Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Rais Vladimir Putin amesema Urusi itaanza kuunda makombora mapya

 


Marekani inahofia makombora mapyaya Urusi

Urusi imejiondoa katika mkataba wa kupinga uundaji wa makombora ya masafa marefu uliyofikiwa enzi ya vita baridi kufutia uamuzi sawa na huo uliyochukuliwa na Marekani.

Rais Vladimir Putin amesema taifa hilo litaanza kuunda makombora mapya.

Marekani ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikiilaumu Urusi kwa kukiuka mkataba huo ilitangaza kusitisha rasmi wajibu wake siku ya Ijumaa.

Mkataba huo uliyofikiwa kati ya Marekani na muungano wa Sovieti, USSR na kutiwa saini mwaka 1987 ulipiga marufuku mataifa yote dhidi ya matumizi ya makombora ya masafa mafupi na yale ya kadri.

"Washirika wetu wa Marekani wametangaza kusitisha wajibu wao katika mkataba huo nasi pia tunafuata mkondo wao,"alisema Bw. Putin siku ya Jumamosi.


Urusi ilirusha kombora katika mazoezi ya kijeshi

Katibu mkuu wa muungano wa kijeshi wa mataifa ya magharibi Nato, Jens Stoltenberg amaiambia kuwa: "Washirika wote [Ulaya] yameunga mkono hatua ya Marekani kwasababu Urusi imekiuka mkataba huo kwa miaka kadhaa."

Alisema makataa ya miezi sita iliyotolewa na Marekani kwa Urusi kufuata kutekeleza kikamilifu yanafaa kuzingatiwa.

Urusi imekuwa ikikanusha tuhuma za kukiuka mkataba wa vita baridi.

Rais wa Putin aidha amesema tuhuma za Nato dhidi ya taifa lake ni kisingizio cha Marekani kujiondoa katika mkataba huo.


Rais wa Urusi Vladimir Putin

Urusi inalaumiwa kwa nini?

Marekani imesema ina ushahidi kuwa kombora mpya iliyoundwa na Urusi ni moja ya mokombora yaliyopigwa marufuku katika mkataba wa INF.

Baadhi ya maafisa wa Marekani wanasema kuwa makombora ya aina ya 9M729 - yanayotambuilwa na Nato kama SSC-8 tayari yameanza kutumika.

Mwezi Disemba mwaka jana, Rais wa Marekani Donald Trump, aligusia kuwa taifa hilo huenda likajiondoa katika mkataba wa INF ikiwa Urusi haitabadili msimamo wake.


Kombora mpya aina 9M729 lililoundwa na Urusi inatia Marekani tumbo joto

Nini kitakachofuata?

Katika mkutano wa Jumamosi akiandamana na mawaziri wake ulinzi na wa mambo ya nje, rais Putin alisema wataanza kuunda silaha mpya ikiwa ni pamoja na makombora ya kulipua meli na mengine yaliyo na kasi ya mara tano zaidi ya mlio wasauti.

Bw. Putin hata hivyo amesema kuwa hatajihusisha katika mradi wa gharama ya juu ya uundaji silaha na kuongeza kuwa taifa lake litatumia silaha hizo endapo marekani itaanza kuzitumia.

''Mashindano ya uundaji wa silaha kama hizo ni tishio kubwa kwa mataifa ya bara Ulaya'' Jens Stoltenberg aliiambia BBC .

Ni yapi yaliyomo katika makubaliano ya kuunda makombora ya masafa ya kadri (INF)?


Kiongozi wa Sovieti Mikhail Gorbachev na rais wa zamani wa Marekani Ronald Reagan walitia saini mkataba wa INF mwaka 1987

Mkataba huo uliotiwa saini na Marekani na USSR mwaka in 1987, ulikuwa wa kudhibiti uundaji wa silaha za nuklia na makombora ya masafa ya mafupi na ya kadri, isipokuwa yale ya kurushwa baharini.


Marekani ilikuwa na hofu kuhusiana hatua ya Usoviyeti kuunda kombora la USS-20 na kujibu hatua hiyo kwa kuunda makombora ya kulipua meli barani Ulaya - hatua hiyo ililaaniwa sana.


Kufikia mwaka 1991, karibu makombora 2,700 ilikuwa imeharibiwa.


Mataifa yote mawili yaliruhusiwa kukagua mitambo ya mwingine.


Mwaka 2007, rais wa Urusi Vladimir Putin ilitangaza kuwa mkataba huo haulindi tena maslahi yake


Hatua hiyo ilikuja baada ya Marekani kujiondoa katika mkataba wa kudhibiti uundaji wa makombora ya masafa marefu uliyofikiwa mwaka 2002


Mara ya mwisho Marekani ilijiondoa katika mkataba wa silaha ilikuwa mwaka 2002, wakati rais George W Bush alipojiondoa kutoka mkataba wa kudhibiti uundaji wa makombora ya nuklia ambayo ilipiga marufuku uundaji wa silaha za kujibu mahambulio ya silaha hizo.
'


Hatua ya utawala wake wa kuweka kituo cha kujikinga dhidi ya makombora barani ulaya iliikasirisha Kremlin.

Hata hivyo kituo hicho kilifungwa na utawala wa Obama mwaka 2009 na mahala pake pakachukuliwa na mfumo wa ulinzi uliyoimarishwa mwaka 2016

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...