Droo UEFA na Europa League hii hapa


Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya England Manchester City wamepangiwa kucheza na klabu ya Schalke ya Ujerumani katika hatua ya 16 bora Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya baada ya droo kufanywa.

Manchester United wamekabidhiwa miamba wa Ufaransa Paris Saint Germain.


Mabingwa hao watetezi wa ubingwa Ufaransa hawajashindwa msimu huu ligini nyumbani ambapo wanaongoza wakiwa na alama 44 kutoka mechi 16. Wana washambuliaji nyota kama vile Neymar, Kylian Mbappe na Edison Cavani.

Walimaliza viongozi Kundi C, kundi ambalo lilikuwa na Liverpool, Napoli na Red Star Belgrade katika hatua ya makundi.

Lakini walishindwa na Liverpool uwanjani Anfield.


United hawajawahi kukutana na Paris St-Germain katika michuano ya Ulaya.

Hata hivyo, mashetani hao wekundu hawajawahi kushinda na klabu yoyote kutoka Ufaransa katika michuano ya Ulaya tangu mwaka 2005.

Droo kamili:

Manchester United v PSG


Schalke v Manchester City


Atletico Madrid v Juventus


Tottenham v Borussia Dortmund


Lyon v Barcelona


Roma v Porto


Ajax v Real Madrid


Liverpool v Bayern Munich


Kwa mashabiki wengi wa Manchester City, wanaonekana kufurahia kukabidhiwa Schalke, ambao kwa kuangalia viwango vya soka ilikuwa ndiyo klabu 'hafifu' zaidi ambayo wangekabidhiwa.

Schalke wamo nafasi ya 13 Bundesliga na wameshinda mechi nne pekee kati ya 15.

Schalke walimaliza wa pili Kundi D nyuma ya Porto lakini mbele ya Galatasaray na Lovomotiv Moscow.

Tofauti na Manchester United na PSG ambao hawajawahi kukutana, Manchester City wamekutana na Schalke awali.

Mara ya karibuni zaidi walikutana Gelsenkirchen mwaka 2008 si muda mrefu baada yao kununuliwa na Sheikh Mansour.

City walishinda mechi hiyo ya hatua ya makundi Europa League kwa mabao 2-0, mabao yao wakifungiwa na Benjani na Stephen Ireland.

Mechi za kwanza zitachezwa 12-13 na 19-20 Februari, na mechi za marudiano 5-6 na 12-13 Machi, 2019.

Katika Europa League, Arsenal wamepangiwa kucheza na Bate Borisov ya Belarus, nao Chelsea - walioshinda kombe hilo mwaka 2013 - wakapewa Malmo ya Sweden.

Mechi hizo nyingi yazo zitachezwa kati ya 14 na 21 Februari 2019.

Arsenal watacheza mechi yao ya marudiano mnamo 20 Februari.

Droo ya Europa League 32 bora

Viktoria Plzen v Dinamo Zagreb


Club Brugge v Red Bull Salzburg


Rapid Vienna v Inter Milan


Slavia Prague v Genk


Krasnodar v Bayer Leverkusen


FC Zurich v Napoli


Malmo v Chelsea


Shakhtar Donetsk v Eintracht Frankfurt


Celtic v Valencia


Rennes v Real Betis


Olympiakos v Dinamo Kiev


Lazio v Sevilla


Fenerbache v Zenit St Petersburg


Sporting Lisbon v Villarreal


Bate Borisov v Arsenal


Galatasaray v Benfica


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

ZIJUWE SHERIA 17 ZA SOKA

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

KUMTUMAINIA MUNGU