
Korea Kaskazini inasema jaribio la hivi karibuni la makombora yake ni onyo kwa Marekani na Korea Kusini
Korea Kaskazini imeiba dola bilioni mbili (Ā£1.6bn) kufadhili mpango wake wa silaha kupitia uvamizi wa kimtando, inasema ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyovuja.
Ripoti hiyo ya kisiri inasema Pyongyang inalenga mabenki na na ubadilishanaji wa sarafu ya crypto-currency kukusanya pesa.
Vyanzo vya habari vimethibitishia BBC kwamba UN ilikuwa ikichunguza mashambulio 35 ya kimtandoa.
Korea Kaskazini ilifyetua makombora mawili siku ya Jumanne ikiwa ni mara ya nne imechukua hatua hiyo katika kipindi cha chini ya wiki mbili
Katika taarifa, Rais wa nchi hiyo Kim Jong-un amesema hatua hiyo ni onyo dhidi ya mazoezi ya pamoja ya kijeshi yanayofanywa na Marekani na Korea Kusini.
Pyongyang imeelezea kuwa mazoezi hayo yanakiuka mkataba wa amani.

How could war with North Korea unfold?
Ripoti t iliyovuja na ambayo ilitumwa kwa kamati ya vikwazo vya Korea Kaskazini katika Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa, inasema Pyongyang "ilitumia uhalifu wa hali ya juu wa kimtandao kuiba pesa kutoka kwa taasisi za kifedha na ubadilishanaji wa sarafu ya crypto-kukusanya mapato yake".
Wataalamu pia wanachunguza shughuli za kimtandao zinolenga malipo kupitia fedha za kigeni.
Ripoti hiyo imeongeza kuwa shambulio la Korea Kaskazini dhidi ya sarafu ya crypto- imeisaidia "kukusanya fedha kwa njia ambazo ni vigumu kutambuliwa na ikilinganishwa na ukaguzi wa kawaida unaofanywa na sekta ya benki".
Pia inasema Korea Kaskazini imekiuka vikwazo vua Umoja wa Mataifa kwa kutumia njia haramu ya kubadilishana fedha pamoja na kupata vifaa vya kutengeneza silaha ya maangamizi.
Tangu mwaka 2006, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa iliiwekea Korea Kaskazini vikwazo vya kuuza nje ya nchi hiyo bidhaa kama vile mkaa wa mawe, vyuma na vyakula vya baharini.
Pia iliwekewa kiwango cha uagizaji kutoka nje mafuta na bidhaa zake.

Kim Jong-un akifuatilia shughuli ya kufanyia majaribio makombora ya nchi yake
Kwa nini Korea Kaskazini inajaribu makombora?
Taarifa ya kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Korea Kaskazini inaeleza kuwa ushirikiano wa kijeshi baina ya Kusini na Marekani unawalazimu kuendelea kufanya ugunduzi na majaribio ya silaha mpya.
"Tunalazimika kuendelea, kujaribu na kutumia makombora mazito ambayo ni muhimu kwa kujilinda," imeeleza taarifa ya Kaskazini.
Taarifa hiyo pia imeeleza kuwa kinachoendelea baina ya Marekani na Korea ya Kusini ni uvunjwaji wa wazi wa mazungumzo ya hivi karibuni baina ya Marekani na Korea Kaskazini (DPRK).

Helikopta za Marekani pia zinahusika katika mazoezi ya kivita Korea Kusini
"Tumeshaonya mara kadhaa kuwa mazoezi ya kivita yatazorotesha mahusiano baina ya Marekani na Korea Kaskazini na mahusiano ya Korea zote mbili kwa ujumlana kutufanya tufikirie kurejea tena hatua zetu za awali," inaeleza taarifa ya Kakazini.
Kwa mujibu wa jeshi la Kusini, makombora yaliyorushwa siku ya Jumanne ni ya masafa mafupi yanayoenda mpaka kilomita 450.
Ndani ya wiki mbili zilizopita, Kaskazini imekuwa ikirusha aina mpya ya makombora ya masafa mafupi.
Ijumaa iliyopita ilirusha makombora mawili yaliyoangukia kwenye bahari ya Japani.

Marais Trump na Mr Kim mjini Hanoi, Vietnam
Kim Jong- un mwaka jana wakati wa mkutano wake na rais wa Marekani Donald Trump nchini Singapore alikubali kuwa atakomesha kufanyia majaribio silaha za nyuklia
Kim pia alikubali kuwa Korea Kaskazini haitarusha tena makombora ya masafa marefu.
Mkutano wa pili kati ya viongozi hao Hanoi, mwaka jana ulimalizika bila makubaliano yoyote.
Kutokea wakati huo mazungumzo ya nyuklia yamekwama japo pande zote mbili zimeonesha juhudi ya katatua suala hilo kwa njia ya kidiplomasia
Maoni