Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Idadi ya vifo vilivyotokana na kimbunga Idai yaongezeka kwa kasi nchini Msumbiji



Wafanyakazi wa shirika la uokoaji wakiwa wanajiandaa kuondoa miili kutoka kwenye helikopter

Idadi ya waliopoteza maisha kutokana na kimbunga Idai kilichoikumba eneo la kusini mwa Afrika zaidi ya juma moja lililopita,imeongezeka kwa kasi siku ya Jumamosi.

Idadi ya waliothibitishwa kupoteza maisha nchini Msumbiji imeongezeka kutoka 242 mpaka 417,waziri wa ardhi na mazingira nchini humo Celso Correia ameeleza.

Idadi hii mpya inafanya waliopoteza maisha Msumbiji, Zimbabwe na Malawi kufikia 700.

Idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka zaidi.

Kimbunga kimeua takribani watu 259 nchini Zimbabwe na Malawi 56.Watu walipoteza maisha kutokana na mvua kubwa iliyonyesha na kusababisha mafuriko.

Lakini Umoja wa mataifa limesema maafisa wataweza kutathimini madhara pale maji yatakapopungua.


Maelfu ya watu wakiwa wanasubiri kuokolewa kutoka kwenye maeneo yaliyokumbwa na mafuriko kusini mwa Afrika

Ofisi ya Umoja wa mataifa inayoshughulikia masuala ya kibinaadamu, OCHA imesema kuwa mto wa Buzi na Zambezi iko kwenye hatari ya kuvujika kingo zake kwa mara nyingine.

''Tutasubiri mpaka maji yaliyotokana na mafuriko yaishe kisha tutafahamu kwa hakika kuhusu idadi ya waliopoteza maisha nchini Msumbiji.Mratibu wa OCHA Sebastian Rhodes Stampa alieleza.

Maelfu wamenasa kutokana na mafuriko, na vituo vingi vya uokoaji vya nchini Msumbuji vimeanza kupokea vyakula.

Watu takriban milioni 1.7 wameathirika kusini mwa Afrika, wakiwa hawana umeme, na maji hasa kwenye maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga hicho.

'Kimbunga kibaya' kuwahi kushuhudiwa kimetua Msumbiji

Kimbunga Idai huenda kikaathiri mvua Afrika mashariki

Siku ya Ijumaa, ilielezwa kuwa kumetokea mlipuko wa maradhi ya kipindupindu mjini Beira, katikati mwa Msumbiji.Shirika la Msalaba mwekundu lilionya hatari ya kutokea maradhi mengine ya mlipuko, huku tayari kukiwa na taarifa ya mlipuko wa maradhi ya malaria.

Wafanyakazi wa mashirika ya misaada wanawasilisha misaada taratibu lakini wakikabiliwa na changamoto ya kuwafikia wengine walio kwenye maeneo yasiyofikika huku vyombo vya anga vya kupeleka misaada vikielezwa kuwa vichache.

Makundi ya watoa misaada nchini Msumbiji yanasema kuwa takriban watu 90,000 wanaishi kwenye maeneo ya muda mfup, huku maelfu wengine bado wakiwa kwenye maeneo yaliyofurika kutokana na mvua.Shirika la Habari la Ufaransa limeripoti

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...