Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Azimio la Zanzibar 2018: Viongozi wa upinzani Tanzania waafikiana 'kudai demokrasia' kwa pamoja




iovngozi hao wameeleza mkutano huo wa Zanzibar kuwa wa kihistoria

Vyama sita vya upinzani nchini Tanzania vimekutana na kutoa azimio la pamoja katika kile kinachotazamwa kama juhudi za mapema za kutaka kuungana nchini humo.

Viongozi hao waliahidi kuungana na kuutangaza mwaka 2019 kuwa ni 'Mwaka wa Kudai Demokrasia', na kadhalika wakaahidi kufanya mikutano ya siasa bila kujali katazo la mikutano ya hadhara.

"Ni mwaka ambao tutapambana kuzidai haki zetu zote tunazonyimwa kinyume na sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania," taarifa ya pamoja ya viongozi wa vyama hivyo inasema.

"Kama vyama vya siasa vyenye uhalali na vyenye utaratibu uliowekwa rasmi kisheria na kikatiba, tutatangaza rasmi namna na utaratibu wa kufanya mikutano yetu ya hadhara katika kila kona ya nchi yetu, hatutaruhusu katazo haramu na lisilo na mashiko ya kisheria litumike kutuzuia kutekeleza wajibu wetu."


Waliotia saini azimio hilo ni Maalim Seif Sharif Hamad (Katibu Mkuu, CUF), James Francis Mbatia(Mwenyekiti Taifa, NCCR Mageuzi), Oscar Emanuel Makaidi (Mwenyekiti Taifa, NLD), Salum Mwalimu (Naibu Katibu Mkuu - Zanzibar, CHADEMA), Hashim Rungwe Spunda (Mwenyekiti Taifa, CHAUMMA) na Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo).

"Tunao wajibu wa kutoa dira kwa wananchi. Tunasema sasa basi, imetosha," walisema.

Maalim Seif: Yanayotokea chini ya Magufuli, hatujawahi kuyaona Tanzania

Viongozi hao walisema madhumuni ya kuandaa kikao hicho cha siku tatu yalikuwa kuandaa mkakati mpya na wa pamoja wa kupambana na hali ya demokrasia kudorora sana Tanzania.

Kwa sasa Kiongozi wa Kambi Upinzani Bungeni Freeman Mbowe ni mahabusu naye Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni Tundu A. Lissu akiendeleza kuuguza majeraha ya kupigwa risasi mwaka uliopita.

Miongoni mwa mambo wanayosema ni dalili za utawala wa kiimla nchini Tanzania ni kufutwa kwa Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wa mwaka 2015 ambao upinzani walidai kushinda; kuzuiwa kwa mikutano ya hadhara na maandamano ya vyama vya siasa na kutekwa na kukamatwa kwa wananchi, wakiwemo viongozi wa kisiasa, waandishi wa habari na wafanyabiashara.

Kadhalika, wametaja shambulio dhidi ya Bw Lissu na uwepo wa sheria mbaya za Habari na Takwimu, pamoja na kanuni za uendeshwaji wa Asasi za Kiraia (AZAKI), Kanuni za Sheria ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na Mswada wa mabadiliko ya Sheria ya Vyama vya Siasa.

'Vita dhidi ya upinzani'

Viongozi ha wanaituhumu serikali ya Rais Dkt John Magufuli kwa kuendeleza vita dhidi ya vyama vya upinzani "pamoja na wote wanaonekana wana mawazo mbadala juu ya namna nchi yetu inavyoendeshwa" hata ndani ya chama tawala cha CCM.

"Imekuwa ni kawaida sasa kwa Mkuu wa Nchi yetu, pamoja na wafuasi wake, kuwaita viongozi na wanasiasa wa vyama vya upinzani, pamoja na wakosoaji wa serikali kuwa ni 'Mawakala wa Nchi za Nje' na si Wazalendo," wamesema.


Viongozi hao wametofautiana na msimamo wa serikali kwamba uchumi wa taifa hilo la Afrika Mashariki unaimarika, na kusema hali ni kinyume."Baada mwelekeo mzuri kiasi wa hali ya uchumi wa nchi yetu kwa miaka kumi, hali ya uchumi wetu imeharibika katika kipindi cha miaka hii mitatu tu ya awamu ya tano," wanasema.

Lowassa: Kuna dalili za ā€˜udiktetaā€™ serikali ya Magufuli Tanzania

Viongozi hao wamewaeleza Freeman Mbowe na Esther Matiko, ambao mpaka sasa wako mahabusu, kuwa wafungwa wa kisiasa na kusema msimamo wao utasalia hivyo hadi pale watakapoachiwa.


"Tutapambana kuhakikisha kuwa wao na wafungwa wenzao wote wa kisiasa, nchi nzima, wanapewa nafasi ya kupata haki katika mfumo ulio huru, mbele ya mahakama na mbele ya macho ya umma," walisema viongozi hao

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...