Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUTANA NA TIMU IYOFUNGWA GOLI 20 JUMAPILI HII

Klabu ya Pro Piacenza yalazwa 20-0 katika mechi ya ligi Serie C

Iwapo unadhania timu yako imekuwa na msururu wa matokeo mabaya wikendi hii basi fikiria kichapo hiki walichopewa Pro Piacenza katika ligi ya Itali.


Klabu hiyo ya ligi ya Serie C iliowekwa katika kundi A ilishindwa magoli 20-0, 'ndio magoli ishirini bila jibu' na wapinzani wao katika ligi hiyo Cuneo siku ya Jumapili jioni.

Walikuwa nyuma kwa magoli 16 kwa bila wakati wa muda wa mapumziko huku mshambuliaji wa Cuneo Hicham Kanis akifunga magoli sita pekee kabla ya mapumziko naye mshambuliaji mwenza Eduardo Defendi akipata magili matano.


Katika safu ya ulinzi ya Pro Piacenza kulikuwa na matatizo yaliosababisha mvua hiyo ya magoli. Wakiwa chini katika ligi hiyo ya tatu ya Itali, klabu hiyo ya kaskazini ina matatizo makubwa ya ufadhili.

Walipokonywa pointi nane mapema katika kampeni yao na wameripotiwa kushindwa kuwalipa wachezaji wao tangu mwezi Agosti hatua iliosababisha kujiuzulu kwa wachezaji wengi wa kikosi cha kwanza.

Walishindwa kushiriki katika mechi tatu kabla ya kichapo hicho cha siku ya Jumapili na iwapo hawangeshiriki ingesababisha kupigwa marufuku katika ligi hiyo ya Serie C.

Wageni hao walichezesha wachezaji wao wote.

Lakini Pro Piacenza walilazimika kuanza mechi hiyo wakiwa na wachezaji saba pekee wakiwempo vijana sita.

Huku wakikosa mkufunzi, nahodha wao mwenye umri wa miaka 18 Nicola Cirigliano alilazimika kuchukua wadhfa wa ukufunzi.

Walimaliza mechi hiyo wakiwa na mchezaji mwengijne wa ziada baada ya mmoja ya wachezaji hao kufanikiwa kupata nyaraka za utambulisho wake baada ya mechi kuanza.

Cuneo ilikuwa imefunga magoli 18 pekee katika mechi zake 24 kabla ya mechi ya siku ya Jumapili , lakini ikafanikiwa kuongeza idadi yao ya msimu huu katika dakika 90 zisizo za kawaida.

Huku ikikabiliwa na hali ngumu ya kifedha , Pro Piacenza inatarajiwa kukutana na shirikisho la soka nchini Itali ili kuamua hatma yao manmo mwezi Machi 11.

'Hali ya kushangaza'

Gabriele Gravina, rais wa shirikisho la soka nchini Itali alitaja matokeo ya siku ya Jumapili kama 'matusi kwa soka'.

''Katika kisa kama hiki Shirikisho la soka nchini Itali ilikuwa na jukumu la kutilia mkazo sheria zote'', alisema.

''Jukumu letu ni kulinda hamu ya mashabiki , afya, biashara na uaminifu wa ligi hii. Tulichoshuhudia itakuwa aibu ya mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...