Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Sababu zilizochangia benki tano kupigwa marufuku ya kubadilisha fedha za kigeni Tanzania




Noti za Tanzania

Benki Kuu ya Tanzania imezipiga benki tano marufuku ya kuendesha biashara ya sarafu za kigeni kwa muda wa mwezi mmoja kwa kukiuka sheria kwa mujibu wa maafisa wa vyeo vya juu.

Marufuku hiyo inakuja baada ya Benki Kuu kufanya ukaguzi wa ghafla kwenye maduka ya kubadilisha fedha za kigeni kwenye mji ulio kaskazini wa Arusha kituo cha utalii na bishara ya madini.

Kwa sasa kuna zaidi ya benki 40 zinazotoa huduma kwenye taifa hilo la Afrika Mashariki.

Kwa nini zimepigwa marufuku?

Benki ya Barclays Tanzania, Exim Bank, UBA Bank, BancABC na Azania Bank zote zilipigwa marufuku ya kuendesha biashara hiyo Novemba 23 kwa kukiuka sheria za biashara, kwa mujibu wa Alexander Ng'winamila, mkurugenzi wa masoko ya fedha katika benki kuu.

"Benki zilizopigwa marufuku aidha zilifanya biashara nje ya viwango vya masoko au hazikuwasilisha kwa Benki Kuu rrekodi za biashara zao, suala ambalo ni kinyume na sheria," Ng'winamila aliliambia shirika la Reuters.



Barclays Tanzania ambayo ni sehemu ya beki ya Afrika Kusini Absa, ilithibitisha marufuku hiyo na kuongeza kuwa ilikuwa inashirikiana na benki kuu kutatua suala hilo.

Benki zimesema nini?

Gilbert Mwandimila, mkurugenzi wa biashara kwenye benki ya Azania amesema changamoto za teknolojia zilichangia kuchelewa kwa ripoti kuhusu biashara ya fedha.

Alisema marufuku ya mwezi mzima itaathiri pakubwa uwezo wa benki kuhudumia wateja.

Stanley Kafu, mkuu wa masoko na mawasiliano Benki ya Exim Tanzania, aliiambia Reuters kuwa marufuku ya benki ya Exim inahusu biashara kati ya dola ya Marekani na shilingi ya Tanzania pekee.

"Tumeruhusiwa kufanya biashara ya sarafu zingine kuu na pia tunaruhusiwa kuendelea na huduma zingine za benki," alisema.

Thamani ya shilingi ya Tanzania dhidi ya dola

Thamani ya shilingi ya Tanzania dhidi ya dola ya Marekani imezidi kuporomoka na kufikia kiwango cha chini zaidi katika miaka mitatu iliyopita.

Dola moja kwa sasa ni wastani wa Sh2,300 mara ya mwisho kwa kiwango hicho kufikiwa ilikuwa ni Julai 2015 ambapo Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliingilia kati.

Mkurugenzi wa Masoko na Fedha wa BoT Alexander Mwinamila aliliambia Gazeti la The Citizen la Tanzania kuwa kuporomoka huko kwa thamani ya shilingi kulitarajiwa.

"Hali ya sasa si kitu cha kustaajabisha, na kwa kiasi imechangiwa na kuimarika kwa dola dhidi ya sarafu nyengine kwa siku za hivi karibuni."

Sababu nyingine zinazotajwa kuchangia kuporomoka huko kwa thamani ya shilingi dhidi ya dola ni kushuka kwa mauzo ya bidhaa nje ya nchi na kuingia kwa fedha za kigeni kutoka kwenye miradi ya wawekezaji.

Hata hivyo, wakati shilingi ikishuka, tarehe 19 Novemba mwaka huu katika hali isiyokuwa ya kawaida, wanajeshi walitanda kwenye maduka ya kubadilishia fedha jijini Arusha.

Hali iliyowafanya baadhi ya wananchi washindwe kufanikisha biashara waliyokusudia

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...