CIA yatoa faili 470,000 za Osama Bin Laden


Shirika la ujasusi la Marekani CIA limetoa karibu faili 470,000 zilizopatikana wakati wa kuuawa kwa aliyekuwa kiongozi wa al-Qaeda Osama Bin Laden mwaka 2011.
Faili hizo mpya ni pamoja na stakabadhi kuhusu mipango yake binafsi na video ya mtoto wake wa kiume Hamza wakati wa hasuri yake.
Marekani kumsaka mtoto wa Osama
Makamando wa Marekani wavamia al-Qaeda Yemen
Hii ndiyo mara ya nne CIA inatoa faili za Osama zilizopatikana wakati wa uvamizi kwenye maficho yake huko Abbottabad nchini Pakistan.
Hata hivyo faili zingine haziwezi kutolewa kwa sababu zinaweza kuathiri usalama wa tiafa.
Kulingana na CIA faili hizo zinafichua uhusiano uliopo sasa kati ya al-Qaeda na ISIS na migawanyiko kati ya al-Qaeda na washirika wake.
Kampiuta iliyopataiaka wakati wa uvamizi huo ilikuwa na filamu za Hollywood, vipindi vya watoto na makala tatu kumhusu Osama Bin Laden.
Mwana wa Osama bin Laden asakwa na Marekani
Video nyingine ni ya harusi na mtoto wa Osama, Hamza Bin Laden akiwa mdogo. Hamza Bin Laden sasa ana umri wa miaka ya 20 licha ya mahali aliko sasa kutojulikana.
Stakabadhi za awali zilionyesha kwa Bin Laden alikuwa akimundaa mtoto wake huyo kumridhi kama kiongozi wa al-Qaeda.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

ZIJUWE SHERIA 17 ZA SOKA

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

KUMTUMAINIA MUNGU