Ruka hadi kwenye maudhui makuu

CHADEMA YAIANDIKIA BARUA MAREKANI, UJERUMANI

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeziandikia barua Marekani na Ujerumani kuzitaka kuziangalia tuhuma zilizoelekezwa dhidi yao za kukihusisha na chama hicho katika kile kinachodaiwa kuwa ni mipango ya kuhatarisha usalama wa Tanzania.


Barua mbili za Chadema ambazo zimeandikwa Machi mosi mwaka huu na kusainiwa na Mkuu wa Kitengo cha Habari cha chama hicho, Tumaini Makene, zimetaka balozi za nchi hizo nchini kujibu tuhuma hizo ambazo zilielekezwa na Cyprian Musiba aliyejitambulisha kama Mkurugenzi wa Kampuni ya CZI.


Gazeti hili ambalo limefanikiwa kuona barua hizo jana, Chadema kimesema kimeona umuhimu wa kuchukua hatua hiyo ili kupata mwitikio wa nchi hizo juu ya tuhuma hizo nzito ambazo zinatakiwa kuangaliwa zaidi.


Katika barua yenye kumbukumbu No. C/HQ/ADM/KS/24/02  ambayo imeelekezwa kwa John Espinos ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Siasa na Uchumi, Ubalozi wa Marekani, Chadema imeeleza kwamba Februari 25, mwaka huu mtu aliyejulikana kwa jina la Cyprian Musiba, aliituhumu Marekani kwa kufanya mipango na mikakati mbalimbali ya kuhatarisha usalama wa Taifa la Tanzania.


Barua hiyo ilielezea kwa urefu kwamba Musiba kwa kupitia majukwaa mbalimbali ya kubadilishana taarifa na mawasiliano vikiwamo vipande vya video vilivyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii alisema Marekani inadaiwa kupanga watu au kuendesha mikakati inayohatarisha usalama wa Tanzania.


ā€œMusiba alikwenda mbali zaidi kwa  kutuhumu kuwa nchi yako imekuwa ikishirikiana na Chadema kupanga uhatarishaji wa usalama wa nchi. ā€œAlituhumu FBI (Federal Bureau of Investgation) kuwa inajihusisha na baadhi ya Watanzania katika mipango hiyo.ā€


Pia barua hiyo ilisema kuwa Musiba alitaka dunia na Afrika yote kutambua uwapo wa hiyo mipango hatari dhidi ya Tanzania ambayo Marekani inahusishwa kwa namna moja au nyingine kufanya mipango hiyo.


ā€œKutokana na mapenzi na uwajibikaji wetu kwa nchi yetu ya Tanzania na kama taasisi  ikiwa ni sehemu ya wadau kwa maisha yajayo ya nchi yetu pendwa, kwa kuweka mbele masilahi ya nchi na wakazi wake ndani na nje ya nchi, katikati ya kila kitu na kwa kuguswa na tuhuma kama mdau, tunahisi msukumo na kuona umuhimu wa kukuandikia, hivyo tunaweza kupata mwitikio wako kwa tuhuma hizi nzito na tunafikiri kuziangalia zaidi.


ā€œKatika barua hii tumeambatanisha CD zenye vipande vya video vinavyomwonyesha Cyprian Musiba akiviambia vyombo vya habari siku tajwa hapo juu.ā€


Kwa kupitia hoja kama hizo barua ya pili yenye kumbukumbu No C/HQ/ADM/KS/24/01 ambayo ilielekezwa kwenda kwa Joerg Hererra ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Siasa na Uchumi cha Ubalozi wa Ujerumani, Chadema ilisema Musiba alikaririwa akikituhumu chama tawala cha nchi hiyo cha Christian Democratic Union (CDU) kushiriki mipango ya kuhatarisha usalama wa Tanzania.


Jumapili iliyopita Musiba alizungumza na baadhi ya waandishi wa habari na kutoa tuhuma nzito kwa nchi hizo mbili huku akitoa orodha ya watu ambao aliwaita ni hatari kwa usalama wa Taifa.


Watu hao ni Mange Kimambi ambaye alimtuhumu kuwa anatumiwa na FBI kuchochea machafuko nchini.


Wengine ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Maria Sarungi, Zitto Kabwe, Tundu Lissu, John Heche, John Marwa, Evarist Chahari, Julius Mtatiro pamoja na kikundi cha Janja weed alichodai kinaratibiwa na wafuasi wa CUF.



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...