Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Hoteli ya Intercontinental Mjini Kabul yavamiwa na magaidi


Walinda usalama wa Afghanistan wamechukua udhibiti wa baadhi za ghorofa ya jumba hilo la Hoteli

Msemaji wa Wizara ya usalama wa ndani nchini humo amesema kwamba, washambuliaji wawili kati ya wavamizi wanne, tayari wameuwawa.

Yamkini watu 20 wanahofiwa kuwawa baada ya hoteli maarufu ya Intercontinental mjini Kabul, Afghanistan kushambuliwa na magaidi.


Wanajeshi wa Afghanistan, wamekuwa wakipigana ghorofa baada ya ghorofa, ili kuchukua udhibiti wa hoteli moja ya kifahari katika mji mkuu Kabul, baada ya kuvamiwa na wapiganaji waliokuwa na silaha nzito nzito.


Msemaji wa Wizara ya usalama wa ndani nchini humo amesema kwamba, washambuliaji wawili kati ya wavamizi wanne, tayari wameuwawa.


Washambuliaji hao walivamia Hoteli ya Intercontinental jana Jumamosi jioni, na kuanza kuwamiminia risasi wageni na wafanyikazi pamoja na kurusha magruneti.


Msemaji wa Wizara ya usalama wa ndani nchini humo, Nasrat Rahimi, ameiambia BBC kuwa, walinda usalama wamechukua udhibiti wa ghorofa ya kwanza ya kifahari ya hoteli hiyo, lakini baadhi ya washambuliaji bado wangali katika orofa zingine hotelini.


Picha ya maktaba: The Intercontinental Hotel, picha iliyopigwa Januari 2016


Taarifa zingine zinasema kwamba, wakati wa uvamizi huo, hoteli hiyo ilikuwa inaandaa kongamano la Teknolojia ya mawasiliani (IT) iliyokuwa inahudhuriwa na maafisa wa mikoa.


Shahidi mmoja ameiambia shirika la habari la Reuters kuwa, washambuliaji hao wanawazuilia baadhi ya watu kama mateka.


Shambulio hilo linatokea siku kadhaa baada ya ubalozi wa Marekani mjini Kabul, kutoa tahadhari ya uwezekano wa kutokea shambulio la kigaidi lililolenga mahoteli kadhaa mjini Kabul.


Kufikia sasa haijabainika ni watu wangapi wameuwawa au kujeruhiwa, lakini taarifa ambazo bado hazijathibitishwa na BBC, zinaasema kuwa watu 15 wameuwawa.


Ramani ya Afghanistan


Sehemu moja ya jumba la Hoteli hiyo inateketea, huku makabiliano makali ya risasi yakiendelea.


Jumba la Hoteli hiyo ya Intercontinental, linachukuliwa kama nembo ya mji mkuu Kabul.


Hoteli hiyo ilishambuliwa na kundi la wapiganaji wa Taliban, miaka 7 iliyopita


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...