Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Msuva, Sure boy , Samatta moto wao nimkali

Sure Boy aipa Taifa Stars kuvuna alama tatu katika mchezo wa kusaka tiketi ya kushiriki fainali za Afcon 2021 baada ya kuifunga Guinea ya Ikweta mabao 2-1.

Mchezo huo uliopigwa Uwanja wa Taifa ulishuhudiwa  Stars wakiutawala kwa asilimia kubwa lakini iliweza kujikuta ikienda mapumziko ikiwa nyuma bao 1-0.

Mchezo huo ulianza kwa kasi kwa wenyeji kuutawala kutokana na mashambulizi yaliyokuwa yakifanywa na nahodha wa  Stars, Mbwana Samatta aliyekuwa akisaidiana na Simon Msuva kuliandama lango la wapinzani.

Samatta alikosa kuiandikia bao Stars dakika ya pili baada ya mpira wake kuokolewa na Mlinda mlango wa Felipe Ovono ambaye alionesha umahiri wake wa kuokoa michomo.

Wakati vijana hao wa Kocha, Etienne Ndayiragije wakiendelea kulisakata soka mbele ya watazamaji waliojitokeza kwa wingi kutoa sapoti, walijikuta wakiruhusu bao dakika ya 15 lililofungwa na Petro Obiang ambalo lilidumu hadi mapumziko.

Hata hivyo Samatta alikosa nafasi nyingne ya kuisawazishia Stars dakika ya 40 lakini, Ovono aliweza kuzuia hatari hiyo langoni mwake na kuonekana kuwa kwenye ubora katika mchezo huo.

Kipindi cha pili kilianza kwa Stars, kumtoa Hassan Kessy na nafasi yake kuchukuliwa na Ditram Nchimbi mabadiliko ambayo yalimfanya, Samatta kuwa huru katika uchezaji wake na yalifanikiwa kusawazisha bao.


Bao la Stars lilifungwa na  Simon Msuva dakika 68 baada ya kumzidi ujanja kipa wa Guinea ambaye muda mwingi alionekana kuwa kinara wa kuizuia Stars kufunga na hadi dakika za nyongeza, Sure Boy alipoachia shuti kali lililozama nyavuni na kuipa ushindi Stars mabao 2-1.


Kikosi kilichanza cha Stars kilikuwa na Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Kelvin Yonda, Hassan Kessy, Bakari Mwamnyeto, Salum Abubakar, Mbwana Samatta, Simon Msuva, Mohamed Hussein, Farid Mussa na Mzamiru Yassin.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...