Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mahakama Uganda yasikiliza kesi dhidi ya ukomo wa umri wa kuwania urais


Rais Yoweri Museveni ameongoza Uganda kwa ziadi ya miaka 30

Mahakama ya Kikatiba inasikiliza kesi iliyoletwa na upande wa upinzani kufuta marekebisho ya katiba ambayo yanatoa ukomo wa miaka ya kuwa rais.


Wabunge waliipigia kura wa kishindo mwaka uliopita kufuta ukomo wa miaka 75.


Ilimaanisha kuwa Rais Yoweri Museveni mwenye miaka 73, ambaye amekuwa madarakani kwa zaidi ya miaka 30, anaweza kuwania tena mwaka 2021.


Mawakili wa upinzani walitoa hoja kuwa marekebisho hayo yaliingizwa "kinyemela" hadi kuwa sheria, na bunge halikufuata kanuni zilizopaswa katika kuweka marekebisho hayo.


Ulinzi umeimarishwa katika eneo la mahakama liliopo katika jiji la Mbale, mashariki mwa Uganda, na baadhi ya barabara zimefungwa kuepusha machafuko.


Hii ni mara ya kwanza ombi la haki la kikatiba linasikilizwa , anaripoti mwandishi wa BBC Patience Atuhaire kutoka jiji kuu la Kampala.


Miongoni mwa waomba haki ni wabunge wa upande wa upinzani,chama cha wanasheria Uganda na asasi za kiraia.


Wabunge wapigana makonde Uganda

Wanasema marekebisho hayo hayana msingi kwa sababu yalipitishwa wakati vurugu ilitokea kwenye vipindi ambapo walinzi waliovaa nguo za kawaida waliwatoa wabunge bungeni.


Pia wanatoa hoja kuwa Bw Museveni anataka kuwa rais wa maisha na kuwa mabadiliko hayo yanakiuka misingi ya kidemokrasia, utwala unamlikiwa na watu.


Washirka wa Museveni wanasema marekebisho hayo yanatoa ubaguzi wa kiumri na yalipitishwa baada ya kupata ushauri wa Umma.


Chama tawala cha National Resistance Movement kiliongoza mabadiliko hayo kupitia bunge na Bw Museveni akatia saini na kuifanya sheria.


Bw Museveni alishinda awamu ya tano mwaka 2016 katika uchaguzi uliodaiwa kuwa na dosari.


Ukomo wa awamu mbili ulifutwa mwaka 2005 ili kumwezesha awanie ofisi tena


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...