Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Zitambue faida za smatphones na athari zake na smatphone ya kwanza duniani

MTEULE THE BEST

Tokeo la picha la smat phone

Miaka 20 ya Smartphone Barani Afrika

Tokeo la picha la smat phone
Miaka 20 tangu simu ya "Smartphone" ilipoingia kwenye soko la mawasiliano, na kuleta mapinduzi ya kimawasiliano barani Afrika, ambako sasa inatumika kama chombo cha kupashana habari za kiuchumi, kijamii na kisiasa
Pokemon Go in Afrika
Waafrika wasiopungua milioni 80 walikuwa na simu ya mkononi mnamo mwaka 1999. Mwaka 2008 idadi hiyo iliongezeka na kufikia watu 500 milioni - hiyo ikiwa sawa na asilimia 60 ya wakaazi jumla wa bara la Afrika. Mnamo mwaka 2015, kwa mujibu wa kamapuni inayotengeneza simu za mkononi chapa Ericsson, kulikuwa na mikataba takriban bilioni moja ya simu za mkononi kote barani Afrika. Wataalam wanakadiria kuna simu bilioni mbili za mkononi zinazokutikana barani Afrika na katika eneo la Mashariki ya Kati. Nusu ya simu hizo ni aina ya Smartphones, anasema mkurugenzi wa kanda ya kusini mwa Afrika wa shirika la kimataifa la Data Corpotration - IDC, Martin Walker:"Kuendelea kupungua thamani kwa teknolojia ya Smartphone na kuzidi kuboreka kwa mawasiliano kupitia mtandao pamoja pia na kuongezeka nguvu za mtandao hadi kufikia 3G na 4G -yote hayo yamechangia kuifanya Smarthphone izidi kuwavutia watu. Wakati huo huo, ufundi wa kutengeneza Smarthphone kuambatana na mahitaji ya bara la Afrika umeongezeka katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita."
Smartphone kama chombo cha kuitisha maandamano

Ramani ya jinsi Smarphone ilivyoenea Afrika na Mashariki ya kati
Hadi mwaka 2017, idadi ya Waafrika wanmaotumia simu za mkononi aina ya Smartphone inatarajiwa kuongezeka mara dufu. Kwa mujibu wa taasisi ya ushauri wa masuala ya kiuchumi - Deloitte, hadi ifikapo mwakani barani Afrika kutakuwa na simu zaidi ya milioni 350 za mkononi zenye mtandao wa intaneti. Hiyo ni fursa kubwa kwa wenye kutengeneza programu za kibiashara kupitia simu za mkononi na kwa mahitaji ya Waafrika. Hata hivyo, simu za mkononi hazitumiwi pekee kwaajili ya masuala ya kiuchumi. Kutokana na kuwepo simu zaidi za mkononi barani Afrika, watu wanazitumia simu hizo za tekonolojia ya kimamboleo pia kuitisha maandamano ya kisiasa dhidi ya tawala zao.
Kwa mujibu wa Professor Marco Manacorda wa Chuo Kikuu cha Queen Mary cha mjini London, simu za mkononi zinatumika pia kueneza ripoti kuhusu hali ya kisiasa na kiuchumi kwa haraka zaidi. Anasema kwa kupashana habari watu wanafanikiwa kujuana pia.
Serikali hazipakati mikono

Smartphone ya kwanza kabisa duniani
Prof. Manacorda anahisi serikali pia zinajifunza jinsi ya kuitumia teknolojia hiyo mpya ya mawasiliano kama chombo cha upelelezi. Na mara nyingi wanazifunga njia hizo za mawasiliano.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...