Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Iran alisema, "hotuba ya Trump ni ya wakati ya mikutano ya wanahabari wala sio kwa Umoja wa Mataifa.
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionHotuba ya Trump kwenye Umoja wa Mataifa yakosolewa
Korea Kaskazini bado haujajibu tisho la Trump kuwa itaharibiwa.
Hotuba ya Trump ilizungumzia zaidi dunia yenye mataifa huru ambayo yana malengo ya kuinua maisha ya watu wao, lakini akatumia muda mwingi akilenga kile alichokija kuwa mataifa yanayoleta matatizo duniani.
Marekani mara kwa mara imeionya Korea Kaskazini kwa majaribio yake ya zana, yanayokiuka maazimio ya Umoja wa Mataifa.
Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionMarekani mara kwa mara imeionya Korea Kaskazini kwa majaribio yake ya zana, yanayokiuka maazimio ya Umoja wa Mataifa
Siku ya Jumanne Trump alimkosoa Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un, akimtaja kuwa mtu wa makombora ambaye yuko katika harakati za kujitia kitanzi.
"Ikiwa Marekani italazimika kujilinda na washirika wake, hatutakuwa na cha kufanya bali tutaiharibu kabisa Korea Kaskazini," aliongeza Trump.
Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Sweden ambaye alikuwa ameketi katika kikao hicho, alisema kuwa ilikuwa hotuba mbaya, wakati usiofaa na kwa watu wasiostahili.
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionHotuba ya Trump kwenye Umoja wa Mataifa yakosolewa
Trump pia aliishambulia nchi ya Venezuela akitaja serikali yake kuwa fisadi na ya kiimla na kuonya kuwa Marekani iko tayari kuichukulia hatua.
Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Venezuela Jorge Arreaza alipinga kile alichokitaja kuwa vitisho.
"Trump sio rais wa dunia, hata hawezi kuongoza serikaii yake," alisema.
Haki miliki ya pichaUN / EVNImage captionWaakilishi kutoka Israel, Syria, Iran, na Saudi Arabia wakiisikiliza hotuba ya Trump
Akizungumza katika kikao hicho rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, aliteta mkataba wa nyuklia na Iran, akisema kuwa kuuvunja itakuwa makosa makubwa.
Lakini waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alimuunga mkono Bw. Trump. Kwenye hotuba yake aliseka mkataba wa Iran unastali kufanyiwa marekebisho au ufutwe kabisa, na kuonya dhidi ya kukua kwa ushawishi wa Iran eneo la mashariki ya kati.
SHERIA 17 ZA SOKA ======================= Mchezo wa soka ni moja ya michezo maarufu sana duniani na ni biashara kubwa sana katika ulimwengu wa michezo na ukitaka kuamini hili angalia makampuni yaliyowekeza katika kudhamini soka – ni makampuni makubwa makubwa yenye hadhi ya kitaifa na kimataifa. Kwa kuzingatia aina hii ya wadhamini, waendeshaji wa mchezo wa soka, wameweka kanuni na miongozo ya kufuatwa ili kuhakikisha kuwa wale wanaowekeza pesa zao wanaona thamani ya uwekezaji wao. Kwa hiyo soka kama ilivyo katika michezo mingine inazo kanuni na tutajadili kanuni moja baada ya nyingine kama zilivobainishwa katika muongozo wa FIFA unaojulikana kwa jina la Law of the Game. Sheria Namba 1: Dimba ============== NYASI - Dimba la soka litakuwa la nyasi asilia au bandia kulingana na kanuni za masindano na nyasi hizo lazima ziwe za rangi ya kijani. Kwa dimba la nyasi bandia na kama mchezo unaochezwa utakuwa wa kutambuliwa na FIFA, basi nyasi hizo bandia lazima zikidhi viwango maalumu ...
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST TUMSIFU YESU KRISTO WAPENDWA KATIKA BWANA!!! MADA YA LEO: KUMTUMAINIA MUNGU SOMO; zaburi 11:1-7 Kwake MWENYEZI-MUNGU nakimbilia usalama; mnawezaje basi kuniambia "ruka kama ndege mpaka mlimani" Maana waovu wanavuta pinde wameweka mishale tayari juu ya uta wawapige mshale watu wema gizani! Kama misingi ikiaribiwa mtu mwadilifu atafanya nini? MWENYEZI-MUNGU yumo hekaluni mwake takatifu ; kiti cha enzi cha MWENYEZI-MUNGU kiko mbinguni Kwa macho yake huwachungulia wanadamu na kujua kila kitu wanachofanya MWENYEZI-MUNGU hupima waadilifu na waovu huwachukia kabisa watu wakatili Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberti upepo wa hari ndiyo itakuwa adhabu yao MWENYEZI-MUNGU ni mwadilifu na apenda uadilifu watu wanyoofu watakaa pamoja naye NENO LA BWANA Unaruhusiwa kuchangia funguka tupate maoni yako MUNGU AKUBARIKI
Maoni