Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Droo UEFA na Europa League hii hapa


Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya England Manchester City wamepangiwa kucheza na klabu ya Schalke ya Ujerumani katika hatua ya 16 bora Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya baada ya droo kufanywa.

Manchester United wamekabidhiwa miamba wa Ufaransa Paris Saint Germain.


Mabingwa hao watetezi wa ubingwa Ufaransa hawajashindwa msimu huu ligini nyumbani ambapo wanaongoza wakiwa na alama 44 kutoka mechi 16. Wana washambuliaji nyota kama vile Neymar, Kylian Mbappe na Edison Cavani.

Walimaliza viongozi Kundi C, kundi ambalo lilikuwa na Liverpool, Napoli na Red Star Belgrade katika hatua ya makundi.

Lakini walishindwa na Liverpool uwanjani Anfield.


United hawajawahi kukutana na Paris St-Germain katika michuano ya Ulaya.

Hata hivyo, mashetani hao wekundu hawajawahi kushinda na klabu yoyote kutoka Ufaransa katika michuano ya Ulaya tangu mwaka 2005.

Droo kamili:

Manchester United v PSG


Schalke v Manchester City


Atletico Madrid v Juventus


Tottenham v Borussia Dortmund


Lyon v Barcelona


Roma v Porto


Ajax v Real Madrid


Liverpool v Bayern Munich


Kwa mashabiki wengi wa Manchester City, wanaonekana kufurahia kukabidhiwa Schalke, ambao kwa kuangalia viwango vya soka ilikuwa ndiyo klabu 'hafifu' zaidi ambayo wangekabidhiwa.

Schalke wamo nafasi ya 13 Bundesliga na wameshinda mechi nne pekee kati ya 15.

Schalke walimaliza wa pili Kundi D nyuma ya Porto lakini mbele ya Galatasaray na Lovomotiv Moscow.

Tofauti na Manchester United na PSG ambao hawajawahi kukutana, Manchester City wamekutana na Schalke awali.

Mara ya karibuni zaidi walikutana Gelsenkirchen mwaka 2008 si muda mrefu baada yao kununuliwa na Sheikh Mansour.

City walishinda mechi hiyo ya hatua ya makundi Europa League kwa mabao 2-0, mabao yao wakifungiwa na Benjani na Stephen Ireland.

Mechi za kwanza zitachezwa 12-13 na 19-20 Februari, na mechi za marudiano 5-6 na 12-13 Machi, 2019.

Katika Europa League, Arsenal wamepangiwa kucheza na Bate Borisov ya Belarus, nao Chelsea - walioshinda kombe hilo mwaka 2013 - wakapewa Malmo ya Sweden.

Mechi hizo nyingi yazo zitachezwa kati ya 14 na 21 Februari 2019.

Arsenal watacheza mechi yao ya marudiano mnamo 20 Februari.

Droo ya Europa League 32 bora

Viktoria Plzen v Dinamo Zagreb


Club Brugge v Red Bull Salzburg


Rapid Vienna v Inter Milan


Slavia Prague v Genk


Krasnodar v Bayer Leverkusen


FC Zurich v Napoli


Malmo v Chelsea


Shakhtar Donetsk v Eintracht Frankfurt


Celtic v Valencia


Rennes v Real Betis


Olympiakos v Dinamo Kiev


Lazio v Sevilla


Fenerbache v Zenit St Petersburg


Sporting Lisbon v Villarreal


Bate Borisov v Arsenal


Galatasaray v Benfica


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...