Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mkenya aliyekamatwa Tanzania afungwa miaka 20

MTEULE THE BEST


Mahakama moja nchini Kenya imemfunga jela Feisal Mohammed, anayetuhumiwa kwa ulanguzi wa pembe za ndovu, kifungo cha miaka 20 gerezani.
Pia Feisal ametozwa faini ya dola 200,000.
Alipatikana na hatia ya kulangua vipande 413 za pembe za ndovu, vyenye thamani ya dola 400,000.
Hakimu Diana Mochache, wa mahakama ya mji wa Mombasa, alisema kuwa ushahidi uliashiria kuwa Feisal ndiye mmiliki wa vipande vya pembe vya ndovu, vilivyopatikana kwenye bohari moja jijini Mombasa yapata miaka miwili iliyopita.
Feisal
Image captionFeisal Mohammed (kulia) akishauriana na mawakili
Hakimu alitaja ulanguzi kama uhalifu mbaya, na kwamba walanguzi wa pembe sharti wafungwe ili kukomesha mauaji ya ndovu.
Ameongeza kuonya kuwa ulanguzi usiposimamishwa, huenda vizazi vivayo vikapewa hadithi tu kuhusu jinsi ndovu walivyokuwa, sawa na jinsi vizazi vya sasa vinapewa hadithi za wanyama waliokuwa wakiitwa dinosaur.
Wanne wengine waliokuwa wameshitakiwa pamoja naye Feisal waliachiliwa.
Pembe
Image captionPembe hizo zilitolewa wakati wa kutolewa kwa hukumu
Lakini mawakili wake Feisal wamesema amebaguliwa Feisal amefanyiwa ubaguzi na uonevu wa hali ya juu, na kamwe hana hatia na kuwa naamini kuna majaji katika mahakama ya juu ambao hawawezi kudanganyika, na wanaweza kutathmini vyema na ushahidi ili kupata ukweli uko wapi.
Kwa hivyo wao watakata rufaa kwenye mahakama kuu.
Feisal Mohammed amekuwa rumande tangu desemba mwaka 2014.
Wakati pembe za ndovu zilipopatikana, aliondoka Mombasa na kutorokea Tanzania, ndipo polisi wa kimataifa Interpol wakamchapisha kama mhalifu anayetafutwa sana na hivyo kukamatwa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...