Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Takriban Waislamu 150 wenye itikadi kali wanashikiliwa Ujerumani

Magereza ya Ujerumani yanajitahidi kukabiliana na wafungwa wenye itikadi kali





Idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka baada kufunguliwa kwa misururu ya uchunguzi unaohusiana na ugaidi katika miezi ya hivi karibuni.


Takriban Waislamu 150 wenye itikadi kali wanashikiliwa katika magereza ya Ujerumani, kwa mujibu wa takwimu za afisi ya Idara ya Upelelezi ya Serikali kuu ya Ujerumani zilizoschapishwa kwenye gazeti la kila siku nchini Ujerumani la Die Welt.

Gazeti hilo lililonukuu afisi ya Idara ya Upelelezi ya Serikali Kuu, linasema kuwa wanaume hao ama wanatumikia kifungo au wanatuhumiwa kwa makosa yanayohusiana na ugaidi.

wafungwa wanaishikiliwa walikuwa wapiganaji wa IS

Wapiganaji wa Dola la Kiislamu-IS

Gazeti hilo linaendelea kusema kuwa, watu kadhaa wanaohusishwa na ugaidi wanashikiliwa katika magereza hayo ambao huenda ni wafuasi wanawaunga mkono itakadi kali.

Waziri wa sheria wa jimbo la Hesse nchini Ujerumani Eve Kuƶhene-Hƶ ameliambia gazeti hilo kuwa, katika miaka michache ijayo, Ujerumani italazimika kutarajia wafungwa wengi zaidi  wenye itikadi kali.

Ameendelea kusema kuwa, ``kuna uchunguzi unaoendelea dhidi ya mamia ya washukiwa. Uchunguzi huo unafanyika kote nchini Ujerumani wanaochunguzwa wengi wao wakiwa wapiganaji wa Kiislamu wanaorejea Ujerumani kutoka Mashariki ya Kati baada ya kuwa katika mapambano ya kulisaidia  kundi la Dola la Kiislamu.``

Kunhe-Hƶrmann ameonya kuwa idadi ya Waislamu wenye itikadi kali walioko kweye magerez ya ya Ujerumani ni ``changamoto kubwa ya kuvunja nguvu ugaidi pamoja na kuuzuia.``

Amesema  iwapo magereza hayatatumika kuwasaidia watu wenye itikadi kali kutangamana na jamii pana ``kuna hatari ya kuachia waislamu wenye itikadi kali katika jamii.``

Visa 1200 vya kigaidi vinachunguzwa

Wafungwa 150 wanazuliwa Ujerumani kwa itikadi kali

Mwezi Desemba, maafisa wa Ujerumani walikiri juu ya kuanzishwa uchunguzi mara tano zaidi dhidi ya ugaidi mwaka 2017 ikilinganishwa na miaka ya awali. Takriban visa 1200 vinavyochunguzwa vinahusu vitendo vya kigaidi na zaidi ya asilimia 80 ya visa hivyo vinahusiana na Waislamu wenye itikadi kali.

Vinajumuisha wahubiri wenye misimamo mikali, wauaji walioshindwa katika njama zao na wale wanaorejea kutoka Syria na Iraq ambako mapigano yanaendelea.

Gazeti la Die Welt, limekinukuu, Chama cha Maafisa wa Magereza wa Ujerumani kikisema kuwa idadi ya wafungwa wenye itikadi kali wanaongeza hatari kwa usalama kwa wafanyikazi, kabla ya kutoa wito wa kutolewa mafunzo zaidi.

Katika taifa jirani la Ufaransa, walinzi wa magereza walifaya maandamano mwezi uliopita , wakilalamikia ghasia katika magereza yalioyokuwa na idadi ya wafungwa kupita kiasi.

Maafisa wa magereza walisusia kazi baada ya mpiganaji wa Kiislamu kutoka Ujerumani alipomkata mlinzi wa gereza kwa kutumia mkasi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...