Maandamano ya kumuunga mkono Morales





Mamia ya waandamanaji walikusanyika katika ubalozi wa Bolivia nchini Argentina wakimuunga mkono Evo Morales





Mamia ya watu nchini Argentina wameandamana kuonyesha kumuunga mkono Evo Morales  Rais wa Bolivia aliyelazimisha na jeshi la nchi hiyo kujiuzulu.



Raia wa Bolivia wanaoishi nchini Argentina kwa uratibu wa asasi za kiraia zenye mrengo wa kushoto walikusanyika mbele ya ubalozi wa Bolivia nchini Argentina.

Waandamanaji hao walilaani hila alizofanyiwa Rais Morales katika uchaguzi na baada ya uchaguzi na kutolea wito jamii la kimataifa kumuunga mkono Morales.

Waandamanaji hao walibeba mabongo yenye ujumbe kama “Hatutaki mapinduzi Bolivia” pia walikuwa wakipeperusha bendera yenye rangi 7 inayowakilisha wakazi wa  eneo la milima ya Andes pamoja na bendera za Bolivia.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

ZIJUWE SHERIA 17 ZA SOKA

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

KUMTUMAINIA MUNGU