Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Serikali Uganda yaondoa mashtaka ya uhaini dhidi ya Bobi Wine

Wine alifikishwa katika mahakama ya jeshi mjini Gulu ambapo maamuzi hayo yalitolewa baada ya serikali kumshtaki kwa kumiliki bunduki kinyume cha sheria


- Kuachiliwa huru kwake kwa muda kuliwadia baada ya shinikizo tele kutoka kwa raia na hali tete kuendelea kushuhudiwa nchini Uganda


- Wine alikamatwa tena mara baada ya kuachiliwa huru na kuwasilishwa katika mahakama ya raia na sasa ataendelea kuiziliwa hadi Agosti 30, 2028


Serikali nchini Uganda imeondoa mashtaka ya uhaini dhidi ya Mbunge wa Kyadondo Mashariki Robert Kyagulanyi, almaarufu Bobi Wine, kufuatia hali tete na ghasia zilizoshuhudiwa nchini humo kutoka kwa raia waliotaka aachiliwe huru.


Wine, ambaye amekuwa kizuizini kwa muda wa wiki moja sasa, alipewa uhuru huo wa muda katika mahakama ya jeshi mjini Gulu, Alhamisi, Agosti 23, na kukamatwa tena.




Maandamano yamekuwa yakishuhudiwa maeneo mbalimbali nchini Uganda na pia Kenya yakilenga kuishinikiza serikali ya Uganda kumwachilia huru Bobi Wine. Picha: NTV Uganda.



TUKO.co.ke imethibitisha mwanasiasa huyo mwasi dhidi ya serikali ya Raia Yoweri Museveni, alikamatwa mara baada ya kuachiliwa huru na kuwasilishwa katika mahakama ya raia, licha ya wafuasi na wakili wake kulalamika.


ā€œHamna sababu yoyote ya kusema Kyagulanyi anatafutwa na polisi ama kuna mashtaka yoyote dhidi yake. Naomba usiifanye korti hii kuwa korti ya kukamata na kumpa Mhe Kyagulanyi uhuru wake,ā€ wakili wa Wine, Medard Ssegona alisema.




Hali ya maandamano na ghasia imeshuhudiwa nchini Uganda tangu kakamatwa kwake wiki moja iliyopita na kumekuwapo na madai kuwa, Wine aliteswa akiwa korokoroni.


Mwanasiasa huyo anayempa wakati mgumu Museveni, alikamatwa kwa madai ya kuhusika na ghasia zilizosababisha msafara wa rais kupigwa mawe mjini Arua, Kaskazini mwa Uganda.




Museveni alikuwa Arua akimpigia debe mwaniaji wa chama chake Nusura Tiperu, wakati Bobi Wine alipokuwa akimpigia kampeini mwaniaji Huru, Kassiano Wadri, na ghasia zikazuka. Polisi walifyatua risasi na kumuua dereva wa Wine na watu wengine watano.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...