Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Idadi ya watu waliothibitishwa kufariki kufuatia tetemeko kubwa la ardhi lililoikumba Ecuador imegonga 233



Idadi ya watu waliothibitishwa kufariki kufuatia tetemeko kubwa la ardhi lililoikumba Ecuador imegonga 233 na kunahofu idadi hiyo itaongezeka maradufu.
Rais wa taifa hilo Rafael Correa amesema katika hotuba fupi kuwa wanajeshi elfu kumi (10,000) wametumwa kusaidia na shughuli za uokozi.
Aidha Polisi 3,500 pia watajiunga nao kusaidia kuokoa maisha ya majeruhi wa janga hilo la kitaifa.
Tetemeko hilo kubwa lililotikisa maeneo ya Kusini mwa pwani ya Ecuador lilikuwa la kiwango cha 7.8 kwenye vipimo vya Richter.

Makamu wa rais wa nchi hiyo ametangaza hali ya tahadhari katika mikoa sita nchini humo, huku maafisa wa huduma za dharura wamepelekwa kusaidia .
Kitovu chake kilikuwa takriban kilomita 27 kutoka kwa mji wa pwani uitwao Muisne mji ambao kwa kawaida hauna wakaazi wengi.
Maafisa wakuu wanahofia kuwa idadi hiyo ya vifo huenda ikaongezeka kwani maeneo ya mashambani mbali na kitovu cha tetemeko hilo yaani mji wa pwani wa Muisne ndiyo yameanza kutoa taarifa kwa vyombo vya dola kuhusu athari ya tetemeko hilo.
Maafisa katika kituo cha Marekani cha utafiti wa kijiologia wamesema tetemeko hilo la ardhi lilitikisa hadi sehemu ya mpakani na taifa jirani ya Colombia.
Image copyright AFP

 

Rais Correa amewahakikishia wahasiriwa wa mkasa huo kuwa msaada wa serikali uko njiani.
Hata hivyo mabasi na malori ya kijeshi yanatatizika kuwafikia wahanga walioporomokewa na majengo yao kufuatia maporomoko makubwa ya ardhi yaliyoziba mabarabara.
Aidha misaada ya chakula na madawa kutoka mataifa jirani yameanza kupokewa kutoka Venezuela na Mexico.

Takriban watu 600 wamejeruhiwa japokuwa idadi hiyo bila shaka inatarajiwa kupanda.
Meya wa mji wa Pedernales Gabriel Alcivar amesema kuwa mji wote umeporomoka

Mji wa Guayaquil ulioko takriban kilomita 300km kutoka kitovu cha tetemeko hilo pia limeathirika vibaya na hata daraja la pekee linaloiunganisha limeporomoka.
Visa vya utovu wa nidhamu pia vimeripotiwa huku watu wakipora majengo ya watu na maduka

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...