Putin Azungumuzia shambulio la kigaidi New Zealand


Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema kuwa sababu kuu ya shambulizi la misikiti miwili New  Zealand ni kuitikisa nchi hiyo


Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema kuwa sababu kuu ya shambulizi la misikiti miwili New  Zealand ni kuitikisa nchi hiyo.


Katika mkutano wake na wawakilishi wa jamii katika Crimea na Sevastopol, Putin amejadili mashambulizi ya kigaidi juu ya misikiti huko New Zealand.

Putin alionyesha heshima yake kwa wale waliouawa katika shambulio hilo.

"Lengo la mashambulizi makubwa ya kigaidi huko New Zealand ni kuitingisha nchi." alisema.

Akionyesha kuwa vitendo vya kigaidi ni hatari kwa kila nchi, Putin amesema kuwa Urusi haitaruhusu mashambulizi hayo.

Katika mji wa Christchurch, New Zealand, wakati wa sala ya Ijumaa, watu 50 waliuawa na gaidi aliyoshambulia misikiti miwili.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

ZIJUWE SHERIA 17 ZA SOKA

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

KUMTUMAINIA MUNGU