Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KENYA:WAZIRI WA USALAMA AFARIKI DUNIA

MTEULE THE BEST
Waziri wa usalama nchini Kenya Jenerali Mstaafu Joseph Nkaissery amefariki dunia.
Waziri huyo amefariki dunia saa chache baada yake kulazwa katika hospitali ya kibinafsi ya Karen kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu.
Taarifa za kifo chake zimetangazwa na mkuu wa utumishi wa umma Bw Joseph Kinyua mwendo wa saa kumi na moja alfajiri.
Upinzani waonywa kuhusu kituo cha kuhesabu kura Kenya
Matiang'i ateuliwa kaimu waziri wa usalama Kenya
"Ni kwa huzuni kubwa na mshangao kwamba tunatangaza kifo cha ghafla cha Waziri wa Usalama wa Ndani Jenerali Mstaafu Joseph Nkaissery," taarifa ya Bw Kinyua imesema.
"Taifa litaendelea kupashwa habari zaidi punde maelezo yatakapopatikana."
Jenerali Joseph Kasaine ole Nkaissery, 67, amefariki siku chache baada ya mwanasiasa mkongwe G.G. Kariuki aliyekuwa seneta wa jimbo la Laikipia kufariki dunia.
Mwanasiasa wa muda mrefu Kenya GG Kariuki afariki dunia
Waziri huyo alizaliwa mwaka 1949 na alihudumu katika jeshi kwa miaka 29 kabla ya kuingia katika siasa wakati wa uchaguzi wa mwaka 2002 ambapo alimshinda David Sakori wa chama cha KANU wakati wa kustaafu kwa Rais Daniel arap Moi katika eneo bunge la Kajiado ya Kati.
Mwaka 2007, alichaguliwa tena kuwa mbunge wa eneo hilo kwa chama cha Orange Democratic Movement (ODM) chake Raila Odinga na wakati wa kuundwa kwa Serikali ya Muungano wa Kitaifa kati ya Bw Odinga na Rais Mwai Kibaki, alipewa wadhifa wa Waziri Msaidizi wa Ulinzi.
Ni wakati wake ambapo Kenya iliingia nchini Somalia, baada ya makubaliano na serikali ya taifa ya Somalia, kupambana na wanamgambo wa al-Shabab mwaka 2011 chini ya Operesheni Linda Nchi.
Alichaguliwa tena kuwa mbunge uchaguzi mkuu wa mwaka 2013 kupitia ODM lakini Desemba mwaka 2014, baada ya kufutwa kazi kwa aliyekuwa waziri wakati huo Joseph Lenku kutokana na kuongezeka kwa mashambulio ya kigaidi ya al-Shabab, aliteuliwa kuwa Waziri wa Masuala ya Ndani, Usalama na Uratibu wa Serikali ya Taifa na Rais Uhuru Kenyatta.
Nkaissery azungumzia kukamatwa kwa mwanahabari
Hatua hiyo iliughadhabisha upinzani ambao ulitazama hatua hiyo kama mpango wa kuudhoofisha upinzani.
Jenerali Nkaissery alijiuzulu wadhifa wake wa ubunge na akaapishwa kuwa waziri 24 Desemba, 2014.
Akiwa waziri, Kenya ilionekana kufanikiwa kuwadhibiti al-Shabaab na mashambulio ndani ya nchi yakapungua.
Alikuwa miongoni mwa mawaziri walioitetea sana serikali na uchaguzi ulipokaribia, alikuwa akipuuzilia mbali vitisho vya upinzani na kuonya kwamba hatawavumilia watu wanaotaka kuvuruga amani nchini Kenya.
Amekuwa waziri wa pili wa usalama kufariki duniakatika kipindi cha miaka mitano. Juni mwaka 2012, waziri usalama wa wakakti huo Prof George Saitoti, ambaye alikuwa wakati mmoja amehudumu kama makamu wa rais chini ya Rais Moi, alifariki dunia kwenye ajali ya ndege eneo la Ngong viungani mwa mji wa Nairobi.
Alifariki dunia pamoja na waziri wake msaidizi Joshua Orwa Ojode.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...