Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Rais George H.W. Bush afarikia dunia


Aliyekuwa Rais wa 41 wa Marekani George H.W. Bush amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 94 huko mjini Houston, msemaji wake Jim McGrath amethibitisha kifo chake.

George H.W. Bush


Rais huyo wa zamani wa Marekani aliongoza kwa awamu moja tu akiingia madarakani mwaka 1989 na kuondoka 1993 hivyo kubaki kama Rais pekee aliyeiongoza Marekani kwa awamu moja.

Chanzo cha kifo cha George Bush hakijawekwa wazi rasmi, lakini Rais huyo mstaafu wa Marekani, kwa muda mrefu alikuwa akipambana na ugonjwa wa 'Vascular Parkinsonism', na kifo chake kimetokea ikiwa imepita miezi michache tangu mke wake Barbara Bush afariki dunia mnamo April 17, 2018 baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Taarifa zaidi zinasema kwamba George Bush alikumbwa na ugonjwa huo tangu miaka ya 90, na mwenyewe aliwahi kuulezea kuwa ni ugonjwa mzuri kuupata kwani haumuumizi, isipokuwa tu anashindwa ku-'move' pale anapotaka hata kunyanyua mguu. 

"Unaathiri miguu, hauumii, unaiambia miguu yako ijongee na haijongei, ni ajabu, lakini iwapo una ugonjwa mbaya, huu ni mzuri kuwa nao", alinukuliwa George Bush akizungumza alipokuwa akihojiwa na jarida la Parade mwaka 2012.

Kwenye maisha yake George Bush ameweka historia ya kuwa waziri Mkuu wa kwanza ambaye alikuwa madarakani kuchaguliwa kuwa Rais, na mtu wa pili kwenye utawala wa Marekani kushuhudia mtoto wake akichukua wadhifa huo, baada ya mtoto wake George Walker Bush kuwa Rais wa 43 wa Marekani.

George Bush alizaliwa huko Massachusetts Juni 12, 1924, akiwa mtoto wa tajiri na mfanyakazi wa Benki ya Wall Street na Senetor wa jimbo la Connecticut, Prescott Bush na mke wake Dorothy Bush.

George Bush ameacha watoto watano wakiwemo aliyekuwa Rais wa 43 wa Marekani, George Walker Bush, Jeb Bush, Dorothy Bush Koch ambaye ndiye mtoto wake wa kike pekee aliyebaki, baada ya mdogo wake Pauline Robinson Bush kufariki dunia akiwa na miaka minne, Neil Bush na Marvin Bush.

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...