Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mnangagwa anusurika jaribio la mauaji

Picha za televisheni ya shirika la utangazaji la Zimbabwe zimeonesha mripuko mkubwa kwenye mkutano wa hadhara uliokuwa ukihutubiwa na Rais Emmerson Mnangagwa katika kile kinachotajwa kuwa jaribio la mauaji dhidi yake.


Msemaji wake, George Charamba, aliliambia shirika la habari la Reuters kwamba rais huyo mwenye umri wa miaka 75, ambaye kwenye mkutano huo alikuwa ameambatana na makamu wake wawili, yuko salama kwenye ikulu ndogo mjini humo.


"Rais ameondoshwa akiwa salama. Yuko kwenye nyumba ya serikali ya Bulawayo. Tunashukuru kwamba ulikuwa ni mripuko, na kwa hakika ulitokezea karibu sana na jukwaa kuu," alisema Charamba.


Shahidi mmoja ameliambia shirika la habari la Associated Press kwamba mripuko ulitokea muda mchache baada ya Mnangagwa kumaliza hotuba yake na wakati akiondoka jukwaani.


Picha zilizotumwa mitandaoni zinamuonesha kiongozi huyo akiwapungia mkono wafuasi wake, akinyanyua hatua kuondoka jukwaani na kuanza kutembea kutoka meza kuu, ambapo sekunde chache baadaye mripuko unasikika. Watu walipiga makelele na moshi mkubwa kushuhudiwa.






Televisheni ya serikali ambayo ilikuwa ikirusha moja kwa moja mkutano huo, ilikatisha ghafla matangazo yake.


Makamu wa Rais miongoni mwa majeruhi


Makamu wote wawili wa rais - Constantino Chiwega na Kembo Mohadi wamejeruhiwa, sambamba na maafisa kadhaa wa chama tawala cha ZANU-PF, huku duru za kisiasa nchini Zimbabwe zikisema kwamba mashambulizi hayo yalikuwa ni jaribio la mauaji dhidi ya Mnangagwa. 


Makamu wa Rais Jenerali Constantino Chimwega ni miongoni mwa waliojeruhiwa.


Mwandishi wa shirika la habari la Ufaransa, AFP, aliripoti kushuhudia watu kadhaa waliojeruhiwa ingawa hakuweza kutaja idadi kamili.


Picha za televisheni zinaonesha mtafaruku ukitokea, huku madaktari wakijaribu kuwaokoa waliojeruhiwa kwenye mripuko huo katika uwanja wa White City. 


Mnagangwa alikuwa kwenye mji huo akijaribu kuwashawishi wapigakura kumchaguwa kwenye uchaguzi wa tarehe 30 Julai.


Huu utakuwa uchaguzi wa kwanza tangu mwanajeshi huyo wa zamani kumuondoa madarakani kwa mapinduzi baridi mshirika wake mkuu wa zamani, Robert Mugabe, mwezi Novemba mwaka jana baada ya kuwapo madarakani kwa miaka 37.


Uchaguzi huo utakuwa kipimo muhimu kwa Mnangagwa, ambaye ameahidi kuwa utakuwa huru na wa haki, katika wakati ambapo anaonekana kujaribu kujenga mahusiano mapya na jamii ya kimataifa.


Msemaji wa Rais Mnangagwa aliliambia gazeti la Zimbabwe Herald kuwa uchunguzi unaendelea, akisema kuwa kumekuwa na majaribio kadhaa ya kumuua rais huyo kwa kipindi kirefu.


Kama ilivyotokea Addis Ababa


Mripuko huo ulitokea masaa machache baada ya mwengine kama huo kutokea nchini Ethiopia, ambako mtu mmoja anatajwa kuuawa na wengine zaidi ya 80 kujeruhiwa, baada ya waziri mkuu mpya kuhutubia mkutano mkubwa wa hadhara kwenye mji mkuu, Addis Ababa. 


Mkutano wa hadhara wa Waziri Mkuu Abiy Ahmed wa Ethiopia nao pia ulikumbwa na mkasa huo wa mashambulizi masaa machache kabla ya wa Mnangagwa.


Mripuko ulisikika muda mchache baada ya Abiy Ahmed kumaliza hotuba yake katikati ya Addis Ababa, na kuwasababishia watu kukimbia kunusuru maisha yao. Waziri mkuu huyo aliwahiwa kukimbizwa akiwa salama.


Awali Abiy alikuwa ameliambia shirika la habari la FBC kuwa "watu wachache wameuawa na ni mashahidi wa upendo na amani," lakini taarifa za baadaye kutoka ofisi yake zilisema hakuna aliyepoteza maisha kwenye mripuko huo. 


Waziri mkuu huyo mwenye umri wa miaka 42 alisema mripuko huo "yalikuwa mashambulizi yaliyopangwa vyema lakini yaliyoshindwa." Hata hivyo, hakurusha lawama zake kwa kundi lolote, ingawa alisema polisi wanaendelea na uchunguzi, akiongeza kuwa "mashambulizi hayo yalikuwa ya kitoto na yasiyokubalika. Daima mapenzi yatashinda. Kuwauwa wengine ni kushindwa. Kwa wale wanaojaribu kutugawa, nataka kuwaambia kuwa hamujafanikiwa."


Mripuko huo kwenye Uwanja wa Meskel uliokuwa umejaa watu mjini Addis Ababa, ulitokea baada ya wiki kadhaa za mageuzi makubwa kabisa ambayo yamewashitua wengi kwenye taifa hilo la pili kwa idadi ya watu barani Afrika, na baada ya miaka kadhaa ya hasira kali dhidi ya serikali, hali ya hatari, watu kukamatwa ovyo na kufungiwa kwa huduma za intaneti.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...