Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Wafadhili waichangishia fedha Congo

Wafadhili wanakutana mjini Geneva Uswisi Ijumaa katika harakati za kuchangisha dola bilioni 1.7 kwa ajili ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo ambayo inakabiliwa na mzozo.

Uganda FlĆ¼chtlinge aus DR Kongo UNHCR Camp (Reuters/J. Akena)

Wataalam wanasema huenda mzozo huo ukapindukia na kuwa janga kubwa. Mkutano huo unakuja wakati kukiwa na hofu kwamba  mizozo ya kikabila, ufisadi na hali mbaya ya usalama ni mambo yanayozusha hofu ya umwagikaji damu.

Kwa wale walioachwa bila makao, kitisho ni cha kweli. Raia mmoja wa Congo alielezea mzozo wa kikabila katika mkoa wa Ituri kwa kusema, "ni kama wakati tulipokuwa katika vita vya wenyewe kwa wenyewe." Kulingana na makadirio ya shirika la msalaba mwekundu karibu Wacongo 70,000 wamekimbilia Uganda kwa kuuvuka mto Albert tangu Januari. Ituri ni mkoa mmoja tu kati ya mingi ambayo makundi yaliyojihami na wahalifu wanawasumbua raia.

Ukosefu wa usalama umezidisha idadi ya wakimbizi wa ndani ya nchi

Zaidi ya hayo kuna mzozo wa kisiasa unaozunguka suala la urais ambapo watu wengi wanamtaka rais Joseph Kabila ambaye muhula wake ulikwisha Desemba mwaka 2016 ajiuzulu. Lakini makubaliano yanayonuiwa kutoa nafasi ya kipindi cha mpito cha serikali mpya bado hayajatekelezwa na maandamano nchini humo yanadhibitiwa.

Deutschland Treffen Steinmeier mit Filippo Grandi in Berlin (picture-alliance/dpa/R. Jensen)

Kamishna wa UNHCR Filippo Grandi

Kulingana na Afisi ya mratibu wa misaada ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa OCHA, ukosefu wa usalama nchini Congo ambao umekuwa ukiendelea umepelekea watu milioni 4.3 kuachwa bila makao nchini mwao. Kamishna wa Shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu wakimbizi Filippo Grandi wakati wa ziara nchini Congo wiki iliyopita alisema,

"Kwa bahati mbaya shughuli za wakimbizi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo zinaendelea kukumbwa na uhaba wa fedha na kwa bahati mbaya ndivyo hali hii ilivyo katika sehemu zengine Afrika. Na nataka kuikumbusha jamii ya kimataifa kwamba Afrika bado iko mbali sana kuzifikia nchi tajiri duniani," alisema Grandi. "Idadi kubwa ya wakimbizi hawa hawawezi kusafiri kuelekea Ulaya kuikumbusha dunia kuhusiana na uwepo wao. Wanaishi hapa, wanapitia magumu hapa na wana mahitaji pia," aliongeza Mkuu huyo wa UNHCR.

Waziri Mkuu wa zamani Badibanga ataka maendeleo yazingatiwe baada ya mkutano huu 

Grandi ameitaka jamii ya kimataifa kuongeza viwango vya fedha zilivyojitolea kutoa. Kwa mantiki hii ndiyo mkutano wa uchangishaji fedha wa leo huko Geneva ukaratibiwa ambapo alioupanga ni mwanasiasa na Waziri Mkuu wa zamani wa Congo Samy Badibanga. OCHA, Uholanzi pamoja na Umoja wa Ulaya wamealikwa ili kufanikisha 


uchangishaji wa dola bilioni 1.7.

 Kinshasa Samy Badibanga Pressekonferenz (Reuters/K.Katombe)

Waziri Mkuu wa zamani wa DRC Samy Badibanga

Katika mahojiano ya hivi majuzi na DW Badibanga alisema kustawi kwa Congo kunahitaji mshikamano na jamii ya kimataifa.

"Baada ya mkutano huu wa uchangishaji fedha, maendeleo ya nchi lazima yaangaziwe kwasababu ni rahisi sana kwa nchi maskini na ambayo iko nyuma kimaendeleo kutumbukia kwenye machafuko tena," alisema Badibanga.

Lakini serikali ya Congo inapinga mkutano huo wa uchangishaji fedha ikisema Umoja wa Mataifa ulichapisha idadi ya isiyo ya kweli ya wakimbizi waliokimbia kutoka Congo. Msemaji wa serikali ya Congo Lambert Mende alisema kwamba iwapo hakutokuwa na mawasiliano ya kusawazisha idadi ya wakimbizi basi serikali haitohudhuria mkutano huo.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...