Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mfungwa achagua kuuawa kwa kutumika kiti cha umeme badala ya sindano ya sumu Marekani




The electric chair has gradually been replaced as the main method of execution

Mfungwa mmoja katika jimbo la Tennessee nchini Marekani atauawa kwa kiti cha umeme baada ya kudai kuwa sindano ya sumu itasababisha ateseke.

David Earl Miller, ambaye amekuwa kwenye hukumu ya kifo kwa miaka 36 ni kati ya wafungwa wanaoongezeka wanaojaribu kukwepa sindano ya sumu kufuatia visa kadhaa vya kufeli.

Mfungwa mwingine huko Tennessee Edmund Zagorski, aliuawa kwa njia ya umeme mwezi uliopita.

Kuuliwa kwa kutumia sindano ya sumu ndiyo njia kuu ya kuwaua wafungwa katika jimbo hilo.

Hata hivyo wafungwa katika jimbo hilo ambao walitenda uhalifu kabla ya mwaka 1999 wataruhusiwa kuchagua kuuliwa kwa njia ya umeme.

Mahakamani, Miller na Zagorski walitaja kisa cha kuuuliwa Billy Ray Irick cha mwezi Agosti ambaye alibadilika rangi kuwa Zambarau na kuchukua dakika 20 kufa.



Kuuliwa kwa Zagorski ilikuwa mara ya pili kiti cha umeme kimetumiwa katika jimbo hilo tangu mwaka 1960.

Miller alikutwa na hatia ya kumuua mwanamke aliyekuwa na matatizo ya akili mwenye miaka 23 mwaka 1981.

Ni kwa nini sindano ya sumu ina utata?

Miller, 61, na Zagorski, 63, walidai kuwa sindano hiyo ya sumu inayotumiwa na jimbo la Tennesee itasababisha kifo kirefu na chenye uchungu.

Hii ni baada mauaji kadhaa yaliyofanyika kwa kutumia mchanganyiko wa dawa ambapo wafungwa wameonekana wakiteseka.


Tennessee ilitumia kiti cha umeme kumuua Edmund Zagorski mwezi uliopita

Mwezi Septemba daktari mmoja aliiambia mahakama huko Tennessee kuwa Irick alihisi uchungu sawa na mateso wakati akiuawa.

Hata hivyo wale wanaounga mkono kutumika kwa sindano ya sumu wanasema haisababishi uchungu.

Miller pia ni mmoja wa wafungwa wanne waliohukumiwa kifo ambao wamepeleka kesi mahakamani wakitaka jimbo la Tennesee kutumia risasi badala ya sindano au umeme.

Katika jimbo jirani la Alabama, zaidi ya wafungwa 50 wamechagua kuuawa kwa kutumia gesi ya nitrogen badala la sindano ya sumu baada ya kuruhusiwa kuchagua mapema mwaka huu.

Ni majimbo yapi yanatumia kiti cha umeme?

Kutumika kwa umeme sio tena njia kuu ya kuwaua wafungwa katika jimbo lolote nchini Marekani.



Mahakama huko Georgia na Nebraska zimesema kuwa kiti cha umeme ni kinyume cha katiba.

Hata hivyo Miller ameambiwa kuwa hawezi kudai kuwa kiti cha umeme ni kinyume na katiba kwa sababu yeye mwenyewe amekichagua.

Kunyongwa ilikuwa njia kuu ya kuwaua wafungwa nchini Marekani hadi miaka ya 1890. Kisha kiti cha umeme kikaanza kutumika kwa wingi.

Mwaka 1982 matumizi ya kwanza ya sindano ya sumu yalifanyika katika jimbo la Texas na kuchukua taratibu mahala pa kiti cha umeme

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...