Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Urusi yakana kuwashambulia wapiganaji wanaoungwa mkono na Marekani nchini Syria

MTEULE THE BEST
A Su-24 bomber takes off from the an airbase in Syria (file picture)Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionUrusi yakana kuwashambulia wapiganaji wanaoungwa mkono na Marekani
Wizara ya ulinzi nchini Urusi imekana madai kuwa ndege zake zilishambulia wapiganaji wanaoungwa mkono na Marekani nchini Syria siku ya Jumapili.
Wizara hiyo ilisema kuwa jeshi lake la wanahewa lililenga wapiganaji wa Islamic State.
Jeshi la Urusi lilikuwa likijibu madai ya SDF ambao ni muungano wa wakurdi na makundi ya kiarabu kuwa wapiganaai wake sita walijeruhiwa kwenye mashambulizi ya angani ya Urusi mashariki mwa Syria.
Pro-Syrian government militiamen sit in the back of an armed vehicle in Bir Qabaqib, west of Deir al-Zour (4 September 2017)Haki miliki ya pichaAFP
Image captionUrusi yakana kuwashambulia wapiganaji wanaoungwa mkono na Marekani
SDF wanasonga mbele kuelekea mji wa Deir al-Zour ambapo vikosi vinavyoiunga mkono serikali , vinavyosaidiwa na Urusi, vinataka kuuteka mji huo kutoka kwa IS.
Siku ya Jumamosi Syrian Democratic Forces (SDF), walisema kuwa saa za asubuhi siku hiyo, wapiganaji wao mashariki mwa mto Euphrates walilengwa na ndege za Urusi pamoja na za Syria.
Lakini leo Jumapili msemaji wa wizara ya ulinzi ya Urusi meja jenerali Igor Konashenkov, alisema kuwa ndege za Urusi ziliwalenga wapiganaji wa IS katika mkoa wa Deir al-Zour.
Syrian army officers and pro-government militiamen inspect the desert from Bir Qabaqib, west of Deir al-Zour (4 September 2017)Haki miliki ya pichaAFP
Image captionUrusi yakana kuwashambulia wapiganaji wanaoungwa mkono na Marekani

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...