Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda Wasanii kutumia mitandao kutangaza utalii

Picha za Amber Rutty zinaleta joto DSM" - Makonda Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amewataka wasanii kutumia mitandao ya Kijamii kuhamasisha masuala ya Utalii wa nchi ili waweze kuitangaza Tanzania kupitia wafuasi wao wa mitandao ya kijamii ambao wanapatikana nchi mbalimbali. Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda (kulia), na Amber Rutty. Akizungumza Jijini Dar es salaam, mbele ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, pamoja na Waziri Maliasili na Utalii Dkt Hamis Kigwangalla, Makonda amewataka wasanii wapewe nafasi ya kutangaza utalii huo. Makonda amesema " niwaombe wananchi wa Dar es salaam tutumie fursa hii kutangaza utalii wetu, niwaombe wasanii wenye wafuasi mitandaoni watangaze utalii wetu hapa nchini ili dunia ifahamu kuliko kusambaza picha za Amber Rutty ambazo zinaleta joto kali na laana ". " Tunatamani Dar es salaam isiwe sehemu ya kupita bali iwe sehemu ya watu kukaa, kwa sababu tuna maeneo ya utalii, ikiwemo ghorofa la kwanza kujengwa Ta...

Msanii wa The Mafik akamatwa kwa wizi

Msanii wa kundi la The Mafik anayejulikana kwa jina la Mbalamwezi, amekamatwa na jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni kwa tuhuma za wizi. Wasanii wanaounda kundi la The Mafik, Hamadai (kushoto) Mbalamwezi (kati kati) na Rhino (kulia) Tukio hilo limetokea hapo jana baada ya msanii huyo kumuibia dereva wa gari ya moja ya kampuni zinazotoa huduma za usafiri binafsi jijini Dar es salaam (Taxify), aliyejulikana kwa jina la Calvin. Akisimulia tukio hilo Calvin amesema Mbalamwezi aliitisha usafiri akitumia simu ya mwenzake, lakini alipokuwa njiani alionekana kuwapigia simu watu kuomba hela kwani hakuwa na pesa ya kumlipa dereva, na ndipo alipochukua uamuzi wa kumuibia dereva baada ya kumfanya apoteze fahamu. Meneja wa kundi la The Mafik aliyejitambulisha kwa jina la Kapasta amesema ni kweli kuna hilo tukio, lakini ndio yuko njiani akielekea kituo cha Polisi Oysterbay ambako msanii huyo amewekwa rumande ili ajue kinachoendelea. East Africa Television ilifanya jitihada za kumtafuta Kama...

Bunge la Umoja wa Ulaya latoa azimio la kulinda haki za binadamu Tanzania

Rais wa Tanzania akiwa na mjumbe wa Umoja wa Ulaya Tanzania, Balozi Roeland van de Geer Bunge la Umoja wa Ulaya limetoa njia iitakayo kwa mustakabali wao juu ya uhusiano kati yao na Tanzania kutokana kile walichokiita kuongezeka kwa ukiukwaji wa haki za binaadamu Tanzania. Azimio hilo limeeleza namna ambavyo hali ya kisiasa nchini Tanzania inavyokandamiza uhuru wa wananchi kutokana na sheria kali zilizopo dhidi ya asasi za kiraia, watetezi wa haki za binadamu, vyombo vya habari na vyama vya siasa na huku hofu kubwa ikitanda kwa wapenzi wa jinsia moja. Vilevile wamekemea matukio yote ya chuki na vurugu dhidi ya wapenzi wa jinsia moja na kuitaka serikali ya Tanzania kuhakikisha kuwa Paul Makonda anaacha kuwatishia watu jamii hiyo na haki kutendeka. Hata hivyoserikali ya Tanzania ilijitenga na msimamo wa kiongozi huyo wa Dar es salaam. Bunge hilo limetaka uchunguzi huru kufanyika ili ukweli juu ya mashambulio na unyanyasaji dhidi ya waandishi wa habari, wapenzi wa jinsia mo...

Benki ya TIB imetoa taarifa ya kusikitishwa

Benki ya TIB imetoa taarifa ya kusikitishwa kwake na kitendo cha dereva wa gari inayomilikiwa na benki hiyo yenye namba za usajili SU 38431 cha kubeba mbuzi kwenye tairi ya akiba iliyopo nyuma ya gari. Kwenye taarifa hiyo ambayo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TIB Tawi la Mlimani City, imeeleza ni kwa namna gani dereva huyo ametumia mali ya umma vibaya, na pia kukiuka haki za wanyama. Benki hiyo imesema itamchukulia hatua stahiki dereva huyo, ambaye alikuwa akiendesha gari hilo kutoka Mwanza kuelekea jijini Dar es salaam.

TFF YA THIBITISHA TIMU HAZIJAPEWA PESA ZA UBIGWA

'Simba na Mtibwa hazijapewa fedha za ubingwa'' Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kupitia kwa katibu Mkuu wake, Kidao Wilfred, limeweka wazi kuwa mabingwa wa michuano ya kombe la shirikisho nchini, ambao ni Simba na Mtibwa Sugar bado hawajapewa fedha za ubingwa. Wachezaji wa Simba walipokabidhiwa ubingwa wa ligi kuu. Akionge leo na wana habari Kidao amefafanua mambo mbalimbali likiwemo hilo la fedha za zawadi ya mashindano hayo ambapo ameweka wazi kuwa hata Simba bado hawajapewa. ''Ni kweli Mtibwa Sugar hawajapata fedha zao milioni 50 za ushindi wa Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) msimu uliopita 2017/18 lakini hata Simba ambao ni mabingwa wa msimu wa 2016/17 nao hawajapata kuna vitu tunaweka sawa'', amesema. Kidao amesema kwamba sababu kubwa ni kuwa kuna vitu vya kimkataba baina yao na wadhamini vinafanyiwa marekebisho kutokana na uongozi kuwa mpya madarakani hivyo kuna mapitio ya kuboresha vipengele vya mkataba na fedha hiz...

Museveni: siwezikuachia kiti cha urasi

Museveni aweka wazi mipango ya kutoachia madaraka Rais wa Uganda, Yoweri Kaguta Museveni, amewaambia wazi wapinzani wake kuwa hana mpango wa kuachia madaraka hivi karibuni, hivyo waachane na mawazo yao ya kuwaza kiti hicho. Rais Museveni ameyasema hayo kwenye mkutano wa ndani wa chama ambao uliwakusanya pamoja viongozi wa vyama vilivyopo Bungeni, mkutano uliofanyika Jijini Kampala. Museveni amesema amefurahia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea kwenye mkutano huo, ambapo aliwaambia wapinzani wake kwamba hatofikiria kubadilishana madaraka mpaka pale atakaporidhishwa na Ustawi na usalama wa kimkakati wa nchi za Afrika. “Nasikia watu kama Mao wanazungumzia kuachia madaraka, ni kwa namna gani watakaa kwenye umati na kumuona Museveni akikabidhi madaraka. Hicho ndicho kitu muhimu kwake. Sidhani kama ni sahihi kwa yeye kusema hivyo, badala ya kuzungumzia hatma ya Afrika, mnaongelea vitu visivyo na maana, uchaguzi, nani atakuwa nani. Na ndio kwa sababu nilisema kama bado nina ...

Rais wa Venezuela Nicolas Maduro Marekani inapanga njama ya kumuua na kupindua serikali yake

John Bolton amepewa jukumu la kupanga jinsi ya kuniangamiza' Rais wa Venezuela Nicolas Maduro akizungumza na wanahabari mjini Caracas Desmba 12,2018 Rais wa Venezuela Nicolás Maduro amedai kuwa Marekani inapanga njama ya kumuua na kupindua serikali yake. Amewaambia wanahabari kuwa mshauri wa usalama wa kitaifa wa Marekani John Bolton, anahusuka moja kwa moja na njama hiyo japo hakutoa ushahidi wowote kuthibitisha madai hayo. Rais Trump amemtaja Maduro kama kiongozi wa kiimla na kumwekea vikwazo. Mapema wiki hii maafisa wakuu wa Urusi na Marekani walijibizana baada ya ndege mbili kubwa za kuangusha mabomu za Urusi kutua nchini Venezuela, taifa linalopatikana Amerika Kusini. Ndege hizo za kivita aina ya Tu-160 zilitua Venezuela Jumatatu katika kile kinachoonekana kama jaribio la kuonyesha uungaji mkono wa Urusi kwa rais wa kisoshialisti wa Venezuela Nicolás Maduro ambaye amekuwa akikabiliwa na shinikizo. Ndege hizo mbili zina uwezo wa kubeba silaha za nyuklia. Madur...