Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Diamond Platnumz na ATCL: Mwanamuziki azozana na Air Tanzania kuhusu kuachwa na ndege uwanjani Mwanza


Mwanamuziki nyota kutoka Tanzania Diamond Platnumz ametofautiana na Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) kuhusu kilichotokea hadi akaachwa na ndege uwanjani mwanza.

Mwanamuziki huyo anasema tamko lililotolewa na shirika hilo kwamba alichelewa kufika uwanjani si za kweli.

ATCL kupitia taarifa wamesema Diamond , ambaye wamemrejelea kama Isaack Nasibu, alikuwa miongoni mwa abiria waliopaswa kusafiri na ndege ya shirika hilo Jumapili 16 Desemba, 2018 hakuachwa kama inavyodaiwa bali alichelewa kufika uwanjani kwa muda unaotakikana.

Anadaiwa kufika dirishani robo saa baada ya dirisha kufungwa.

Jina rasmi la mwanamuziki huyo ni Nasibu Abdul Juma Issaack.

"Kampuni inapenda kutoa ufafanuzi kuwa abiria huyo alifika uwanjani kwa kuchelewa na hivyo kuzuiliwa na mamlaka zinazosimamia uwanja kwa mujibu na taratibu," ATCL wamesema.


Aidha, shirika hilo la serikali limepuuzilia mbali madai ya msanii huyo kwamba tiketi yake iliuzwa kwa abiria wengine.

"Kampuni inapenda kutoa ufafanuzi kwamba, tuhuma hizo si za kweli kwani tiketi za kampuni yetu zinamruhusu mteja wetu kuitumia tiketi yake ambayo haijatumika kwa siku nyingine ambapo atakuwa tayari kusafiri nasi.

"Hata hivyo mteja wetu aliyelalamika ameiomba kampuni kutumia tiketi yake siku ya leo.

"Kampuni ya ndege Tanzania (ATCL) imesikitishwa na tuhuma na malalamiko yaliyotolewa na ndugu Issaack Nasibu na wenzake kwa kupitia video waliyojirekodi na kuirusha kwenye mitandao ya kijamii wakati kampuni inazo taratibu za namna ya kuwasilisha malalamiko pindi mteja asiporidhika na huduma zetu."

ATCL wametoa wito kwa abiria "kuzingatia muda unaoonyeshwa katika tiketi zao ili kuepuka usumbufu usiokuwa wa lazima."

Mkuu wa mawasiliano wa shirika hilo Josephat Kagirwa amesema shirika lililazimika kutoa ufafanuzi kwa umma baada ya kuona malalamiko ya Diamond yakisambaa katika mitandao ya kijamii.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diamond amesema hakuchelewa kamwe na badala yake akadai kuna mchezo ulifanyika ikiwa ni pamoja na tiketi za abiria kuuzwa kwa abiria wengine, ambapo anasema miongoni mwa waliokuwa wanauziwa ni baadhi ya wafanyakazi wa kampuni yake ya Wasafi Media.

Licha ya kwamba ujumbe ni wa kulalamika, kwenye picha yake ameweka picha ya ndege ya Air Tanzania na kitambulisha mada #WakwanzaAfrika, kuashiria kwamba shirika hilo litakuwa la kwanza Afrika kupokea ndege aina ya Airbus A220-300.


"Sikuchelewa ndege Kabisa..Nilifika muda sawia kama usafiri wa ndege za ndani unavyotaka, na kulidhihirisha hilo.. nikiwa niko pale kuna hata abiria wengine waliingia nusu saa baadae, tena nikiwepo nimesimama palepale..." ameandika kwenye Instagram.

Haki miliki ya pichaFACEBOOK/DIAMOND PLATINUMZImage captionDiamond Platinumz

".. na mmoja ya watu waloingia nikiwepo nimesimama ni @Harmonize_tz ..."

"Kilichotokea ni kuwa Mmoja ya watu wenye dhamana pale, siti zetu (viti vyetu) aliziuza kwa abilia (abiria) wa fastjet...kwa abiria watalii wazungu, na walichokuwa hawajajua pia waliwauzia na baadhi ya watu ambao ni wafanyakazi wetu wa Wasafi Media..."


"Na Kuthibitisha tena kuwa hatukuchelewa, alikuja tena mtu wa Air Tanzania na kutuambia kuwa siti zimebaki mbili...Hivyo tuchague watu wawili tu wasafiri....

"Kama kweli tulichelewa, sasa hao wawili, sasa wangewezaje ingia??? tukasema hatuwezi safiri wawili lazima tuwe wote kama tulivyokata... hivyo ni dhahiri kuwa hatukuchelewa....ila kutokana na Ndege nyingi za kuja mwanza zilicancel trip zao, ikiwepo Fastjet hivyo tickets zikawa ni dili sana na ndio yote kutokea...."

Ametetea msimamo wake na kusema ā€ž kama Mtanzania Mzalendo Mwenye akili Timamu, siwezi tu kukurupuka kusema jambo kwani ni jukumu langu kuhakikisha nalilinda shirika hili."

"Nikiwa kama Mtanzania mwenye uchungu siwezi kuona mtu alopewa dhamana ya kuzisimamia ndege hizo anafanya vitu tofauti halafu eti nikakaa kimya..."

Harmonize, mwanamuziki mwenzake, ameandika maoni kwenye ujumbe wa Diamond na kusema 'Fact', kwa Kiingereza kwa maana ya kweli kabisa.

ATCL wanasema nini kilitokea?

Kwa mujibu wa shirika hilo la ndege, abiria Issaack Nasib aliyekuwa na tiketi namba- 197 2400458865 ya kampuni ya ndege ya Tanzania alikuwa katika safari ya kutoka Mwanza kwenda Dar Es Salaam, ndege nambari TC103 ya jioni tarehe 16 Disemba 2018. Kwa kawaida shirika hilo linasema abiria hutakiwa kufika uwanjani masaa mawili kabla ya ndege kuruka.

ATCL wanasema afisi yao ya Mwanza ilifungua dirisha kwa ajili ya kuwahudumia wateja (wasafiri) majira ya 17:45 na kulifunga majira ya 20:00.

Ndege hiyo iliruka kutoka Mwanza kuja Dar Es Salaam majira ya saa 20:45 na kuwasili Dar Es Salaam saa 22:00.

"Kwa kumbukumbu zilizopo kwa kutumia vyanzo mbalimbali, zikiwemo Camera (CCTV) za uwanjani inaonekana abiria tajwa hapo juu alifika majira ya 20:15 ambapo dirisha lilikuwa limeshafungwa. "

Bw Kagirwa, akizungumza na wanahabari alisema: "Tiketi ya mteja haiwezi kuuzwa. Ila asipoonekana uwanjani na akawepo mtu mwingine anahitaji huduma tutampa nafasi maana nafasi katika ndege thamani yake inaisha ndege inaporuka lakini tiketi baada ya hapo inabadilishwa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...