Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mwaka mchungu na mtamu kwa Diamond



Toka mwaka 2009 hadi sasa Diamond Platnumz amekuwa akifanya vizuri kimuziki na kipindi chote hicho ameweza kushinda tuzo za ndani na za kimataifa pia. Kabati lake lina tuzo kubwa zaidi ya 10 kama Channel O Music Video Awards, HiPipo Music Awards, MTV Europe Music Awards/WORLDWIDE ACT AFRICA/INDIA, MTV Africa Music Awards, African Muzik Magazine Awards (AFRIMMA) na nyinginezo. 

Kwa mwaka huu amefanya mengi makubwa na mazuri ingawa amekuwa na changamoto kubwa kwake.Chini nimeweka yale aliyofanikiwa na yale yalimpatia changamoto kwa huu. 

1. Muziki Wake 

Ni mwaka ambao Diamond Platnumz amejikuta nyimbo zake tatu zikifungiwa na Baraza la Sanaa Taifa (BASATA). Diamond hakuwa msanii wa kufungiwa lakini mwaka huu upepo huo umempuliza vilivyo. 

February 28, 2018 Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ilipokea orodha ya nyimbo 15 zisizokuwa na maadili kutoka kwa Baraza la Sanaa Taifa (BASATA). Nyimbo hizo ni zile ambazo hazikupaswa kuchezwa kwenye vyombo vya habari. 

Katika orodha hiyo zilikuwepo nyimbo mbili za Diamond ambazo ni Waka aliyomshirikisha Rick Ross, pamoja na Hallelujah ambayo amewashirikisha Morgan Heritage kutoka nchini Jamaica. 

Tukija hadi November 12, 2018 wimbo 'Mwanza' wa Rayvanny alioshirikiana na Diamond ulifungiwa na Basata na kuamuriwa kutolewa Youtube kabisa, pia wasanii hao wametozwa faini ya Tsh. Milioni 9. Hivyo kufanya nyimbo zake tatu kwa mwaka huu kutupwa jela ya kimuziki. 

Pia ni mwaka huu ambao kwa mara ya kwanza msanii wa kwanza ameondoka kwenye lebo yake ya WCB. Rich Mavoko ambaye alisaini kuwa chini ya lebo hiyo June 2, 2016 na wimbo wake wa kwanza kutoa ulikwenda kwa jina la Ibaki Stori. 

Baada ya miaka miwili Rich Mavoko ameamua kuondoka hapo na kwenda kuanzisha lebo yake ya Bilione Kid. Kuondoka kwa Rich Mavoko kumefanya WCB kusaliwa na wasanii watano ambao ni Harmonize, Rayvanny, Mbosso, Lava Lava na Queen Darleen. 

2. Mahusiano 

Huu ni mwaka ambao mahusiano ya Diamond yameripotiwa zaidi kwenye vyombo vya habari, hii ni kutokana na kuachana na wazazi wenzake wawili, Zari The Bosslady na Hamisa Mobetto. 

Siku ya wapendanao (Valentineā€™s Day) February 14, 2018 Zari The Boss Lady alitangaza rasmi kuachana na Diamond kutokana na kuchoshwa na habari za kusalitiwa ambazo husikika kila siku  katika vyombo vya habari. 

"There have been multiple rumors some with evidence floating around in ALL SORTS of media in regards to Diamondā€™s constant cheating and sadly I have decided to end my relationship with Diamond, as my RESPECT, INTEGRITY, DIGNITY & WELL BEING cannot be compromised," taarifa ya Zari ilieleza. 

Hatua hiyo ilikuja baada ya September 19, 2017 Diamond kukiri kuzaa na Mwanamitindo Hamisa Mobetto licha ya kukanusha na kufanya siri kwa kipindi kirefu. 

3. Biashara  

Kwa mwaka huu kwa mara ya kwanza Diamond ameweza kutimiza ndoto yake ya kumiliki vyombo vya habari (Wasafi TV & Radio) na kuwa msanii wa kwanza wa Bongo Fleva kufanya hivyo. 

Hatua hiyo inatafsiriwa kama mwanzo wa wasanii kuanza kujikwamua kutoka kwenye 'siasa' zilizokuwa zikiendelea kwenye baadhi ya vyombo vya habari kwa kucheza baadhi ya nyimbo za wasanii kwa upendeleo na wengine kutopewa nafasi kabisa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...