Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Maandamano baada ya polisi mzungu kuondolewa mashtaka ya kumuua mtu mweusi Marekani

MTEULE THE BEST
Protesters march through the West County Center in St Louis' Des Peres suburb. Photo: 16 September 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMaandamano baada ya polisi mzungu kuondolewa mashtaka ya kumuua mtu mweusi
Maandamano mapya yametokea katika mji wa St Louis nchini Marekani, ambapo polisi mzungu wa zamani alipatwa kutokuwa na hatia kwa kumuua mtu mweusi mwaka 2011.
Mamia ya watu waliandaanama katika mji wa Missouri kwa siku ya pili wakisema kuwa maisha ya weusi yana maana.
Zaidi ya waandamanaji 33 walikamatwa na polisi 11 kujeruhiwa wakati wa ghasia za siku ya Ijumaa usiku.
Polisi huyo Jason Stockley 36, aliondolewa mashtaka ya kumuua Antony Lamar Smitjh 24.
Jumamosi jioni, polis walitokea wakati waandamanaji walikusanyika katika mji wa St Louis.
Protesters clash with police in St Louis. Photo: 15 September 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMaandamano baada ya polisi mzungu kuondolewa mashtaka ya kumuua mtu mweusi
Umati ulitembea katika barabara za Des Peres na kufunga barabra moja kuu.
Bwana Smith alikuwa baba na alikuwa afunge ndoa wakati aliuawa tarehe 20 Desemba mwaka 2011.
Bwana Stockley na mwenzake walisema waliamini kuwa Bw Smith alikuwa akishriki katika kitendo kinachohusu madawa ya kulevya nje ya mkahawa.
Lamar SmithHaki miliki ya pichaCBS
Image captionBwana Smith alikuwa baba na alikuwa afunge ndoa wakati aliuawa tarehe 20 Desemba mwaka 2011.
Video ya polisi ilionyesha Bw Smith akirudisha gari nyuma kwenda kwa lile la polisi mara mbili katika jaribio la kutoroka.
Baada ya kumfuata kwa kasi kwa muda wa dakika tatu, Bw Stockley alimuambia mwenzake ambaye alikuwa akiendesha gari aligonge gari la Smith.
Bwa Stockley kisha akakimbia kwenda kwa dirisha la gari la Smith na kumfytulia risasi mara tano.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...