Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ole Gunnar Solskjaer kupewa kazi Manchester United akishinda Paris St-Germain

Tetesi za Soka Ulaya Jumamosi 02.02.2019: Solskjaer, Hudson-Odoi, Willian, Bakayoko




Manchester United hawajashindwa hata mechi moja chini ya uongozi wa Ole Gunnar Solskjaer

Manchester United watampatia kazi meneja wao wa sasa Ole Gunnar Solskjaer akifanikiwa kushinda Paris St-Germain katika mchuano wao wa ligi ya mabingwa. (Sun)


Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino ameelezea kutoridhishwa kwake na usimamizi wa klabu hiyo baada ya kushindwa kusajili wachezaji wapya kwa misimu miwili mfululizo. (Mirror)

Chelsea watakabiliana na Bayern Munich katika uhamisho wa mshambuliaji Callum Hudson-Odoi, baada ya klabu hiyo ya Bundesliga kushindwa kumsajili nyota huyo wa miaka. (Sun)


Hudson-Odoi, wa kati

Winga Willian, 30 wa Chelsea na Brazil, anataka kusaini mkataba wa miaka mitatu, lakini kuna tetesi amepewa mkataba wa mwaka mmoja. (Sport Witness)

Meneja wa West Ham Manuel Pellegrini alitaka kumsaini mchezaji wa zamani wa Cardiff, Gary Medel mwezi Januari lakini juhudi zake zilitibuka baada ya Besiktas kuitisha ada ya uhamisho. (Talksport)

Solskjaer: Pogba anafaa kuwa nahodha wa Man Utd


Meneja wa Inter Milan Luciano Spalletti anaamini Arsenal "walimlaghai" winga wa Croatia Ivan Perisic, 29, katika pendekezo la uhamisho wa Januari. (Rai Sport via Independent)


Tiemoue Bakayoko, kushoto

Kiungo wa kati wa Ufaransa Tiemoue Bakayoko, 24, ambaye yuko AC Milan kwa mkopo kutoka Chelsea, amesema angependelea kusalia katika klabu huyo ya Italia. (Corriere dello Sport via Four Four Two)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp anahofia mlinzi wake Joe Gomez,21 huenda akahitaji kufanyiwa upasuaji. (Liverpool Echo)

Newcastle wanajianda kutangaza kuondoka kwa kocha wao wa zamani Peter Beardsley ambaye alikua mkufunzi wa timu ya wachezaji wa chini ya miaka -23. (Mail

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...