Haki miliki ya pichaAFP/GETTYImage captionMagari yaliyokuwa yamewabeba viongozi wa upinzani Nairobi yalirushiwa vitoa machozi
Watu wawili wameuawa kwa kupigwa risasi wakati wa maandamano ya muungano wa upinzani katika mji wa Bondo, magharibi mwa Kenya.
Taarisa zinasema wawili hao wamefariki baada ya polisi kuwafyatulia risasi waandamanaji ambao inadaiwa walijaribu kuvamia kituo cha polisi cha Bondo katika kaunti ya Siaya.
Mkuu wa polisi wa eneo hilo John Kiarie ameambia BBC kwamba hawezi kukanusha au kuthibitisha vifo hivyo kwani bado hajapokea maelezo ya kina kuhusu tukio hilo.
Muungano wa upinzani National Super Alliance wake waziri mkuu wa zamani Raila Odinga umekuwa ukifanya maandamano kushinikiza mageuzi kwenye Tume ya taifa ya Uchaguzi IEBC kabla ya uchaguzi mpya kufanyika.
Alhamisi, serikali ilipiga marufuku maandamano katika maeneo ya kati ya miji ya Nairobi, Mombasa na Kisumu baada ya visa vya uporaji kushuhudiwa wakati wa maandamano ya awali.
Jijini Nairobi, polisi leo wamekuwa wakishika doria katika barabara kuu kuwazuia waandamanaji kuingia katikati mwa jiji.
Katika baadhi ya maeneo, polisi walitumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya au kuwadhibiti waandamanaji.
Katika jiji la Nairobi, kumukuwepo na taarifa za wanahabari kushambuliwa na polisi hao wa kupambana na fujo.
Mahakama ya Juu nchini humo ilifuta matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika tarehe 8 Agosti ikisema ulijaa kasoro nyingi kiasi kwamba ilikuwa vigumu kubaini nani alishinda kwa njia halali.
Tume ya uchaguzi ilitangaza uchaguzi mpya ungefanyika tarehe 17 Oktoba lakini baadaye ikabadilisha tarehe hiyo hadi 26 Oktoba.
Bw Odinga ambaye alitarajiwa kukabiliana na Rais Uhuru Kenyatta alijiondoa Jumanne akisema mageuzi ambayo yanahitajika bado hayajatekelezwa.
Haki miliki ya pichaREUTERS
Mahakama Kuu baadaye iliagiza kuongezwa kwa jina la Ekuru Aukot miongoni mwa wawaniaji wa urais hatua iliyoifanya IEBC kutangaza baadaye kwamba wagombea wote wanane watashiriki.
Hali ya utata kuhusu kuandaliwa kwa uchaguzi huo imezidi kwambi Nasa wameendelea kusisitiza kwamba hawatashiriki.
Bw Odinga kwa sasa yuko ziarani Uingereza na amesisitiza kwamba hatatia saini Fomu 24A ambayo tume ya uchaguzi ilisema anafaa kujaza ndipo ajiondoe rasmi kutoka kwa uchaguzi huo.
Image captionBw Odinga akihutubu katika Taasisi ya Masuala ya Kimataifa, Jumba la Catham jijini London
Pendekezo la IEBC kuhusu fomu hiyo limekosolewa na baadhi ya mawakili wanaosema fomu hiyo inaweza tu kutumiwa iwapo kumefanyika uteuzi wa wagombea jambo ambalo haliwezekani wakati huu kwani uchaguzi ni wa marudio.
Jijini Mombasa waandamanaji walifaulu kuingia katikati mwa jiji kabla ya polisi kuwarushia vitoa machozi na kuwatawanya.
Wabunge wa eneo hilo wanasisitiza kuwa marufuku ya serikali kuzuia maandamano katikati ya miji mikubwa inakiuka katiba. Kutoka Mombasa, Mwandishi wa BBC aliyepo Mombasa Ferdinand Omondi anasema waandamanaji walifika jijini Mombasa alfajiri na kukusanyika katika bustani moja maarufu, wakiwa na baadhi ya wabunge ya mji huo.
Waliandamana kwa amani huku wakiimba wakielekea katika afisi za tume ya uchaguzi.
Walipita katikati ya mji kwa muda huku polisi wakionekana kusita kuwatawanya kwani waandamani walionekana kutotaka kuzua rabsha zozote. Lakini ghafla tu, askari wakaanza kuwarushia vitoa machozi na kuwatawayanya. Baadaye wakaanzisha msako wa kuwatafuta waandamanaji kwa kuavamia majumba ya watu.
Mbunge wa Upinzani Badi Twalib amelaani hatua hiyo akisema wao hawakufanya lolote lililostahili polisi kutumia nguvu kuwatawanya.
Mbunge mwenzake Abdulswamad Shariff Nassir naye ameambia BBC kuwa amri la waziri wa usalama Fred Matiang'i ya ni kinyume na katiba inayoruhusu wananchi kulalamika kwa njia ya maandamano.
Wabunge wa Mombasa sasa wameitisha mkutano wa hadhara siku ya jumapili katika bustani ya ufukwe wa Mama Ngina kisiwani Mombasa , ili kuwapa wafuasi wao muelekeo wa hatua watakayochukua.
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.
Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...
Maoni