Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya ETHIOPIA

TANZANIA YAUNGA MKONO UHURU WA CHAKULA KATIKA MKUTANO WA UNFSS+4 JIJINI ADDIS ABABA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), ameongoza ujumbe wa Tanzania katika mkutano wa ngazi ya Mawaziri uliofanyika tarehe 29 Julai 2025, jijini Addis Ababa, Ethiopia, uliokuwa sehemu ya Mkutano wa Pili wa Mfumo wa Chakula wa Umoja wa Mataifa (UNFSS+4). Katika hotuba yake kwenye majadiliano ya Meza ya Mawaziri kuhusu Uhuru wa Chakula na Njia za Kitaifa katika Kuharakisha Mageuzi ya Mifumo ya Chakula, Mhe. Kombo amesisitiza msimamo wa Tanzania wa kuunga mkono dhana ya uhuru wa chakula (food sovereignty), akisema ni haki ya jamii kuamua namna bora ya kuzalisha, kusambaza na kutumia chakula kulingana na mahitaji, tamaduni na vipaumbele vyao. Amesema kwa Tanzania, uhuru wa chakula si ndoto ya muda mrefu bali ni sharti la msingi kwa ustawi wa kizazi cha sasa na kijacho, hasa ikizingatiwa changamoto za mabadiliko ya tabianchi, kupanda kwa bei za chakula, upotevu wa mazao baada ya mavuno na usumbufu katika minyororo ya usambazaji ya ...

Watu wawili wapoteza maisha baada ya mlipuko wa bomu nchini Ethiopia

Picha
Maelfu walikusanyika kwenye mkutano wa Waziri mkuu Abiy Ahmed Maafisa nchini Ethiopia wamesema kuwa watu wawili wamepoteza maisha na wengine kadhaa wamejeruhiwa, baada ya mlipuko wa bomu kutokea kwenye mkutano wa kisiasa wa Waziri mkuu, Abiy Ahmed. Bwana Abiy amelitaja shambulio hilo kuwa ''jaribio lililoshindwa la vikosi ambavyo havitaki Ethiopia iungane''. Kiongozi huyo aliondolewa mara tu baada ya mlipuko, unaoelezwa wa guruneti linaloaminika kurushwa kati ya maelfu ya watu katika viwanja vya Meskel , mjini Adis Ababa Naibu mkuu wa Polisi mjini humo anashikiliwa kutokana na kushindwa kusimamia hali ya usalama katika eneo hilo. Maafisa wa polisi wanane wanashikiliwa na wakihojiwa kwa kushindwa kulilinda eneo lilofanyiwa mkutano Waziri wa afya nchini Ethiopia aliandika kwenye akaunti yake ya twitter kuwa watu wawili wamepoteza maisha na wengine 44 wako hospitalini, watano kati yao wakiwa na hali mbaya sana. Abiy alikuwa Waziri Mkuu baada ya...

Hatari tano kwa biashara Afrika Mashariki 2018

Picha
Kenya inarudi katika hali ya utulivu kisiasa baada ya uchaguzi wa rais uliochukua muda mrefu na uliokumbwa na misukosuko. Hata hivyo changamoto zitaendelea kuwepo mwaka huu kwa mashirika yanayohudumu nchini humo na Afrika Mashariki kwa ujumla. Hayo ni kwa mujibu wa shirika la kitaalamu Control Risks linalochambua hatari na udhibiti wa hatari za kibiashara na uwekezaji. Daniel Heal ambaye ni mshirika mkuu wa shirika hilo katika kanda ya Afrika Mashariki, amesema "mwaka 2018 ni mwaka wenye matumaini kwa Kenya na Afrika Mashariki. Tayari tumeanza kuona imani ya wawekezaji ikirejea taratibu kufuatia udhibiti wa kisasa Kenya na azma katika miradi mipya ya miundo mbinu Kenya na katika kanda hiyo kwa jumla. Tunatarajia hili kuendelea hadi mwisho wa mwaka huu." Hata hivyo Daniel anasema nchini Kenya, hitaji la kulipa awamu ya kwanza ya mkopo wa fedha za Eurobond ambazo zilikuwa dola milioni 774.8, linapaswa kuishawishi serikali kudhibiti ukopaji na matumizi kabla deni kufi...