Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya ROMANI CATHOLIC

Makardinali 133 wapiga kura wamewasili Roma na mada nyingi zinajadiliwa

Picha
  Makardinali wanaoendelea na maadalizi katika Mkutano wao,wapo wanajiandaa vema kwa ajili ya Mkutano Mkuu wa uchaguzi ujao na wakati huohuo mkutano wa 10 asubuhi Mei 5,mijadala yao ilihusu hali ya Kanisa na matumaini yao ya siku zijazo. Vatican News Jumatatu tarehe 5 Mei 2025, Makardinali wameendelea na mkutano wa kumi katika kujiandaa kwa ajili ya Mkutano Mkuu ujao wa uchaguzi wa Papa mpya na kuendeleza mijadala yao kuhusu hali ya Kanisa na matumaini yao ya siku zijazo. Msemaji mkuu wa Ofisi ya Waandishi wa Habari ya Vatican, Dk. Matteo Bruni, aliwaambia waandishi wa habari siku ya Jumatatu kwamba Makardinali 179, wakiwemo makardinali 132 wapiga kura, walishiriki katika Mkutano Mkuu wa kumi. Katika taarifa yake alibainisha kwamba Makardinali wote wapiga kura 133 wapo mjini Roma, kabla ya mkutano utakaoanza Jumatano tarehe 7 Mei 2025. Mkutano wa 10 wa makardinali   (@VATICAN MEDIA)   Kwa upande wa Kardinali Giovanni Battista Re, Dekano wa Baraza la Makardinali, aliliambi...

Kupaa kwa Yesu na Kumwagwa kwa Roho Mtakatifu

Picha
Somo la Kupaa kwa Yesu na Kumwagwa kwa Roho Mtakatifu Utangulizi Baada ya Yesu kufufuliwa kutoka kwa wafu, yeye      alijidhihirisha kwao, baada ya mateso yake, kwa dalili nyingi, akiwatokea siku arobaini, akinena habari za ufalme wa Mungu.      Matendo 1:3 Wanafunzi walipata uthibitisho usio na shaka kwamba Yesu alikuwa amefufuka kweli. Hili lilikuwa lazima, kwa sababu kila mmoja wao angeteseka sana kwa ajili ya Yesu. Haiwezekani kuvumilia mateso mengi kwa kitu ambacho huna uhakika nacho au ambacho unajua ni uwongo! Kupaa Baada ya zile siku arobaini, Yesu alikutana na wanafunzi wake na kuwaambia:      “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.”      Mathayo 28:18 Yesu alikuwa amemshinda Shetani na kumponda kichwa (akitimiza ahadi ambayo Mungu alimpa Hawa kwamba uzao wake ungeponda kichwa cha nyoka) Aliendelea:      "Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa...

PAPA FRANCISCO NA MAPADRE WATANZANIA & CDF MABEYO

Picha
▪︎Katika picha ni Papa Francisco akiwa na Mapadre watanzania wanaosoma na kufanya utume wako nchini Italia pamoja Na Jenerali Venance Mabeyo, Mkuu wa Majeshi Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. ▪︎Ikumbukwe Maaskofu wote nchini Tanzania wako katika ziara ya Kichungaji yalipo makao makuu ya Kanisa Katoliki duniani mjini Vatican tangu May 14 hadi May 21, 2023. ▪︎Pia katika ziara hiyo wameambatana na Mapadre kadhaa akiwemo Padre Charles Kitima, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania, Padre Chesco Msaga C.PP.S Naibu Katibu Mkuu (TEC) bila kumsahau Padre Thomas Kiangio Msimamizi  wa Jimbo Katoliki Tanga. . . RADIO MARIA TANZANIA