Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Iran alisema, "hotuba ya Trump ni ya wakati ya mikutano ya wanahabari wala sio kwa Umoja wa Mataifa.
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionHotuba ya Trump kwenye Umoja wa Mataifa yakosolewa
Korea Kaskazini bado haujajibu tisho la Trump kuwa itaharibiwa.
Hotuba ya Trump ilizungumzia zaidi dunia yenye mataifa huru ambayo yana malengo ya kuinua maisha ya watu wao, lakini akatumia muda mwingi akilenga kile alichokija kuwa mataifa yanayoleta matatizo duniani.
Marekani mara kwa mara imeionya Korea Kaskazini kwa majaribio yake ya zana, yanayokiuka maazimio ya Umoja wa Mataifa.
Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionMarekani mara kwa mara imeionya Korea Kaskazini kwa majaribio yake ya zana, yanayokiuka maazimio ya Umoja wa Mataifa
Siku ya Jumanne Trump alimkosoa Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un, akimtaja kuwa mtu wa makombora ambaye yuko katika harakati za kujitia kitanzi.
"Ikiwa Marekani italazimika kujilinda na washirika wake, hatutakuwa na cha kufanya bali tutaiharibu kabisa Korea Kaskazini," aliongeza Trump.
Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Sweden ambaye alikuwa ameketi katika kikao hicho, alisema kuwa ilikuwa hotuba mbaya, wakati usiofaa na kwa watu wasiostahili.
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionHotuba ya Trump kwenye Umoja wa Mataifa yakosolewa
Trump pia aliishambulia nchi ya Venezuela akitaja serikali yake kuwa fisadi na ya kiimla na kuonya kuwa Marekani iko tayari kuichukulia hatua.
Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Venezuela Jorge Arreaza alipinga kile alichokitaja kuwa vitisho.
"Trump sio rais wa dunia, hata hawezi kuongoza serikaii yake," alisema.
Haki miliki ya pichaUN / EVNImage captionWaakilishi kutoka Israel, Syria, Iran, na Saudi Arabia wakiisikiliza hotuba ya Trump
Akizungumza katika kikao hicho rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, aliteta mkataba wa nyuklia na Iran, akisema kuwa kuuvunja itakuwa makosa makubwa.
Lakini waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alimuunga mkono Bw. Trump. Kwenye hotuba yake aliseka mkataba wa Iran unastali kufanyiwa marekebisho au ufutwe kabisa, na kuonya dhidi ya kukua kwa ushawishi wa Iran eneo la mashariki ya kati.
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.
Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...
Maoni