazwa baada ya neno la: "Habemus Papam” yaani "Tunaye Papa" kupitia katikati ya dirisha la Baraka la Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro na Kardinali, Shemasi wa ufaransa, Dominique Mamberti? Jina linalosubiriwa kwa hamu kubwa. Moshi mweupe   (@Vatican Media) I...

Mkutano wa Makardinali wa 11 ulifanyika na kiapo kwa wasaidizi wa mkutano mkuu

Picha
KILINGENI  walitoa kiapo cha usiri kabisa.  (ANSA) Conclave: maofisa na wahusika wengine walitoa kiapo cha usiri kabisa.  (ANSA) Mkutano wa 11 wa Makardinali ulifanyika jioni na mijadala kama 20 hivi ilihusiana na mada kubwa ya umuhimu wa kichungaji na kikanisa.Na wale watakaosaidia katika mkutano wa uchaguzi walitoa kiapo cha usiri kabisa kwa mujibu wa katiba ya Kitume ya Universi Dominici Gregis.Miongoni mwao mshehereshaji wa liturujia za kipapa,watu wa sakrestia,usafi,madaktari,manesi na waungamishi. Vatican News Mkutano wa 11 wa makardinali ulifanyika saa kumi na moja jioni kwa kufunguliwa na sala ya pamoja. Walikuwapo makardinali 170, miongini mwake makardinali 132 wa kupiga kura. Mijadala kama 20 hivi ilijihusiana na mada kubwa ya umuhimu wa kichungaji na kikanisa. Muda ulitolewa kwa suala la ukabila ndani ya Kanisa na  katika jamii. Uhamiaji ulijadiliwa, kwa kutambua wahamiaji kama zawadi kwa Kanisa, lakini pia kusisitiza uharaka wa kusindikizana nao na kuunga...

Kard.Re:Roho Mtakatifu aangazie makardinali kupata Papa anayehitajika kwa wakati wetu

Picha
Kardinali Re   (@Vatican Media) Katika misa kabla ya uchaguzi wa Papa mpya iliyoongozwa na Kadinali Re,Dekano wa Makardinali katika Kanisa Kuu la Vatican ameainisha kazi za kila mrithi wa Petro,kwa kuzingatia amri mpya ya upendo.Wito kwa makardinali wapiga kura:kuchagua kwa majukumu ya juu zaidi ya kibinadamu na ya kikanisa,kuepuka mawazo ya kibinafsi na kuangalia kwa manufaa ya Kanisa na ubinadamu. Na Angella Rwezaula – Vatican. Nitamwinua kuhani mwaminifu, atakayetenda sawasawa na haja za moyo wa Mungu ndiyo ilikuwa antifoni ya wimbo wa ufunguzi iliyosindikiza maandamano marefu ambayo asubuhi ya leo tarehe 7 Mei 2025 iliwaona  wakiingia makardinali wateule kwa upole kama kawaida katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican lililojaa waamini elfu tano, wakati wa Misa ya Pro eligendo Romano Pontifice, yaani kabla ya kuchagua Papa wa Roma. Aliyeongoza misa hiyo katika madhabahu ya kukiri ni Kardinali Giovanni Battista Re, Dekano wa Baraza la Makardinali. Katika mahali pa ...

Askofu Mkuu Gabriele Caccia, Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican katika Umoja wa Mataifa.

Picha
KILINGENI Vatican NEWS Askofu Mkuu Gabriele Caccia, Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican katika Umoja wa Mataifa. Ask.Caccia:Hakikisha mazingatio ya maadili ya AI yawe msingi na usambazaji wa maendeleo Vatican inasisitiza umuhimu wa kuhakikisha kwamba maendeleo na matumizi ya AI daima yanabaki katika huduma ya wanaume na wanawake,kukuza udugu na kuhifadhi fikra makini na uwezo wa utambuzi.Haya yameo katika hotuba ya Askofu Mkuu Caccia,Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican katika Umoja wa Mataifa huko New York,Marekani aliyotoa kwenye kikao maalum cha ECOSOC kuhusu Akili Mnemba jijini New York -Marekani tarehe 6 Mei 2025. Na Angela Rwezaula -Vatican. Askofu Mkuu Gabriele Caccia Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican katika Umoja wa Mataifa alitoa hotuba yake katika Mkutano Maalum wa Baraza la Kiuchumi na Kijamii (ECOSOC) ambalo ni jukwaa kuu la Umoja wa Mataifa, kuhusu Akili Mnemba tarehe 6 Mei 2025 huko mjini New York, Marekani. Katika Hotuba ya kikao cha kwanza kilichoongozwa na mada ya “Mitindo inayo...

Makardinali 133 wapiga kura wamewasili Roma na mada nyingi zinajadiliwa

Picha
  Makardinali wanaoendelea na maadalizi katika Mkutano wao,wapo wanajiandaa vema kwa ajili ya Mkutano Mkuu wa uchaguzi ujao na wakati huohuo mkutano wa 10 asubuhi Mei 5,mijadala yao ilihusu hali ya Kanisa na matumaini yao ya siku zijazo. Vatican News Jumatatu tarehe 5 Mei 2025, Makardinali wameendelea na mkutano wa kumi katika kujiandaa kwa ajili ya Mkutano Mkuu ujao wa uchaguzi wa Papa mpya na kuendeleza mijadala yao kuhusu hali ya Kanisa na matumaini yao ya siku zijazo. Msemaji mkuu wa Ofisi ya Waandishi wa Habari ya Vatican, Dk. Matteo Bruni, aliwaambia waandishi wa habari siku ya Jumatatu kwamba Makardinali 179, wakiwemo makardinali 132 wapiga kura, walishiriki katika Mkutano Mkuu wa kumi. Katika taarifa yake alibainisha kwamba Makardinali wote wapiga kura 133 wapo mjini Roma, kabla ya mkutano utakaoanza Jumatano tarehe 7 Mei 2025. Mkutano wa 10 wa makardinali   (@VATICAN MEDIA)   Kwa upande wa Kardinali Giovanni Battista Re, Dekano wa Baraza la Makardinali, aliliambi...

Kupaa kwa Yesu na Kumwagwa kwa Roho Mtakatifu

Picha
Somo la Kupaa kwa Yesu na Kumwagwa kwa Roho Mtakatifu Utangulizi Baada ya Yesu kufufuliwa kutoka kwa wafu, yeye      alijidhihirisha kwao, baada ya mateso yake, kwa dalili nyingi, akiwatokea siku arobaini, akinena habari za ufalme wa Mungu.      Matendo 1:3 Wanafunzi walipata uthibitisho usio na shaka kwamba Yesu alikuwa amefufuka kweli. Hili lilikuwa lazima, kwa sababu kila mmoja wao angeteseka sana kwa ajili ya Yesu. Haiwezekani kuvumilia mateso mengi kwa kitu ambacho huna uhakika nacho au ambacho unajua ni uwongo! Kupaa Baada ya zile siku arobaini, Yesu alikutana na wanafunzi wake na kuwaambia:      “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.”      Mathayo 28:18 Yesu alikuwa amemshinda Shetani na kumponda kichwa (akitimiza ahadi ambayo Mungu alimpa Hawa kwamba uzao wake ungeponda kichwa cha nyoka) Aliendelea:      "Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa...

MATESO YA YESU

Picha
Somo la Mateso ya Yesu Utangulizi Yesu hakuwa Mwokozi ambaye alitimiza matarajio ya watu. Viongozi wa kidini wa wakati wake walianza kumkasirikia. Hawakutaka kukubali kwamba yeye ndiye Masihi aliyeahidiwa, Mwana wa Mungu. Walichukizwa na ukweli kwamba watu wengi walipenda kumsikiliza Yesu badala ya kuwasikiliza. Walimchukia kwa kudai kuwa Mwana wa Mungu, kwa kusamehe dhambi (ni Mungu pekee awezaye kufanya hivyo) na kwa kuwaponya watu siku ya Sabato, siku takatifu ya pumziko. Mara nyingi walijaribu kumfanya Yesu aseme mambo ambayo yangemwingiza kwenye matatizo, lakini sikuzote aliona mtego huo. Hatimaye viongozi wa kidini walianza kupanga mipango ya kumwua Yesu na kuangamizwa pamoja naye milele. Wanafunzi wa Yesu Yesu alijua kwamba ingemlazimu kuteseka na kufa ili kutimiza mipango ya Mungu ya kutoa msamaha wa dhambi. Aliwaambia wanafunzi mara kadhaa kwamba jambo hilo lingetukia. Mmoja wa wanafunzi wake, Yuda, alikatishwa tamaa na Yesu. Hivi ndivyo alivyofanya:      Ki...