Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAHAKAMA NA BUNGE KENYA ZATOA MAAMUZI MAGUMU

MTEULE THE BEST

Mahakama, bunge Kenya zatoa maamuzi magumu uchaguzi wa Oktoba 26

Bunge la Kenya limepitisha marekebisho tata kuhusu sheria ya uchaguzi, likisema ikiwa mgombea mmoja atajitoa katika uchaguzi wa marudio mwingine atashinda moja kwa moja. Wapinzani wamekosoa na kususia kikao cha bunge.

Kenia Nairobi Demonstration Odinga AnhƤnger (Getty Images/AFP/T. Karumba)
Kiongozi wa upinzani, Raila Odinga, alitangaza kujitoa katika uchaguzi wa marudio uliopangwa kufanyika Oktoba 26, akielezea wasiwasi kuhusu uadilifu na uwazi katika mchakato mzima. Sheria hiyo sasa inapaswa kutiwa saini na rais Uhuru Kenyatta.
Hatua hiyo imekuja huku mahakama ya juu ikitoa hukumu kuwa mgombea aliepata chini ya asilimia moja ya kura katika uchaguzi wa Agosti 8 ambayo mahakama ya juu iliubatilisha, Ekuru Aukot ana haki ya kujumlishwa kwenye kura mpya.
Jaji John Mativo alisema siku ya Jumatano kuwa hakuona sababu yoyote kwa Aukot kuzuwia kushiriki uchaguzi wa marudio. Aukot alipata karibu kura 27,000 kati ya zaidi ya kura milioni 15 zilizopigwa katika uchaguzi uliobatilishwa.
Mahakama iliukataa uchaguzi wa Agosti 8, ambamo Rais Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi baada ya Odinga kupinga matokeo hayo akisema wadukuzi waliingilia mfumo wa computer wa tume ya uchaguzi na kubadilisha matokeo kwa faida ya Kenyatta.
Kenia | Proteste gegen den Wahlausgang vor dem Obersten Gerichtshof in Nairobi (picture-alliance/AP Photo/B. Curtis)
Wafuasi wa Odinga wakiandamana.
Odinga alitangaza kujiondoa katika uchaguzi mpya siku ya Jumanne, akisema tume ya uchaguzi laazima ibadilishwe. Na wakati maafisa wa uchaguzi wakitafakari hatua inayofuata baada ya Odinga kujitoa, wafuasi wake wameingia mitaani Jumatano kuandamana kushinikiza mageuzi ndani ya tume hiyo.
Mgawanyiko kuhusu uamuzi wa Odinga
Maoni yamegawanyika kuhusu nini uamuzi wa mwanasiasa huyo mkongwe unamaanisha, kwa uchaguzi ambao tayari umezusha taharuki, ambapo rais Kenyatta anasisitiza kura ya Oktoba 26 laazima ifanyike.
Maelfu ya wafuasi wa Odinga waliingia katika mitaa ya ngome zake magharibi mwa Kenya - Kisumu na Homa Bay, wakiwa wamebeba viboko na mabango yenye ujumbe usemao: "Hakuna mageuzi, hakuna uchaguzi".
Mahakama ya juu nchini Kenya ilibatilisha ushindi wa Kenyatta na kuamuru uchaguzi mpya uitishwe ndani ya siku 60. Lakini mchakato huo ulikwaa kisiki haraka, ambapo Odinga alidai mageuzi makubwa ambayo tume ya IEBC ilisema hayawezekani kufanyika katika muda uliohurusiwa kikatiba.
Ni kushindwa huu kufanya mabadiliko yanayohitajika ambako Odinga alisema kumemsukuma kujotoa katika uchaguzi mpya wa Oktoba 26. "Ishara zote zinaonyesha kwamba uchaguzi uliopangwa kufanyika Oktoba 26 utakuwa mbaya kuliko wa mwanzo," alisema.
Odinga aliweka matumaini yake kwa  hukumu ya mahakama ya juu mwaka 2013 iliyotaka kufafanua sheria za sasa kwa kusema kwamba iwapo mgombea anafariki au kujitoa kwenye uchaguzi, IEBC laazima ianze mchakato wa uteuzi kuanzia sifuri. Matarajio yake yalikuwa kwamba hilo lingetoa muda zaidi wa kufanyika mageuzi.
Kenias Staatschef Kenyatta gewinnt PrƤsidentschaftswahl (Picture-Alliance/dpa/AP/S. A. Azim)
Rais Uhuru Kenyatta
Hali ya mashaka yatawala
Uamuzi wa Odinga uliongeza hali mashaka iliowakumba raia wa taifa hilo kuhusiana na uwezekano wa kutumbukia tena katika machafuko na kukwama kwa uchumi katika taifa hilo tajiri zaidi kitika kanda ya Afrika Mashariki, na mshirika wa muda mrefu wa mataifa ya Magharibi.
Kwa wakati huu hakuna uwezekano wa kurudiwa kwa mapigano ya kikabila yaliosababisha vifo vya watu 1,200 yaliofuatia uchaguzi wa rais uliobishaniwa mwaka 2007. Lakini watu wasiopungua 37 waliuawa katika maandamano yalifuatia kura ya mwaka huu, karibu wote wakiuawa na polisi, kulingana na shirika la haki za binadamu la Kenya.
Uamuzi wa Mahakama ya Juu wa Septemba 1 uliobatilisha ushindi wa kura milioni 1.4 wa Kenyatta, ulianisha pia kwamba uchaguzi unapaswa kufanyika ndani ya siku 60. Ikiwa hilo halitafikiwa, katiba inaagiza spika wa bunge, ambaye ni manachama wa chama cha Kenyatta, kuchukuwa madaraka.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...