BAADA ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutangaza kuanza mchakato wa kumsaka kocha mpya wa Taifa Stars, Mbelgiji, Adel Amrouche ameibuka na kufunguka kuwa, akipewa nafasi ya kuinoa timu hiyo, ataipambania ishiriki Kombe la Dunia mwaka 2022 nchini Qatar.
Mbali na Kombe la Dunia, pia Mbelgiji huyo mwenye asili ya Algeria, amesema ataanza kwanza kupambana kuhakikisha Taifa Stars inashiriki Kombe la Mataifa Afrika (Afcon) inayotarajiwa kufanyika mwakani nchini Cameroon.
Hivi karibuni, Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Kidao Wilfred, alisema mchakato huo wa kumsaka kocha, unaendelea vizuri ambapo wanaanza kupitia wasifu āCVā mbalimbali za makocha walioomba nafasi hiyo baada ya kocha wa sasa, Salum Mayanga kumaliza mkataba wake tangu mwezi uliopita.
Akizungumza na Championi Jumatatu , Kocha Amrouche aliyezaliwa Machi 7, 1968 katika Mji wa Kouba, Algiers nchini Algeria, amesema: āNina uzoefu na soka la Afrika, nimefundisha timu ya taifa ya Kenya na Burundi, lakini pia kwenye klabu, nimefundisha DC Motema Pembe ya DR Congo na USM Alger ya Algeria.
āNajiamini na ndiyo maana nimekuwa nikitamani sana kuifundisha Taifa Stars ambayo imekuwa na kiu kubwa ya mafanikio, kama nikifanikiwa kuwa kocha wa timu hiyo, nitahakikisha mwakani tunaĀshiriki Afcon, kisha 2022 lazima twende kushiriki Kombe la Dunia. Hayo yote yanawezekana kwani ikiwekwa mikakati madhubuti nadhani hakuna kitakachoshindikana.ā
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni