Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Bakwata yarejesha kiwanja chake, Waislamu kupiga dua maalum kuishukuru Mahakama


BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) mkoa wa Mwanza limerejesha umiliki wa kiwanja namba 111 kitalu T kilichopo Kenyatta Road jijini hapa kwenye eneo maarufu la 'Muslim' (ilipo stendi ya Igombe) kilichokuwa kimechukuliwa na halmashauri ya Jiji la Mwanza.

 
Bakwata imerejesha umiliki huo baada ya kushinda kesi kufuatia halmashauri ya Jiji la Mwanza kushindwa kutimiza masharti iliyopewa na mahakama.
 
Shauri hilo namba 150 ya mwaka 2020 lililotokana na kesi namba 58 ya mwaka 2017 liliamuliwa Juni 3, 2022 ambapo Mahakama ilithibitisha kwamba kiwanja hicho ni mali halali ya Bakwata.
 
Akitoa taarifa kwa umma wa kiislam leo Juni 5, 2023 wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Bakwata jijini Mwanza, Sheikh wa Mkoa wa Mwanza, Hasani Kabeke amesema katika uamuzi wake mahakama ilitoa masharti mawili kwa halmashauri ya Jiji ikitakiwa kulipa fidia ili kukitwaa kiwanja hicho ama irudishe kiwanja hicho kama fidia itashindwa kufikiwa ndani ya miezi mitatu, ambapo halmashauri hiyo ilishindwa kutekeleza yote mawili hadi leo Juni 5, 2023.
 
Amesema kiwanja hicho ni sehemu ya mali zilizokuwa zinamilikiwa na East Africa Welfare Society ambazo baadae zilihamishiwa Bakwata, ambapo Baraza hilo litaendesha dua maalum Juni 7, mwaka huu saa 4 asubuhi kupongeza maamuzi ya mahakama, kumuombea Rais Samia Suluhu Hassan na wazee waliotoa maeneo hayo kwa ajili ya jamii ya kiislamu.
"Tunajua ni wajibu wa mahakama kutenda haki lakini tunashukuru ili kutimiza maelekezo ya mtume wetu na kupaza sauti kuiombea mahakama Mungu awape uimara katika kuwatendea haki Watanzania kama ilivyofanya kwetu," amesema Kabeke
Kwa upande wake, Mhasibu wa baraza hilo, Said Mrisho amesema mahakama iliipa halmashauri ya Jiji la Mwanza sharti la kulipa fidia ya Sh 539 milioni kama inataka kutwaa eneo hilo baada ya uthamini kufanyika lakini imeshindwa kufanya hivyo, ambapo sasa litaendelea kuwa mali ya Bakwata.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...