Sure Boy aipa Taifa Stars kuvuna alama tatu katika mchezo wa kusaka tiketi ya kushiriki fainali za Afcon 2021 baada ya kuifunga Guinea ya Ikweta mabao 2-1.
Mchezo huo uliopigwa Uwanja wa Taifa ulishuhudiwa Stars wakiutawala kwa asilimia kubwa lakini iliweza kujikuta ikienda mapumziko ikiwa nyuma bao 1-0.
Mchezo huo ulianza kwa kasi kwa wenyeji kuutawala kutokana na mashambulizi yaliyokuwa yakifanywa na nahodha wa Stars, Mbwana Samatta aliyekuwa akisaidiana na Simon Msuva kuliandama lango la wapinzani.
Samatta alikosa kuiandikia bao Stars dakika ya pili baada ya mpira wake kuokolewa na Mlinda mlango wa Felipe Ovono ambaye alionesha umahiri wake wa kuokoa michomo.
Wakati vijana hao wa Kocha, Etienne Ndayiragije wakiendelea kulisakata soka mbele ya watazamaji waliojitokeza kwa wingi kutoa sapoti, walijikuta wakiruhusu bao dakika ya 15 lililofungwa na Petro Obiang ambalo lilidumu hadi mapumziko.
Hata hivyo Samatta alikosa nafasi nyingne ya kuisawazishia Stars dakika ya 40 lakini, Ovono aliweza kuzuia hatari hiyo langoni mwake na kuonekana kuwa kwenye ubora katika mchezo huo.
Kipindi cha pili kilianza kwa Stars, kumtoa Hassan Kessy na nafasi yake kuchukuliwa na Ditram Nchimbi mabadiliko ambayo yalimfanya, Samatta kuwa huru katika uchezaji wake na yalifanikiwa kusawazisha bao.
Bao la Stars lilifungwa na Simon Msuva dakika 68 baada ya kumzidi ujanja kipa wa Guinea ambaye muda mwingi alionekana kuwa kinara wa kuizuia Stars kufunga na hadi dakika za nyongeza, Sure Boy alipoachia shuti kali lililozama nyavuni na kuipa ushindi Stars mabao 2-1.
Kikosi kilichanza cha Stars kilikuwa na Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Kelvin Yonda, Hassan Kessy, Bakari Mwamnyeto, Salum Abubakar, Mbwana Samatta, Simon Msuva, Mohamed Hussein, Farid Mussa na Mzamiru Yassin.
Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi. Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria. Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao. Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...
Maoni